Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Dalili za Ugonjwa wa Dengue.
1 Dalili ya kwanza ni homa ya Dengue
Hii ni mojawapo ya homa ambayo huwa tofauti kidogo na homa nyingine kwa sababu kunakuwepo na maumivu ya macho, kichwa kinauma kweli kweli, maupele yanaweza kuambatana na hiyo homa,na maumivu ya kwenye fizi za meno ambayo Usababisha na kuvuja damu kwenye fizi, kutapika damu na kwa wakati mwingine damu inaweza kuwa kwenye kinyesi, kutapika,kuishiwa na hamu ya kula, maumivu ya tumbo hayo yote uambatana na homa.
2. Dalili ya pili ni pale ambapo homa inaongezeka na kusababisha kila sehemu iliyokuwa inavuja kawaida kwenye homa ya kwanza ya dengua kuongeza na maumivu yanaongezeka na sehemu hii kwa kitaalamu huitwa hemorrhagic fever, homa hii inaweza kwenda kuanzia kwenye siku ya kwanza mpaka saba yaan wiki nzima na kwa upande wa watoto kuongezeka kwa homa usababisha kuwepo kwa degedege hali inayosababisha Ugonjwa huu kuleta shida sana kwa watoto.
3. Katika sehemu hii ya pili maumivu ya macho pia uongezeka na kusababisha kuwa mekundu na pia joint kwenye miguuu kuuumia na pia sehemu ile iliyokuwa na upele kidogo kidogo uongezeka na kuwa na mabaka mabaka hali ambayo ufanya Mgonjwa kuweza kuonekana vibaya na pia kiwango cha seli nyeupe za damu kupungua kwa sababu ya kuwepo kwa mashambulizi kati ya seli na Maambukizi kwenye mwili.
4. Katika hatua hiii ya mwisho ni pale Mgonjwa anakuwa amezidiwa sana na katika dalili hizi kupona ni bahati kwa sababu Mzunguko wa damu unapungua, upumuaji upungua , na msukumo wa damu nao upungua hali ambayo husababisha presha kuwa chini na pengine Mgonjwa huwa wa baridi na mgonjwa anashindwa kutulia. Kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa mgonjwa akifikia kwenye dalili hizi anaweza kufariki.
5.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za Ugonjwa huu na kutoa taarifa kwa wahusika ili kuweza kuokoa maisha ya watu kwa kusaidia kuzuia kuongezeka kwa dalili hali ambayo Usababisha kuwepo kwa vifo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 ai web app ๐2 Simulizi za Hadithi Audio ๐3 Bongolite - Game zone - Play free game ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 Kitabu cha Afya ๐6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Jinsi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa (STIs).
Magonjwa ya zinaa, yanayojulikana pia kama STIs (Sexually Transmitted Infections), ni miongoni mwa changamoto kubwa za afya ya umma duniani. Kila mwaka, mamilioni ya watu hupata maambukizi mapya ya magonjwa haya, huku wengi wakikosa kutambua kuwa wameambukizwa kutokana na kutokuwa na dalili katika hatua za awali. Habari njema ni kwamba sehemu kubwa ya maambukizi ya magonjwa ya zinaa inaweza kuzuilika kwa kufuata mbinu sahihi za kinga na kufanya maamuzi salama kuhusu afya ya uzazi. Katika makala hii utajifunza maana ya magonjwa ya zinaa, namna yanavyoenea, sababu zinazoongeza hatari ya maambukizi, njia bora za kujikinga, umuhimu wa kupima afya mara kwa mara, pamoja na ukweli muhimu ambao kila mtu anapaswa kuufahamu kuhusu STIs.
Soma Zaidi...UGONJWA WA HOMA YA VIRUSI VYA ZIKA (ZIKV) VINAVYO SABABISHWA NA KUNG'ATWA NA MBU
Mnamo mwaka 2016 World Health Organization (WHO) iliitisha kikao cha dharura mnamo mwezi tarehe 1 mwezi wa pili mpaka tarehe 13 mwezi wa nne.
Soma Zaidi...Dawa za kutibu kiungulia
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dawa za kutibu kiungulia
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi ya via vya uzazi (PID) na tiba yake.
Maambukizi ya viungo vya uzazi, kitaalamu kama Pelvic Inflammatory Disease (PID), ni hali ya kuvimba kwa viungo vya uzazi vya ndani ya mwanamke, ikiwemo mji wa mimba, mirija ya uzazi, na ovari. Makala hii inaelezea dalili za ugonjwa huu, sababu zake, na umuhimu wa kupata tiba sahihi na ya haraka ili kulinda uwezo wako wa kuzaa.
Soma Zaidi...Dalili za UKIMWI kwa Mwanamke Zinazoonekana Mapema
โMuhtasari โMakala haya yanatoa mwongozo wa kielimu kuhusu ishara za awali ambazo mwili wa mwanamke unaweza kuonyesha baada ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI (HIV). Tunasisitiza kuwa dalili hizi si mbadala wa vipimo vya maabara na tunahimiza upimaji wa hiari kwa ajili ya afya bora.
Soma Zaidi...Homa ya matumbo (Typhoid): Jinsi ya kuepuka kurudia kwa ugonjwa.
โHoma ya matumbo (Typhoid fever) ni ugonjwa unaoambukizwa kupitia chakula na maji yaliyochafuka, ukiwa unasababishwa na bakteria aina ya Salmonella Typhi. Licha ya kupata matibabu ya dawa, wagonjwa wengi hukabiliwa na hatari ya ugonjwa huu kujirudia. Makala haya yanatoa mwongozo wa kina kuhusu namna ya kuzuia maambukizi mapya na kuelewa umuhimu wa usafi wa mazingira na chanjo katika kuimarisha afya yako.
Soma Zaidi...