NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?: maji, vyakula, nyama, udongo, kinyesi, mayai ya minyoo, uchafu wa mwili na mazingira
NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?
NINI WANACHOKULA MINYOO
NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?
Kama tulivyokwisha kuona aina za minyoo, bila shaka umetambua kidogo kuhusu nini wanakifanya wakiwa mwilini. Hivyo basi katika sehemu hii nitakwenda kukueleza chakula cha minyoo ndani ya mwili:-
1.Wanakula chakula tunachokula, katika aina hizi za minyoo wapo minyoo wanaishi kwenye utumbo mdogo. Hii ndiyo sehemu ambayo chakula kinameng’enywa na kuupa mwili nishati na afya yaani kuupatia mwili virutubisho. Lakini minyoo hawa wakati mwingine wanakula chakula alichokula mtu hata kabla ya kumeng’enywa. Hali hii inaweza kusababishia mtu kukosa virutubisho na hatimaye kukonda ama kupoteza usito.
2.Wanakunywa damu, wapo minyoo wengine wanaishi kwenye mfumo wa damu ama ameneo mengine na kuanza kunyonya damu. Minyoo hawa ni hatari sana kwani wanaweza kusababisha ugonjwa wa anaemia. Ugonjwa huu husababishwa na upungufu wa damu.
3.Wanakula viungo vya mwili, katika minyoo hawa kwa mfano liverfluke hawa wanaishi kwenye ini ama maeneo ya nyongo. Minyoo hawa wanakula ini, na kulisababishia vidonda. Pia ini linaweza kuvimba hatimaye kuleta madhara makubwa.
4.Wanakula tishu nyingine, tofauti na hayo tuliyotaja minyoo hawa wanaweza kula tishu nyingine ndani ya mwili. Kama tulivyoona kuna baadhi ya minyoo wanakaa kwenye ngozi, viungio, ini na sehemu nyingine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Dalili za kisukari na njia za kuzuia kisukari
Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisakari, dalili zake,na namna ya kujikinga usipate kisukari au Kama tayari unakisukari ukijikinga madhara yanapungua au kupona kabisa.Kisukari au bolisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwa
Soma Zaidi...Shinikizo la damu (High Blood Pressure): Sababu na vyakula vya kuepuka.
Shinikizo la damu (Hypertension) ni tatizo sugu la kiafya linaloathiri mamilioni ya watu duniani kote. Makala hii inachunguza kwa kina kiini cha shinikizo la damu, sababu zake kuu, na umuhimu wa lishe katika kudhibiti hali hii. Kwa kuelewa vyakula vya kuepuka na mabadiliko ya mtindo wa maisha, unaweza kulinda afya ya moyo wako na kuzuia madhara makubwa kama kiharusi na ugonjwa wa figo.
Soma Zaidi...Dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa
Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mtoto aliyezaliwa, ni dalili ambazo ujitokeza tu mtoto anapozaliwa kwa hiyo dalili hizi zinapaswa kuzuiwa ili zisilete madhara makubwa.
Soma Zaidi...Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa
Soma Zaidi...Kushambuliwa kwa moyo na kupumua
Post hii inahusu zaidi kuhusu kushambuliwa kwa moyo na kupumua, kushambuliwa kwa moyo na kupumua kwa kitaala huitwa (cardiopulmonary Arrest) ni kitendo Cha kusimama ghafla kwa moyo na kupumua.
Soma Zaidi...Nini husababisha ugonjwa wa kifua na maumivu ya kifua?
Posti hii inazungumzia sababu zinazopelekea kuumwa na kifua.
Soma Zaidi...