Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.
Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano.
1.lengo la kwanza ni kuzuia vifo kwa watoto wadogo chini ya miaka mitano.
Hili ni mojawapo ya lengo ambalo limeweza kuwepo kwa sababu hapo mwanzoni palikuwepo na vifo vingi vya watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa sababu ya kutokuwepo kwa chanjo na baada ya kuwepo kwa chuo Magonjwa mengi yamepungua kama vile kifua kikuu, kifadulo, Surua na magonjwa mengine mengi.
2.Lengo la pili ni kupunguza magonjwa.
Kuanzia malengo yalipoanza na mpaka sasa hivi magonjwa mengi yamepungua ambapo watoto Upata chanjo mapema na pia akina mama uweza kupata chanjo na dawa ili kuwakinga watoto wadogo na pia mahudhurio ya kliniki kila mwezi ambayo uangalia maendeleo ya mtoto.
3. Kuondoa aina yoyote ya ulemavu kwa watoto.
Hapo mwanzoni palikuwepo na ulemavu mbalimbali kwa watoto na sasa hivi ulemavu huo umetoweka kwa sababu ya kuwepo kwa dawa na maelekezo mbalimbali ya wataalamu wa afya kwa kufanya hivyo ulemavu kwa watoto wadogo umepungua kwa kiasi kikubwa.
4. Lengo lingine ni kuona maendeleo mazuri na ukuaji wa watoto kwa wakati, kufuatana na lengo hili watoto wengi wameweza kuangaliwa kuanzia miaka sifuri mpaka miaka mitano na pia mahudhurio ya kliniki yanafanyika ili kuweza kuangalia maendeleo ya mtoto kwa kutumia vigezo mbalimbali ambavyo ni uzito na kuangalia maendeleo ya kwa ujumla.
5. Kwa hiyo tunaona malengo haya ni mazuri na yameleta faida kubwa kwa watoto kwa hiyo tunapaswa kuwapeleka watoto kupata chanjo na mahudhurio ya kliniki ili kuweza kutokomeza maradhi yanayowapata watoto na kuzuia vifo kwa watoto wadogo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo
Soma Zaidi...Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.
Soma Zaidi...Miongoni mwa dalili zamwanzo za ujauzito ni maumivu ya tumbo ama kupatwa na damu kidogo. Mabadiliko ya ute ute sehemu za siri ni katika baadhi ya dalili. Endelea na makala hii utajifunza zaidi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutanuka kwa tezi dume, ni tatizo ambalo linawakumba wanaume wengi kwa wakati huu kwa sababu ya kuwepo kwa maaambukizi kwenye tezi ambayo Usababishwa na vitu mbalimbali kama tulivyoona.
Soma Zaidi...