Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.
Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano.
1.lengo la kwanza ni kuzuia vifo kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano.
Hili ni mojawapo ya lengo ambalo limeweza kuwepo kwa sababu hapo mwanzoni palikuwepo na vifo vingi vya watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa sababu ya kutokuwepo kwa chanjo na baada ya kuwepo kwa chuo Magonjwa mengi yamepungua kama vile kifua kikuu, kifadulo, Surua na magonjwa mengine mengi.
2.Lengo la pili ni kupunguza magonjwa.
Kuanzia malengo yalipoanza na mpaka sasa hivi magonjwa mengi yamepungua ambapo watoto Upata chanjo mapema na pia akina mama uweza kupata chanjo na dawa ili kuwakinga watoto wadogo na pia mahudhurio ya kliniki kila mwezi ambayo uangalia maendeleo ya mtoto.
3. Kuondoa aina yoyote ya ulemavu kwa watoto.
Hapo mwanzoni palikuwepo na ulemavu mbalimbali kwa watoto na sasa hivi ulemavu huo umetoweka kwa sababu ya kuwepo kwa dawa na maelekezo mbalimbali ya wataalamu wa afya kwa kufanya hivyo ulemavu kwa watoto wadogo umepungua kwa kiasi kikubwa.
4. Lengo lingine ni kuona maendeleo mazuri na ukuaji wa watoto kwa wakati, kufuatana na lengo hili watoto wengi wameweza kuangaliwa kuanzia miaka sifuri mpaka miaka mitano na pia mahudhurio ya kliniki yanafanyika ili kuweza kuangalia maendeleo ya mtoto kwa kutumia vigezo mbalimbali ambavyo ni uzito na kuangalia maendeleo ya kwa ujumla.
5. Kwa hiyo tunaona malengo haya ni mazuri na yameleta faida kubwa kwa watoto kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto kupata chanjo na mahudhurio ya kliniki ili kuweza kutokomeza maradhi yanayowapata watoto na kuzuia vifo kwa watoto wadogo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Maumivu ya tumbo kabla ya kupata hedhi
Je unasumbuliwa na maumivu ya tumbo. Unadhani ni dalili za mimba na ukapima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba,ni vipimo vya moja kwa moja kutoka maabara na vingine sio vya maabara.
Soma Zaidi...Madhara ya tumbaku na sigara
Post hii itakwenda kuangalia madhara ya tumbaku na sigara anayoweza kuyapata mvutaji
Soma Zaidi...Sifa za siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba
Soma Zaidi...Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...