Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto.
Sababu za mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.
1.Kama tulivyotangulia kusema kwamba mishipa ya watoto wadogo uanza kufunguka pale anapofikisaha wiki 2 mpaka miezi 3 ama lakini kwa watoto wengine mishipa huu ubaki imefungwa na kusababisha madhara makubwa kwa mtoto katika makuzi yake, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali ambazo ufanya mishipa hiyo kufunga na kusababisha madhara makubwa kwa mtoto kama ifuatavyo.
2. Pengine kuna valve ambazo zipo kwenye mwisho wamishipa ya machozi kutofunguka kama inavyotakiwa.
Kwa kawaida kwa mtoto ni lazima valve zote ambazo ziko kwenye macho zinapaswa kufungunguka kwa wakati wake lakini nyingine hubakia zimefungwa hali ambayo Usababisha mishipa ya machozi kwa mtoto kufunga na kusababisha madhara kwa mtoto na kwa jamii inayotunza mtoto huyu kwa hiyo tatizo liligunduliwa linaweza kutibiwa ambapo upasuaji unaweza kufanyika ili kufungua hizo valve.
3. Kuwepo kwa uwazi sehemu ambapo machozi upitia
Kwa sababu ya kuwepo kwa uwazi kwenye sehemu ya machozi yanapopitia kwa kitaalamu huitwa eylid usababisha mishipa ya machozi kufunga, kwa hiyo ili tatizo la kuwepo kwa uwazi usababishwa na maumbile ya mtoto au kuna Maambukizi ya macho ambayo Usababisha kuwepo kwa uwazi huo.Na pia hili tatizo linaweza kusaidiwa kwa kuwepo kwa upasuaji na kuziba sehemu hiyo.
4. Mishipa ya machozi kuwa nyembamba kuzidi kawaida.
Kwa wakati mwingine kuna kipindi mishipa ya machozi inakuwa kweli nyembamba kupita kiasi hali ambayo Usababisha kufunga kwa mishipa ya machozi kwa watoto, kwa hiyo basi ni vizuri kabisa kumpeleka mtoto hospitalini ili kuweza kuona tatizo mliko wapi na kuweza kulifanyia kazi kwa hiyo mishipa nya machozi kwa kawaida inapaswa iwe mipango.
5.Kuwepo kwa Maambukizi kwenye macho.
Kwa wakati mwingine maambukizi ndicho chanzo kikuu cha kuwepo kwa Ugonjwa huu, kwa sababu kama kuna Maambukizi ni vizuri kuyatibu ili kuweza kuruhusu mishipa ya machozi iweze kufunguka na mtoto aweze kuwa kama watoto wengine.
6. Kuuumia kwenye eneo la mishipa ya machozi na mifupa ya pua kuziba.
Kwa wakati mwingine mtoto anaweza kuumia kutokana na vitu mbalimbali kwenye eneo la mishipa ya machozi na kusababisha kufunga kwa mishipa ya machozi na kwa wakati mwingine kama kunakuwepo na kuziba kwenye mishipa ya pua pia usababisha kuziba kwa mishipa ya machozi.
Dalili za mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.
Pengine tunaweza kujiuliza juwa ni Dalili zipi zinazoonyesha kubwa kuna tatizo kwenye mishipa ya machozi kwa sababu tatizo lenyewe liko ndani na hatuwezi kuliona kwa nje, kwa hiyo Dalili ni kama ifuatavyo.
1. Macho kuwa na maji maji.
Kwa kawaida kama mishipa ya machozi imefungwa kitu cha kwanza utaona macho ya mtoto yanatoa maji mara kwa mara na pia mtoto anakaa bila raha kwa wakati mwingine macho yanakuwa yanawasha na mtoto anajikuna kwa hiyo hali hii umfanya mtoto kujihisi vibaya hata kama anacheza na wengine na kwa wakati mwingine wanakuwa wanamnyanyapa kwa sababu ya kutokwa na majimaji machoni.
2. Na pia macho ya mtoto mda wote yanakuwa yanatoka na Matongo tongo.
Kwa kawaida uchafu kwenye macho unakuwa hauna sehemu ya kuchujiwa kwa hiyo Matongo tongo utoka machoni, na kwa wakati mwingine ni kwa sababu ya kuwepo na Maambukizi kwenye jicho ndio yanasababisha hali ya kuwepo kwa Matongo , kwa hiyo mtoto anakosa raha na kujitenga na wengine kwa sababu ya tatizo la kuwepo kwa Matongo tongo kwenye macho
3. Uchafu mwingi kutoka machoni na pengine unakuwa na harufu mbaya.
Kwa wakati mwingine kunakuwepo na uchafu mwingi kwenye macho ambapo mtoto ukaa anapangusa uchafu kwa kitambaa kama ameshakuwa na uwezo huo kwa wakati mwingine mtoto anakuwa na mafua yanayoambatana na uchafu kutoka kwenye macho.
4.Na pia presha ya macho inawezekana kutokea ikiambatana na upofu
Kama tatizo halijafanyiwa ufumbuzi na kuweza kutibiwa upofu wa macho unaweza kutokea kwa mtoto na kusababisha madhara makubwa zaidi. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kufanya mawasiliano na wataalamu wa afya ili kuweza kupata matibabu kwa mda mwafaka.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii utakwenda kutoa sababu kuu za kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi. Kama na wewe numiongini mwaka endelea kusoma
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Ujauzito unaweza kutoka kwa sababu nyingi kama maradhi, madawa, vyakula na ajali. Unawezakutoa mimba bila kujuwa amakwakujuwa. Damu kutoka ni moja ya dalili za kutoka kwa mimba hata hivyo maumivu ya tumbo huweza kuandamana na damu hii.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba.
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kuangalia madhara ya tumbaku na sigara anayoweza kuyapata mvutaji
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.
Soma Zaidi...Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kuhusu njia za uzazi wa mpango, uzazi wa mpango ni njia za kupanga uzazi Ili kupata idadi ya watoto unaohitaji
Soma Zaidi...