Dalili za Dengue.

Dalili za Dengue.

Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg

Dalili za Ugonjwa wa Dengue.

1 Dalili ya kwanza ni homa ya Dengue 

Hii ni mojawapo ya homa ambayo huwa tofauti kidogo na homa nyingine kwa sababu kunakuwepo na maumivu ya macho, kichwa kinauma kweli kweli, maupele yanaweza kuambatana na hiyo homa,na maumivu ya kwenye fizi za meno ambayo Usababisha na kuvuja damu kwenye fizi, kutapika damu na kwa wakati mwingine damu inaweza kuwa kwenye kinyesi, kutapika,kuishiwa na hamu ya kula, maumivu ya tumbo hayo yote uambatana na homa.

 

2. Dalili ya pili ni pale ambapo homa inaongezeka na kusababisha kila sehemu iliyokuwa inavuja kawaida kwenye homa ya kwanza ya dengua kuongeza na maumivu yanaongezeka na sehemu hii kwa kitaalamu huitwa hemorrhagic fever, homa hii inaweza kwenda kuanzia kwenye siku ya kwanza mpaka saba yaan wiki nzima na kwa upande wa watoto kuongezeka kwa homa usababisha kuwepo kwa degedege hali inayosababisha Ugonjwa huu kuleta shida sana kwa watoto.

 

3. Katika sehemu hii ya pili maumivu ya macho pia uongezeka na kusababisha kuwa mekundu na pia joint kwenye miguuu kuuumia na pia sehemu ile iliyokuwa na upele kidogo kidogo uongezeka na kuwa na mabaka mabaka hali ambayo ufanya Mgonjwa kuweza kuonekana vibaya na pia kiwango cha seli nyeupe za damu kupungua kwa sababu ya kuwepo kwa mashambulizi kati ya seli na Maambukizi kwenye mwili.

 

4. Katika hatua hiii ya mwisho ni pale Mgonjwa anakuwa amezidiwa sana na katika dalili hizi kupona ni bahati kwa sababu Mzunguko wa damu unapungua, upumuaji upungua , na msukumo wa damu nao upungua hali ambayo husababisha presha kuwa chini na pengine Mgonjwa huwa wa baridi na mgonjwa anashindwa kutulia. Kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa mgonjwa akifikia kwenye dalili hizi anaweza kufariki.

 

5.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za Ugonjwa huu na kutoa taarifa kwa wahusika ili kuweza kuokoa maisha ya watu kwa kusaidia kuzuia kuongezeka kwa dalili hali ambayo Usababisha kuwepo kwa vifo.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 2605

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi ya sikio kwa watoto

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za maambukizi ya sikio kwa watoto.

Soma Zaidi...
Magonjwa ya moyo

Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya moyo, kwa kawaida watu wakisikia habari za magonjwa ya moyo huwa hawaelewi yanakuwaje kuwaje, Leo nataka niwafahamishe kuhusu magonjwa ya moyo na sehemu mbalimbali zinazoathirika.

Soma Zaidi...
Matatizo ya tezi ya shingo (Thyroid disorders): Dalili zake.

Tezi ya shingo (Thyroid gland) ni kiungo kidogo chenye umbo la kipepeo kilichopo sehemu ya mbele ya shingo. Ingawa ni ndogo, ina kazi kubwa sana ya kuzalisha homoni zinazodhibiti kila kitu kuanzia kasi ya mapigo ya moyo, joto la mwili, hadi namna tunavyochoma kalori. Matatizo ya tezi hutokea pale tezi hii inapozalisha homoni nyingi sana (Hyperthyroidism) au kidogo sana (Hypothyroidism). Makala haya yanachambua dalili za hali hizi mbili ili kukusaidia kuelewa ishara za mwili wako.

Soma Zaidi...
KAMA UNASUMBULIWA NA FANGASI

Post hii fupi inakwenda kukujuza juu ya tatizo la fangasi na nini ufanye.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kinywa

Post hii inahusu dalili za uvimbe kwenye kinywa ambapo kitaalamu hujulikana Kama oral candidiasis Uvimbe kwenye kinywa husababisha vidonda vyeupe, kwa kawaida kwenye ulimi au mashavu ya ndani. Wakati mwingine uvimbe kwenye kinywa huweza ku

Soma Zaidi...