Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.
Madhara yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa tatizo la kushindwa kupitisha mkojo.
1.Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo.
Tukumbuke kuwa mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo mara nyingi mkojo huwa na wadudu na wadudu hao inabidi watolewe nje na wakibaki ndani wanaanza kushambulia sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi, kwa hiyo hali hii ya kushindwa kupitisha mkojo inabidi ishughulikiwe mara Moja kwa sababu inaweza kuleta maambukizi makubwa kwenye kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi ambayo ni makubwa zaidi na hayakutarajiwa.
2. Kuharibika kwa figo.
Tunajua kazi za figo kwenye mwili wa binadamu ni kubwa mno kwa hiyo figo likiharibika matatizo mengi utokea kwenye sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu, kwa hiyo figo likiharibika mkojo utashindwa kutengenezwa na damu utashindwa kuchuja na mwisho wake mtu asipotibiwa haraka anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili mapema iwezekanavyo Ili kuweza kuepuka madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kujitokeza na tukashindwa kuyatibu kwa hiyo tutibu tatizo dogo Ili tuepuke kuwepo kwa tatizo kubwa baadae.
3. Kupungua kwa nguvu ya misuli ya kwenye kibofu Cha mkojo.
Hali hii utokea pale ambapo kibofu Cha mkojo kikijaa kinatuna na kusababisha madhara makubwa kwenye misuli ambayo nayo ulegea iwapo tatizo hili kama halijatibiwa mapema linawza kufanya kibofu Cha mkojo kulegea na hatimaye kufanya mkojo ukawa unapita bila taarifa kwa hiyo Tunapaswa kuwa makini katika kutibu ugonjwa huu maana usipotibiwa unaweza kuleta kitu kingine tofauti.
4. Kuwepo kwa UTI.
Ugonjwa wa kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu unaweza kusababisha UTI kwa mgonjwa hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na wadudu ambao wapo ndani ya mkojo kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili iwezekanavyo Ili tuweze kuepuka na janga hili la Ugonjwa wa UTI ambao ni hatari katika maisha ya watu walio wengi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .piaย tutangaliaย njia za kujikinga naย ugonjwa wa UKIMWI
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m
Soma Zaidi...