Mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.

Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto.

Sababu za mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.

1.Kama tulivyotangulia kusema kwamba mishipa ya watoto wadogo uanza kufunguka pale anapofikisaha wiki 2 mpaka miezi 3 ama  lakini kwa watoto wengine mishipa huu ubaki  imefungwa na kusababisha madhara makubwa kwa mtoto katika makuzi yake, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali ambazo ufanya mishipa hiyo kufunga na kusababisha madhara makubwa kwa mtoto kama ifuatavyo.

 

2. Pengine kuna valve ambazo zipo kwenye mwisho wamishipa ya machozi kutofunguka kama inavyotakiwa.

Kwa kawaida kwa mtoto ni lazima valve zote ambazo ziko kwenye macho zinapaswa kufungunguka kwa wakati wake lakini nyingine hubakia zimefungwa hali ambayo Usababisha mishipa ya machozi kwa mtoto kufunga na kusababisha madhara  kwa mtoto na kwa jamii inayotunza mtoto huyu kwa hiyo tatizo liligunduliwa linaweza kutibiwa ambapo upasuaji unaweza kufanyika ili kufungua hizo valve.

 

3. Kuwepo kwa uwazi sehemu ambapo machozi upitia 

Kwa sababu ya kuwepo kwa uwazi kwenye sehemu ya machozi yanapopitia kwa kitaalamu huitwa eylid usababisha mishipa ya machozi kufunga, kwa hiyo ili tatizo la kuwepo kwa uwazi usababishwa na maumbile ya mtoto au kuna Maambukizi ya macho ambayo Usababisha kuwepo kwa uwazi huo.Na pia hili tatizo linaweza kusaidiwa kwa kuwepo kwa upasuaji na kuziba sehemu hiyo.

 

4. Mishipa ya machozi kuwa nyembamba kuzidi kawaida.

Kwa wakati mwingine kuna kipindi mishipa ya machozi inakuwa kweli nyembamba kupita kiasi hali ambayo Usababisha kufunga kwa mishipa ya machozi kwa watoto, kwa hiyo basi ni vizuri kabisa kumpeleka mtoto hospitalini ili kuweza kuona tatizo mliko wapi na kuweza kulifanyia kazi kwa hiyo mishipa nya machozi kwa kawaida inapaswa iwe mipango.

 

5.Kuwepo kwa Maambukizi kwenye macho.

Kwa wakati mwingine maambukizi ndicho chanzo kikuu cha kuwepo kwa Ugonjwa huu, kwa sababu kama kuna Maambukizi ni vizuri kuyatibu ili kuweza kuruhusu mishipa ya machozi iweze kufunguka na mtoto aweze kuwa kama watoto wengine.

 

6. Kuuumia kwenye eneo la mishipa ya machozi na  mifupa ya pua kuziba.

Kwa wakati mwingine mtoto anaweza kuumia kutokana na vitu mbalimbali kwenye eneo la mishipa ya machozi na kusababisha kufunga kwa mishipa ya machozi na kwa wakati mwingine kama kunakuwepo na kuziba kwenye mishipa ya pua pia usababisha kuziba kwa mishipa ya machozi.

 

Dalili za mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.

Pengine tunaweza kujiuliza juwa ni Dalili zipi zinazoonyesha kubwa kuna tatizo kwenye mishipa ya machozi kwa sababu tatizo lenyewe liko ndani na hatuwezi kuliona kwa nje, kwa hiyo Dalili ni kama ifuatavyo.

 

1. Macho kuwa na maji maji.

Kwa kawaida kama mishipa ya machozi imefungwa kitu cha kwanza utaona macho ya mtoto yanatoa maji mara kwa mara na pia mtoto anakaa bila raha kwa wakati mwingine macho yanakuwa yanawasha na mtoto anajikuna kwa hiyo hali hii umfanya mtoto kujihisi vibaya hata kama anacheza na wengine na kwa wakati mwingine wanakuwa wanamnyanyapa kwa sababu ya kutokwa na majimaji machoni.

 

2. Na pia macho ya mtoto mda wote yanakuwa yanatoka na Matongo tongo.

Kwa kawaida uchafu kwenye macho unakuwa hauna sehemu ya kuchujiwa kwa hiyo Matongo tongo utoka machoni, na kwa wakati mwingine ni kwa sababu ya kuwepo na Maambukizi kwenye jicho ndio yanasababisha hali ya kuwepo kwa Matongo , kwa hiyo mtoto anakosa raha na kujitenga na wengine kwa sababu ya tatizo la kuwepo kwa Matongo tongo kwenye macho

 

3. Uchafu mwingi kutoka machoni na pengine unakuwa na harufu mbaya.

Kwa wakati mwingine kunakuwepo na uchafu mwingi kwenye macho ambapo mtoto ukaa anapangusa uchafu kwa kitambaa kama ameshakuwa na uwezo huo kwa wakati mwingine mtoto anakuwa na mafua yanayoambatana na uchafu kutoka kwenye macho.

 

4.Na pia presha ya macho inawezekana kutokea ikiambatana na upofu 

Kama tatizo halijafanyiwa ufumbuzi na kuweza kutibiwa upofu wa macho unaweza kutokea kwa mtoto na kusababisha madhara makubwa zaidi. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kufanya mawasiliano na wataalamu wa afya ili kuweza kupata matibabu kwa mda mwafaka.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2573

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.

Soma Zaidi...
Endapo nina dalili za mimba na nikipima sina mimba, je, tatizo ni nini?

dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.

Soma Zaidi...
Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dr nahis kuchanganyikiwa nimetoka niliingia hedhi tar 18 mwezi wa9 lakini saivi Jana tena nmeingia dr hii imekaaje mimi?

Kamaumeshawahi kujiuliza kuhusu kutokwaba damu tofautivna siku za hedhi, base mwaka hii ni kwaajiki yako.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kushusha homoni za kiume.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?

Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito.

Soma Zaidi...
Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?

Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.

Soma Zaidi...
Dalili Za hatari ambayo zinaweza kusababisha ugumba

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zilijitokeza zinaweza kusababisha ugumba hasa kwa wanawake, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa makini kwa Dalili hizi hasa kwa wadada, kama kuna uwezekano wa matibabu tibu mapema ili kuepuka tatizo la kuwa mgumba.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutoka kwa mimba

Post hii inahusu zaidi madhara ya kutoka kwa mimba, kwa kawaida tunafahamu kwamba mimba ikitungwa na mwili mzima huwa na wajibu wa kutunza kilichotungwa kwa hiyo ikitokea mimba ikatoka usababisha madhara yafuatayo.

Soma Zaidi...