Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Dalili za Ugonjwa wa Dengue.
1 Dalili ya kwanza ni homa ya Dengue
Hii ni mojawapo ya homa ambayo huwa tofauti kidogo na homa nyingine kwa sababu kunakuwepo na maumivu ya macho, kichwa kinauma kweli kweli, maupele yanaweza kuambatana na hiyo homa,na maumivu ya kwenye fizi za meno ambayo Usababisha na kuvuja damu kwenye fizi, kutapika damu na kwa wakati mwingine damu inaweza kuwa kwenye kinyesi, kutapika,kuishiwa na hamu ya kula, maumivu ya tumbo hayo yote uambatana na homa.
2. Dalili ya pili ni pale ambapo homa inaongezeka na kusababisha kila sehemu iliyokuwa inavuja kawaida kwenye homa ya kwanza ya dengua kuongeza na maumivu yanaongezeka na sehemu hii kwa kitaalamu huitwa hemorrhagic fever, homa hii inaweza kwenda kuanzia kwenye siku ya kwanza mpaka saba yaan wiki nzima na kwa upande wa watoto kuongezeka kwa homa usababisha kuwepo kwa degedege hali inayosababisha Ugonjwa huu kuleta shida sana kwa watoto.
3. Katika sehemu hii ya pili maumivu ya macho pia uongezeka na kusababisha kuwa mekundu na pia joint kwenye miguuu kuuumia na pia sehemu ile iliyokuwa na upele kidogo kidogo uongezeka na kuwa na mabaka mabaka hali ambayo ufanya Mgonjwa kuweza kuonekana vibaya na pia kiwango cha seli nyeupe za damu kupungua kwa sababu ya kuwepo kwa mashambulizi kati ya seli na Maambukizi kwenye mwili.
4. Katika hatua hiii ya mwisho ni pale Mgonjwa anakuwa amezidiwa sana na katika dalili hizi kupona ni bahati kwa sababu Mzunguko wa damu unapungua, upumuaji upungua , na msukumo wa damu nao upungua hali ambayo husababisha presha kuwa chini na pengine Mgonjwa huwa wa baridi na mgonjwa anashindwa kutulia. Kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa mgonjwa akifikia kwenye dalili hizi anaweza kufariki.
5.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za Ugonjwa huu na kutoa taarifa kwa wahusika ili kuweza kuokoa maisha ya watu kwa kusaidia kuzuia kuongezeka kwa dalili hali ambayo Usababisha kuwepo kwa vifo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 ai web app π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Madrasa kiganjani π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Ugonjwa wa kuungua Mdomo (mouth burning syndrome)
Ugonjwa wa mdomo unaounguaΓΒ ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuwaka moto mara kwa mara mdomoni bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea ya mdomo wako wot
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye mfumo wa usagaji chakula unaotokea kwenye utumbo mkubwa (diverticulitis)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mifuko midogo midogo, iliyobubujika ambayo inaweza kuunda kwenye utando wa mfumo wako wa usagaji chakula. Wao hupatikana mara nyingi katika sehemu ya chini ya utumbo mkubwa (koloni). Hali hiyo inajulikana kama Divert
Soma Zaidi...Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV
Soma Zaidi...Habari nasumbuliwa na tumbo upande wakilia adi nikikojoa mkojo wa mwisho uwa wa kahawia tiba take nini?
Maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na mambo mengi ikiwemo typhod, vidonda vya tumbo na shida nyingine kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Watu walio hatarini kupata UTI
Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI
Soma Zaidi...