NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?: maji, vyakula, nyama, udongo, kinyesi, mayai ya minyoo, uchafu wa mwili na mazingira
NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?
NINI WANACHOKULA MINYOO
NI NINI CHAKULA CHA MINYOO?
Kama tulivyokwisha kuona aina za minyoo, bila shaka umetambua kidogo kuhusu nini wanakifanya wakiwa mwilini. Hivyo basi katika sehemu hii nitakwenda kukueleza chakula cha minyoo ndani ya mwili:-
1.Wanakula chakula tunachokula, katika aina hizi za minyoo wapo minyoo wanaishi kwenye utumbo mdogo. Hii ndiyo sehemu ambayo chakula kinameng’enywa na kuupa mwili nishati na afya yaani kuupatia mwili virutubisho. Lakini minyoo hawa wakati mwingine wanakula chakula alichokula mtu hata kabla ya kumeng’enywa. Hali hii inaweza kusababishia mtu kukosa virutubisho na hatimaye kukonda ama kupoteza usito.
2.Wanakunywa damu, wapo minyoo wengine wanaishi kwenye mfumo wa damu ama ameneo mengine na kuanza kunyonya damu. Minyoo hawa ni hatari sana kwani wanaweza kusababisha ugonjwa wa anaemia. Ugonjwa huu husababishwa na upungufu wa damu.
3.Wanakula viungo vya mwili, katika minyoo hawa kwa mfano liverfluke hawa wanaishi kwenye ini ama maeneo ya nyongo. Minyoo hawa wanakula ini, na kulisababishia vidonda. Pia ini linaweza kuvimba hatimaye kuleta madhara makubwa.
4.Wanakula tishu nyingine, tofauti na hayo tuliyotaja minyoo hawa wanaweza kula tishu nyingine ndani ya mwili. Kama tulivyoona kuna baadhi ya minyoo wanakaa kwenye ngozi, viungio, ini na sehemu nyingine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
DALILI ZA HOMA YA BONDE LA UFA (RVFD) NA INAVYOSAMBAZWA.
Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati.
Soma Zaidi...Dalili za maumivu yanayosababishwa na mtiririko mdogo wa Damu.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu yanayosababishwa na mtiririko mdogo wa damu, kwa kawaida wakati wa mazoezi. Wakati mwingine huitwa upenyo wa vipindi, hali hii kwa ujumla huathiri mishipa ya damu kwenye miguu, lakini upenyo unaweza kuathiri mi
Soma Zaidi...Sababu za ugonjwa wa mkojo kuwa na damu
Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu.
Soma Zaidi...dalili za ukimwi kwa mwanaume
Katika post hii utakwenda kujifunza zaidi khusu dalili za ukimwi ama HIV kwa wanaume
Soma Zaidi...Minyoo na athari zao kiafya
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu minyoo na athari zao kiafya
Soma Zaidi...