Athari za ugonjwa wa Dondakoo
Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.
1. Kupumua vibaya kwa mtoto na pengine mtoto anashindwa kumeza au anameza kwa shida.
Ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtoto zinaweza kuwa za kudumu au kwa mda tunajua kuwa ugonjwa huu ushambulia Koo mara nyingine Koo linapata maambukizi makubwa ambayo usababisha mtoto kushindwa kabisa kumeza au wengine wanafaulu kumeza Ila kwa shida kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema na Tiba yenyewe ni kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa kufanya hivyo tutapunguza shida kwenye jamii na watoto tunawaandalia maisha mazuri na yenye natumaini.
2. Kupooza kuanzia kwenye paji la uso mpaka shingoni, kwa sababu ya kuenea kwa bakteria katika sehemu mbalimbali za mfumo wa hewa maambukizi hayo ufanya sehemu hizo kupooza yaani kuanzia kwenye sehemu ya paji la uso mpaka shiy kwa hiyo tunaona hali hii ni ya kuuumiza hasa kwa mtoto na kumsababishis ulemavu wa kudumu kwa sababu zisizi za msingi kama vile Imani potofu juu ya chanjo au kufanya uzembe katika kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa hiyo mtoto anakosa furaha na kupata ulemavu wa kudumu katika maisha yake.
3. Maambukizi yanaenea sana .
Kama ugonjwa huu haujadhibituwa usababisha maambukizi kwa watu wengine na kuleta madhara makubwa ambayo yanawaletea wengine ulemavu wa kudumu ambapo kama na wenyewe hawajatambua dalili mapema wanaweza kuendelea kuishi nao, basi jamii inapaswa kujua wazi dalili za ugonjwa huu wa Donda Koo na kujiadhari mapema kuhusu ugonjwa huu.
4. Kwa Sababu ya kuwepo kwa maumivu makali kwenye shingo, kushindwa kumeza na kupumua kwa mtoto, kuvimba shingo kwa mtoto na kupooza kwa mtoto kifo kinaweza kutokea ikiwa mamb o haya haya kutibiwa mapema, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa Dondakoo ni hatari kwa watoto na kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata chanjo na kama Kuna Imani potofu kuhusu chanjo jamii inabidi kuwa macho Ili kuondoa Imani hizi potofu.
5. Chanjo ambayo utolewa ni mchanganyiko wa chanjo ya kuzuia kifaduro, Pepopunda, Homa ya inni, hima ya uti wa mgongo, kwa Jina Moja huitwa pentavalent. Kwa hiyo mama au walezi wanaweza kuuliza wataalamu wa afya Ili kuhakikisha kama watoto wao wamepata chanjo ya Dondakoo Ili kuepusha madhara mbalimbali katika jamii yetu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Dalili za Mimba Kabla ya Kukosa Hedhi
​Siku za mwanzoni baada ya kutunga mimba, mwili wa mwanamke huanza kuonyesha mabadiliko madogo ya homoni. Post hii inaangazia ishara za awali ambazo zinaweza kujitokeza hata kabla ya siku ya hedhi inayotarajiwa, ikielezea sababu zake na jinsi ya kuzitofautisha na dalili za kawaida za kabla ya hedhi (PMS).
Soma Zaidi...Maumivu wakati wa hedhi
​Maumivu wakati wa hedhi, kitaalamu yakijulikana kama Dysmenorrhea, ni changamoto inayowaathiri mamilioni ya wanawake duniani kote. Wakati maumivu mepesi yakichukuliwa kama hali ya kawaida ya mabadiliko ya mwili, maumivu makali yanayomzuia mwanamke kufanya shughuli zake za kila siku yanaweza kuwa ishara ya matatizo makubwa ya kiafya. Makala haya yanajadili aina za maumivu haya, vyanzo vyake vikuu, njia za nyumbani na za kitabibu za kupata suluhisho, pamoja na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu.
Soma Zaidi...Njia za kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine
Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Soma Zaidi...Ukiwa na aleji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?
Swali langu: Ukiwa na areji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?
Soma Zaidi...Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV
Soma Zaidi...