picha

Madhara ya kushindwa kupitisha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.

Madhara yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa tatizo la kushindwa kupitisha mkojo.

1.Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo.

Tukumbuke kuwa mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo mara nyingi mkojo huwa na wadudu na wadudu hao inabidi watolewe nje na wakibaki ndani wanaanza kushambulia sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi, kwa hiyo hali hii ya kushindwa kupitisha mkojo inabidi ishughulikiwe mara Moja kwa sababu inaweza kuleta maambukizi makubwa kwenye kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi ambayo ni makubwa zaidi na hayakutarajiwa.

 

2. Kuharibika kwa figo.

Tunajua kazi za figo kwenye mwili wa binadamu ni kubwa mno kwa hiyo figo likiharibika matatizo mengi utokea kwenye sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu, kwa hiyo figo likiharibika mkojo utashindwa kutengenezwa na damu utashindwa kuchuja na mwisho wake mtu asipotibiwa haraka anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili mapema iwezekanavyo Ili kuweza kuepuka madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kujitokeza na tukashindwa kuyatibu kwa hiyo tutibu tatizo dogo Ili tuepuke kuwepo kwa tatizo kubwa baadae.

 

3. Kupungua kwa nguvu ya misuli ya kwenye kibofu Cha mkojo.

Hali hii utokea pale ambapo kibofu Cha mkojo kikijaa kinatuna na kusababisha madhara makubwa kwenye misuli ambayo nayo ulegea iwapo tatizo hili kama halijatibiwa mapema linawza kufanya kibofu Cha mkojo kulegea na hatimaye  kufanya mkojo ukawa unapita bila taarifa kwa hiyo Tunapaswa kuwa makini katika kutibu ugonjwa huu  maana usipotibiwa unaweza kuleta kitu kingine tofauti.

 

4. Kuwepo kwa UTI.

Ugonjwa wa kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu unaweza kusababisha UTI kwa mgonjwa hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na wadudu ambao wapo ndani ya mkojo kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili iwezekanavyo Ili tuweze kuepuka na janga hili la Ugonjwa wa UTI ambao ni hatari katika maisha ya watu walio wengi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1251

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 web hosting     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Kwa nini kung’atwa na mbu hakuambukizi UKIMWI?

Ingawa mbu hunyonya damu kwa binadamu, hawana uwezo wa kueneza virusi vya UKIMWI (VVU). Sababu ni kwamba virusi vya VVU haviwezi kuishi wala kuzaliana ndani ya mwili wa mbu, na pia mbu hawaingizi damu ya mtu mmoja kwa mwingine wanapong’ata.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya magonjwa ya ngono

Posti hii inahusu athari za maambukizi ya magonjwa ya ngono  ambapo magonjwa ya ngono isipokuwa UKIMWI  yanatibika .mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitali au kituo chochote cha afya kupata matibabu mara anapoona dalili za magonjwa haya.

Soma Zaidi...
Nini sababu ya kuchubuka midomo na kuwa myeupe

Kama una tatizo la midomo kuchubuka na kuwa myeupe ama kuwa na vidonda. Post hii inakwenda kuangalia swala hili.

Soma Zaidi...
MTAMBUE MDUDU MBU ILI UWEZE KUJIKINGA NA UGONJWA WA MALARIA (yajuwe maajabu makubwa ya mdudu mbu)

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik.

Soma Zaidi...
Tatizo la mapafu kuwa na usaha.

Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha .

Soma Zaidi...
Namna madonda koo yanavyotokea

Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.

Soma Zaidi...