NINI MAANA YA MINYOO: vimelea wa minyoo (parasites)
MINYOO NI NINI?
NINI MAANA YA MINYOO?
MINYOO NI NINI?
Minyoo ni katika vimelea ama wadudu wanaoishi ndani ya kiumbe aliye hai. Wanaweza kuishi kwenye wanyama kama ngoβombe, ngurue na mbuzi, pia wanaweza kuishi ndani ya binadamu. Wanajipatia mahitaji humo kama chakula, hewa na kila wanachohitaji. Wakiwa wanaishi ndani ya mwili wa kiumbe hai wanaweza kusababisha madhara makubwa sana katika afya ya mtu. Wadudu hawa kitaalamu wanatambulika kama parasitic worm.
Katika makala hii tutakwenda kujifunza, dalili, sababu, matibabu na njia za kupambana na minyoo katika mazingira yetu. Pia tutaona madhara ya kiafya yanayoletwa na kuishi na minyoo mwilini. Endelea kuwa nasi upate faida hii
Hatari ya kupata minyoo ni kubwa sana maeneo ya vijijini ama katika maeneo ambayo hali ya usafi sionzuri. Nchi zinazoendelea kama nchi za afrika ni katika maeneo ambayo yanakabil;iwa sana na minyoo kuliko nchi zilizo endelea.
Wataalamu wanatueleza kuwa kuna aina zaidi ya 300,000 (laki tatu) za minyoo. Na katika aina hizi kuna aina 300 (mia tatu) za minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu na kumuathiri kwa namna moja ama nyingine.
Minyoo wanazaliana kwa kutaga mayai, na mayai yao yanatofautiana ukubwa, kuna ambayo yanaonekana kwa macho na mengine ni madogo zaidi kwa kuonekana kwa macho. Kuna aina za minyoo hutaga mayai bila ya kuhitaji kuwepo kwa dume, kwani kuna minyoo ambayo ina jinsia zote kwa pamoja (hermaphroditc).
Minyoo huweza kutaga mayai zaidi ya mara sita kwa siku. Na idadi ya mayai yao ni kati ya mayai 3000, mpaka 700000. na mayai yao yanaweza kudumu kwa miezi mingi biala ya kufa, na yanaweza kuvumialia hali mbalimbali za joto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Bongolite - Game zone - Play free game π4 Kitabu cha Afya π5 web hosting π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)
Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.
Soma Zaidi...Dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa
Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa, ni dalili ambazo ujitokeza tu mtoto anapozaliwa kwa hiyo dalili hizi zinapaswa kuzuiwa ili zisilete madhara makubwa.
Soma Zaidi...Jipu: Chanzo chake na njia salama ya kulitibu.
βJipu (abscess) ni mkusanyiko wa usaha unaotokea chini ya ngozi au ndani ya tishu za mwili kutokana na maambukizi ya bakteria. Mwili hujaribu kujilinda dhidi ya vimelea hivyo kwa kutuma seli nyeupe za damu kwenye eneo husika, na matokeo yake ni kutengeneza mfuko wa usaha unaosababisha maumivu, uvimbe, na joto. Makala haya yanafafanua chanzo cha majipu na mbinu salama za kuyatibu bila kusababisha maambukizi zaidi.
Soma Zaidi...Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili na sababu za mawe kwenye in yaani liver stone au intrahepatic stones
Katika post hii utakwend akujifunza kuhusu tatizo la kuwa na vijiwe kwenye ini vijiwe hivi hufahamika kama intrahepatic stones.
Soma Zaidi...Tofauti kati ya homa ya mapafu (Nimonia) na mafua makali.
βMara nyingi watu huchanganya Nimonia (Pneumonia) na mafua makali kwa sababu yote huathiri mfumo wa upumuaji. Hata hivyo, haya ni magonjwa tofauti kimsingi: mafua husababishwa na virusi na huathiri njia ya juu ya hewa (pua, koo), wakati Nimonia ni maambukizi ya viini (bakteria, virusi, au fangasi) yanayoshambulia mifuko ya hewa ndani ya mapafu (alveoli). Makala hii inaelezea tofauti za kifizikia na umuhimu wa kupata matibabu sahihi.
Soma Zaidi...