Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake
1. Kwanza kabisa mama anatokwa na damu nyingi kwa ghafla inawezekana zikawa ni tofauti na damu za siku damu hizo zinaweza kuwepo kwa sababu ya kupasuka kwa uvimbe.
2. Kutokwa na damu nyingi wakati wa siku za mwezi na damu hizo kwa mara nyingi huwa ni za mda mrefu na uchukua mda kuweza kuisha zinaweza kufika hata siku saba.
3. Maumivu ya nyonga.
Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwa hiyo ukandamiza viungo vya nyonga na kusababisha nyonga kuuma
4. Kuwepo kwa haja ndogo ya mara kwa mara.
Kwa kawaida mkojo utoka kama mtu amekunywa chochote ila kama kuna uvimbe mkojo utoka mwingi na wa mara kwa mara.
5. Kuwepo kwa maumivu ya mgongo.
Kwa kawaida mgongo uuma sana na kusababishwa kwa mgandamizo wa uvimbe kwa sababu uvimbe uweza kugandamiza nevu za kwenda kwenye mgongo.
6. Maumivu wakati wa kujamiiana.
Kwa kawaida watu wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na maumivu wakati wa kujamiiana.
7. Kuwepo kwa upungufu wa damu.
Kwa kawaida dalili kubwa ya mtu mwenye uvimbe ni kutokwa kwa damu na damu ikitoka uwepo wa kupungukiwa kwa kiwango cha damu ni kawaida.
8. Maumivu ya kichwa uwapata wenye tatizo la uvimbe, kwa sababu ya kupungua kwa damu na pia maumivu ya kichwa uongezeka.
9. Maumivu kwenye miguu.
Hali hiyo utokea kwa sababu ya mgandamizo wa nevu zinazoenda miguuni pia na kuwepo kwa upungufu wa damu kwa hiyo Usababisha maumivu kwenye miguu.
10. Kuvimba kwenye sehemu za chini ya tumbo hili ni kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi.
11. Kupata uzazi wa shida.
Kwa kawaida wenye uvimbe kwenye via vya uzazi wanaweza kuwa wagumba kama tatizo halijagunduliwa mapema pamoja na kupata uzazi wa shida.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Nimesoma makala yenu, sasa nina swaliJe kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
Soma Zaidi...Tunaposema uzazi wa mpango, tunamaanisha ile hali ya kuachanisha muda kutoka mtoto hadi mwingine. Inatakiwa angalau mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Uzazi wa mpango ni maamuzi kati ya mama na baba.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi Ugonjwa wa kifafa cha mimba ambapo kwa kitaalamu huitwa eclampsia, utokea pale ambapo Mama anapokuwa na degedege wakati wa mimba na baada ya kujiunga.
Soma Zaidi...Download Kitabu cha elimu ya Ujauzito na malezi ya mimba.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kwa mjamzito huweza kuanaa kuonekana mwanzoni kabisa mwaujauzito, ndani ya mwezi mmoja. Ikabidi si dalili pekee ya kuwa ni mjamzito.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...