Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake
1. Kwanza kabisa mama anatokwa na damu nyingi kwa ghafla inawezekana zikawa ni tofauti na damu za siku damu hizo zinaweza kuwepo kwa sababu ya kupasuka kwa uvimbe.
2. Kutokwa na damu nyingi wakati wa siku za mwezi na damu hizo kwa mara nyingi huwa ni za mda mrefu na uchukua mda kuweza kuisha zinaweza kufika hata siku saba.
3. Maumivu ya nyonga.
Kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwa hiyo ukandamiza viungo vya nyonga na kusababisha nyonga kuuma
4. Kuwepo kwa haja ndogo ya mara kwa mara.
Kwa kawaida mkojo utoka kama mtu amekunywa chochote ila kama kuna uvimbe mkojo utoka mwingi na wa mara kwa mara.
5. Kuwepo kwa maumivu ya mgongo.
Kwa kawaida mgongo uuma sana na kusababishwa kwa mgandamizo wa uvimbe kwa sababu uvimbe uweza kugandamiza nevu za kwenda kwenye mgongo.
6. Maumivu wakati wa kujamiiana.
Kwa kawaida watu wenye matatizo ya kuwepo kwa uvimbe huwa na maumivu wakati wa kujamiiana.
7. Kuwepo kwa upungufu wa damu.
Kwa kawaida dalili kubwa ya mtu mwenye uvimbe ni kutokwa kwa damu na damu ikitoka uwepo wa kupungukiwa kwa kiwango cha damu ni kawaida.
8. Maumivu ya kichwa uwapata wenye tatizo la uvimbe, kwa sababu ya kupungua kwa damu na pia maumivu ya kichwa uongezeka.
9. Maumivu kwenye miguu.
Hali hiyo utokea kwa sababu ya mgandamizo wa nevu zinazoenda miguuni pia na kuwepo kwa upungufu wa damu kwa hiyo Usababisha maumivu kwenye miguu.
10. Kuvimba kwenye sehemu za chini ya tumbo hili ni kwa sababu ya kuwepo kwa uvimbe kwenye via vya uzazi.
11. Kupata uzazi wa shida.
Kwa kawaida wenye uvimbe kwenye via vya uzazi wanaweza kuwa wagumba kama tatizo halijagunduliwa mapema pamoja na kupata uzazi wa shida.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba katika mwezi was kwanza
Soma Zaidi...Download Kitabu cha elimu ya Ujauzito na malezi ya mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...Kama uume wako unauma ama unahisi kuwa unaunguza ama kuchoma choma, post hii imekuandalia somo hili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wanaoingia kwenye siku zao zaidi ya mara moja kwa mwezi.
Soma Zaidi...Je umeshawahi kujiukiza kuwa, dawa ya P2 ni kweli inaweza kuzuia mimba, ukifanya mapenzi siku hatari?
Soma Zaidi...