Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa.
1.Kwanza kabisa watoto wadogo wanapaswa kuwa karibu sana na walezi wao ili waweze kupata huduma muhimu na za msingi kwa hiyo mtoto akiwa mgonjwa na akaleta hospitalini Mama au mlezi wanapaswa kupewa maelekezo yafuatayo ili kuweza kuwafanya wampatie Mtoto dawa sahihi na kwa wakati wake.
2. Kwanza mama au mlezi wanapaswa kujua dozi na dawa ipi mtoto anapaswa kupewa, na pia wanapaswa kuambiwa wazi sababu ya kupewa dawa hizo, kwa hiyo akina mama wakiwa wanaenda hospitalini ni muhimu kuuliza sababu ya kupewa dawa, mtoto anapaswa kupata dozi ipi na kwa mda gani kwa hiyo ni haki kuuliza na kupewa jibu.
3. Pia Mama anapaswa kuonyeshwa kwa vitendo namna ya kumpatia mtoto dawa na pia ikiwezekana anaweza nkujarubisha akiwa anaangaliwa na kama mtoto hajapewa dawa dozi ya kwanza inaweza kutolewa ili kumfanya Mama aweze kupata uzoefu wakati wa kutoa dawa.
4. Na kama dawa ni zaidi ya moja ni lazima kuziweka alama ili zisije kuchanganywa na pia mama anapaswa kujua kuwa lazima dawa zitolewe kwa mtoto mpaka ziishe hata kama mtoto amepona kwa hiyo ni lazima kumalizia dawa zote ili kuepuka hali ambayo siyo nzuri ikitokea dawa haijaisha.
5.Kwa hiyo ni vizuri kwa akina mama na walezi wa watoto kubwa makini pindi mnapokuwa hospitalini hakikisha kuwa dawa unazopewa unajua wazi matumizi yake na unaweza kujisimamia mwenyewe na kumpatia mtoto kwa mda mwafaka na akapona kwa hiyo kama hauwezi au haujui matumizi uliza kwa sababu unayo haki ya kupata matibabu kwa wakati na kwa mda wake
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 ai web app π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 kitabu cha Simulizi π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Zijue sababu za kutobeba mimba
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Madhara ya kutoka kwa mimba
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutoka kwa mimba, kwa kawaida tunafahamu kwamba mimba ikitungwa na mwili mzima huwa na wajibu wa kutunza kilichotungwa kwa hiyo ikitokea mimba ikatoka usababisha madhara yafuatayo.
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Mimi nilipima na kipimo mwenyewe nkakuta mistari miwili iliokoza lkn nikifanya tendo nakua naumia sana tatizo ni Nini docta
Je anapatwa maumivu Γ°ΕΈΛΒ makali wakati wa tendo la ndoa ama ukiwa katika hedhi? Soma makala hii hadi mwisho
Soma Zaidi...Madhara ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
Soma Zaidi...mambo HATARI KWA UJAUZITO (MIMBA) mambo yanayopelekea kujauzito kuwa hatarini kutoka
Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.
Soma Zaidi...