Zifahamu fibroids (uvimbe kwenye via vya uzazi)
Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake
Dalili za fibroids.
1. Kwanza kabisa mama anatokwa na damu nyingi kwa ghafla inawezekana zikawa ni tofauti na damu za siku damu hizo zinaweza kuwepo kwa sababu ya kupasuka kwa uvimbe.
2. Kutokwa na damu nyingi wakati wa siku za mwezi na damu hizo kwa mara nyingi huwa ni za mda mrefu na uchukua mda kuweza kuisha zinaweza kufika hata siku saba.
3. Maumivu ya nyonga.
Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwa hiyo ukandamiza viungo vya nyonga na kusababisha nyonga kuuma
4. Kuwepo kwa haja ndogo ya mara kwa mara.
Kwa kawaida mkojo utoka kama mtu amekunywa chochote ila kama kuna uvimbe mkojo utoka mwingi na wa mara kwa mara.
5. Kuwepo kwa maumivu ya mgongo.
Kwa kawaida mgongo uuma sana na kusababishwa kwa mgandamizo wa uvimbe kwa sababu uvimbe uweza kugandamiza nevu za kwenda kwenye mgongo.
6. Maumivu wakati wa kujamiiana.
Kwa kawaida watu wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na maumivu wakati wa kujamiiana.
7. Kuwepo kwa upungufu wa damu.
Kwa kawaida dalili kubwa ya mtu mwenye uvimbe ni kutokwa kwa damu na damu ikitoka uwepo wa kupungukiwa kwa kiwango cha damu ni kawaida.
8. Maumivu ya kichwa uwapata wenye tatizo la uvimbe, kwa sababu ya kupungua kwa damu na pia maumivu ya kichwa uongezeka.
9. Maumivu kwenye miguu.
Hali hiyo utokea kwa sababu ya mgandamizo wa nevu zinazoenda miguuni pia na kuwepo kwa upungufu wa damu kwa hiyo Usababisha maumivu kwenye miguu.
10. Kuvimba kwenye sehemu za chini ya tumbo hili ni kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi.
11. Kupata uzazi wa shida.
Kwa kawaida wenye uvimbe kwenye via vya uzazi wanaweza kuwa wagumba kama tatizo halijagunduliwa mapema pamoja na kupata uzazi wa shida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Njia huanza kufunguka mda gani kabla ya kujifungua
Mtoto huweza kuzaliwa ndani ya miezi 6 na unaweza kupona. Na huyu mdoe mtoto njiti. Na anaweza kuzliwa kwa njia ya kawaida. Hakuna ushahidi unaiinyesha kuwa njiti hukabiliwanamatatizo ya kitalima kwenye ukubwa wako.
Soma Zaidi...Siku za kupata mimba
Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta
Soma Zaidi...Mimi imepita miezi mitatu sioni hedhi na wala sioni dalili ya kuwa na mimba unaweza ukaniambia tatizo la kuwa na hali hii
Kama na wewe una tatizo la kupitiliza siku zako za hedhi hli ya kuwa huna ujauzito, soma post hii ina majibu yako.
Soma Zaidi...Dalili za tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Endapo nina dalili za mimba na nikipima sina mimba, je, tatizo ni nini?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...