Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Dalili za Ugonjwa wa Dengue.
1 Dalili ya kwanza ni homa ya Dengue
Hii ni mojawapo ya homa ambayo huwa tofauti kidogo na homa nyingine kwa sababu kunakuwepo na maumivu ya macho, kichwa kinauma kweli kweli, maupele yanaweza kuambatana na hiyo homa,na maumivu ya kwenye fizi za meno ambayo Usababisha na kuvuja damu kwenye fizi, kutapika damu na kwa wakati mwingine damu inaweza kuwa kwenye kinyesi, kutapika,kuishiwa na hamu ya kula, maumivu ya tumbo hayo yote uambatana na homa.
2. Dalili ya pili ni pale ambapo homa inaongezeka na kusababisha kila sehemu iliyokuwa inavuja kawaida kwenye homa ya kwanza ya dengua kuongeza na maumivu yanaongezeka na sehemu hii kwa kitaalamu huitwa hemorrhagic fever, homa hii inaweza kwenda kuanzia kwenye siku ya kwanza mpaka saba yaan wiki nzima na kwa upande wa watoto kuongezeka kwa homa usababisha kuwepo kwa degedege hali inayosababisha Ugonjwa huu kuleta shida sana kwa watoto.
3. Katika sehemu hii ya pili maumivu ya macho pia uongezeka na kusababisha kuwa mekundu na pia joint kwenye miguuu kuuumia na pia sehemu ile iliyokuwa na upele kidogo kidogo uongezeka na kuwa na mabaka mabaka hali ambayo ufanya Mgonjwa kuweza kuonekana vibaya na pia kiwango cha seli nyeupe za damu kupungua kwa sababu ya kuwepo kwa mashambulizi kati ya seli na Maambukizi kwenye mwili.
4. Katika hatua hiii ya mwisho ni pale Mgonjwa anakuwa amezidiwa sana na katika dalili hizi kupona ni bahati kwa sababu Mzunguko wa damu unapungua, upumuaji upungua , na msukumo wa damu nao upungua hali ambayo husababisha presha kuwa chini na pengine Mgonjwa huwa wa baridi na mgonjwa anashindwa kutulia. Kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa mgonjwa akifikia kwenye dalili hizi anaweza kufariki.
5.Kwa hiyo jamii inapaswa kujua Dalili za Ugonjwa huu na kutoa taarifa kwa wahusika ili kuweza kuokoa maisha ya watu kwa kusaidia kuzuia kuongezeka kwa dalili hali ambayo Usababisha kuwepo kwa vifo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 ai web app π4 Dua za Mitume na Manabii π5 web hosting π6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Saratani ya Matiti ya wanaume.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ya matiti ya Mwanaume ni Saratani nadra ambayo hutokea katika tishu za matiti za wanaume. Ingawa saratani ya matiti hufikiriwa zaidi kuwa ugonjwa wa wanawake, saratani ya matiti ya mwanaume hutokea. Saratani y
Soma Zaidi...Kulegea kwa mwili na uchovu wa mara kwa mara: Chanzo chake.
Uchovu wa mara kwa mara na hali ya kulegea kwa mwili ni malalamiko ya kawaida yanayoweza kuashiria changamoto za kifizikia, kisaikolojia, au mtindo wa maisha. Makala haya yanachunguza visababishi vya ndani na nje vya hali hii, umuhimu wa utambuzi sahihi, na mikakati ya kitaalamu ya kurejesha nishati na ustawi wa mwili.
Soma Zaidi...YAMINYOO NA ATHARI ZAO KIAF
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Soma Zaidi...Ni zipi dalili za awali za pumu
Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.
Soma Zaidi...Dalili za Minyoo kwa Watoto
βMinyoo ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo linaweza kuathiri ukuaji na afya zao kwa ujumla. Makala haya yataeleza dalili za kawaida za maambukizi ya minyoo, ukweli muhimu kuhusu tiba yake, na umuhimu wa usafi katika kuzuia tatizo hili.
Soma Zaidi...