Madhara ya kushindwa kupitisha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kushindwa kupitisha mkojo, ni madhara makubwa yanayotokea kwa mtu iwapo akishindwa kupitisha mkojo.

Madhara yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa tatizo la kushindwa kupitisha mkojo.

1.Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo.

Tukumbuke kuwa mkojo unachujwa kutoka sehemu mbalimbali za mwili kwa hiyo mara nyingi mkojo huwa na wadudu na wadudu hao inabidi watolewe nje na wakibaki ndani wanaanza kushambulia sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi, kwa hiyo hali hii ya kushindwa kupitisha mkojo inabidi ishughulikiwe mara Moja kwa sababu inaweza kuleta maambukizi makubwa kwenye kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi ambayo ni makubwa zaidi na hayakutarajiwa.

 

2. Kuharibika kwa figo.

Tunajua kazi za figo kwenye mwili wa binadamu ni kubwa mno kwa hiyo figo likiharibika matatizo mengi utokea kwenye sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu, kwa hiyo figo likiharibika mkojo utashindwa kutengenezwa na damu utashindwa kuchuja na mwisho wake mtu asipotibiwa haraka anaweza kupoteza maisha, kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili mapema iwezekanavyo Ili kuweza kuepuka madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kujitokeza na tukashindwa kuyatibu kwa hiyo tutibu tatizo dogo Ili tuepuke kuwepo kwa tatizo kubwa baadae.

 

3. Kupungua kwa nguvu ya misuli ya kwenye kibofu Cha mkojo.

Hali hii utokea pale ambapo kibofu Cha mkojo kikijaa kinatuna na kusababisha madhara makubwa kwenye misuli ambayo nayo ulegea iwapo tatizo hili kama halijatibiwa mapema linawza kufanya kibofu Cha mkojo kulegea na hatimaye  kufanya mkojo ukawa unapita bila taarifa kwa hiyo Tunapaswa kuwa makini katika kutibu ugonjwa huu  maana usipotibiwa unaweza kuleta kitu kingine tofauti.

 

4. Kuwepo kwa UTI.

Ugonjwa wa kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu unaweza kusababisha UTI kwa mgonjwa hii ni kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na wadudu ambao wapo ndani ya mkojo kwa hiyo tunapaswa kutibu tatizo hili iwezekanavyo Ili tuweze kuepuka na janga hili la Ugonjwa wa UTI ambao ni hatari katika maisha ya watu walio wengi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 978

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za Mgonjwa wa kisukari

Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.

Soma Zaidi...
Ndugu mke Wang viungo vina mlegea miguu inamuaka moto nn tatozo

Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.

Soma Zaidi...
Fangasi aina ya Candida

Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida.

Soma Zaidi...
Dalili zinazoonyesha joto la kupungua mwilini (hypothermia)

joto la mwili wako linapungua, moyo wako, mfumo wa neva na viungo vingine haviwezi kufanya kazi kwa kawaida. Isipopotibiwa, Hypothermia hatimaye inaweza kusababisha moyo wako na mfumo wa upumuaji kushindwa kabisa na hata kifo.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani (cancer)

Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.

Soma Zaidi...
KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI

Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Hatua za kupambana na ugonjwa wa UTI

Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi ukeni

Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri.

Soma Zaidi...
Viungo vinavyoathiriwa na malaria

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya viungo vinavyoathiriwa na ugonjwa wa malaria

Soma Zaidi...