Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa.
1.Kwanza kabisa watoto wadogo wanapaswa kuwa karibu sana na walezi wao ili waweze kupata huduma muhimu na za msingi kwa hiyo mtoto akiwa mgonjwa na akaleta hospitalini Mama au mlezi wanapaswa kupewa maelekezo yafuatayo ili kuweza kuwafanya wampatie Mtoto dawa sahihi na kwa wakati wake.
2. Kwanza mama au mlezi wanapaswa kujua dozi na dawa ipi mtoto anapaswa kupewa, na pia wanapaswa kuambiwa wazi sababu ya kupewa dawa hizo, kwa hiyo akina mama wakiwa wanaenda hospitalini ni muhimu kuuliza sababu ya kupewa dawa, mtoto anapaswa kupata dozi ipi na kwa mda gani kwa hiyo ni haki kuuliza na kupewa jibu.
3. Pia Mama anapaswa kuonyeshwa kwa vitendo namna ya kumpatia mtoto dawa na pia ikiwezekana anaweza nkujarubisha akiwa anaangaliwa na kama mtoto hajapewa dawa dozi ya kwanza inaweza kutolewa ili kumfanya Mama aweze kupata uzoefu wakati wa kutoa dawa.
4. Na kama dawa ni zaidi ya moja ni lazima kuziweka alama ili zisije kuchanganywa na pia mama anapaswa kujua kuwa lazima dawa zitolewe kwa mtoto mpaka ziishe hata kama mtoto amepona kwa hiyo ni lazima kumalizia dawa zote ili kuepuka hali ambayo siyo nzuri ikitokea dawa haijaisha.
5.Kwa hiyo ni vizuri kwa akina mama na walezi wa watoto kubwa makini pindi mnapokuwa hospitalini hakikisha kuwa dawa unazopewa unajua wazi matumizi yake na unaweza kujisimamia mwenyewe na kumpatia mtoto kwa mda mwafaka na akapona kwa hiyo kama hauwezi au haujui matumizi uliza kwa sababu unayo haki ya kupata matibabu kwa wakati na kwa mda wake
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Utasa wa Mwanaume hutokana na uzalishaji mdogo wa mbegu za kiume, utendakazi usio wa kawaida wa manii au kuziba kwa manii ambayo huzuia utoaji wa mbegu za kiume. Magonjwa, majeraha, matatizo ya kiafya sugu, u
Soma Zaidi...Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kupasuka kwa mfuko wa uzazi hasa mama anapokalibia kujifungua.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo ni moja katika dalili za ujauzito. Maumivu wanawake wengi hushindwa kujuwa kuwa ni ujauzito ama laa. Na hii ni kwa sababu kwa wanawake wengi maumivu ya tumbo ama changu ni jalivya kawaida kwao.
Soma Zaidi...Kondo la nyuma ni sehemu ya mwili wa mama anapokuwa mjamziti,kondo la nyuma husaidia katika kazi mbalimbali katika ukuaji wa mtoto.
Soma Zaidi...Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...