Athari za ugonjwa wa Dondakoo
Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.
1. Kupumua vibaya kwa mtoto na pengine mtoto anashindwa kumeza au anameza kwa shida.
Ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtoto zinaweza kuwa za kudumu au kwa mda tunajua kuwa ugonjwa huu ushambulia Koo mara nyingine Koo linapata maambukizi makubwa ambayo usababisha mtoto kushindwa kabisa kumeza au wengine wanafaulu kumeza Ila kwa shida kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema na Tiba yenyewe ni kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa kufanya hivyo tutapunguza shida kwenye jamii na watoto tunawaandalia maisha mazuri na yenye natumaini.
2. Kupooza kuanzia kwenye paji la uso mpaka shingoni, kwa sababu ya kuenea kwa bakteria katika sehemu mbalimbali za mfumo wa hewa maambukizi hayo ufanya sehemu hizo kupooza yaani kuanzia kwenye sehemu ya paji la uso mpaka shiy kwa hiyo tunaona hali hii ni ya kuuumiza hasa kwa mtoto na kumsababishis ulemavu wa kudumu kwa sababu zisizi za msingi kama vile Imani potofu juu ya chanjo au kufanya uzembe katika kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa hiyo mtoto anakosa furaha na kupata ulemavu wa kudumu katika maisha yake.
3. Maambukizi yanaenea sana .
Kama ugonjwa huu haujadhibituwa usababisha maambukizi kwa watu wengine na kuleta madhara makubwa ambayo yanawaletea wengine ulemavu wa kudumu ambapo kama na wenyewe hawajatambua dalili mapema wanaweza kuendelea kuishi nao, basi jamii inapaswa kujua wazi dalili za ugonjwa huu wa Donda Koo na kujiadhari mapema kuhusu ugonjwa huu.
4. Kwa Sababu ya kuwepo kwa maumivu makali kwenye shingo, kushindwa kumeza na kupumua kwa mtoto, kuvimba shingo kwa mtoto na kupooza kwa mtoto kifo kinaweza kutokea ikiwa mamb o haya haya kutibiwa mapema, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa Dondakoo ni hatari kwa watoto na kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata chanjo na kama Kuna Imani potofu kuhusu chanjo jamii inabidi kuwa macho Ili kuondoa Imani hizi potofu.
5. Chanjo ambayo utolewa ni mchanganyiko wa chanjo ya kuzuia kifaduro, Pepopunda, Homa ya inni, hima ya uti wa mgongo, kwa Jina Moja huitwa pentavalent. Kwa hiyo mama au walezi wanaweza kuuliza wataalamu wa afya Ili kuhakikisha kama watoto wao wamepata chanjo ya Dondakoo Ili kuepusha madhara mbalimbali katika jamii yetu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.
Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu
Soma Zaidi...Kiasi gani cha maji kinatakiwa kunywa kwa siku?
Kunywa maji ya kutosha ni nguzo kuu ya afya bora, lakini swali la "ni kiasi gani hasa?" limekuwa likileta utata kwa muda mrefu. Makala haya yanachunguza sayansi nyuma ya mahitaji ya maji mwilini, ikivunja dhana potofu ya "glasi nane kwa siku," na kutoa mwongozo wa kitaalamu kulingana na umri, jinsia, kiwango cha mazoezi, na mazingira ya hali ya hewa.
Soma Zaidi...Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Soma Zaidi...Vidonda vya miguuni kwa wagonjwa wa kisukari.
Kwa nini vidonda vya miguuni ni hatari sana kwa mgonjwa wa kisukari? Sababu kuu ni mbili: Uharibifu wa neva (neuropathy) na mzunguko hafifu wa damu. Mgonjwa anaweza kujikata au kupata malengelenge na asihisi maumivu yoyote, hivyo kidonda kinakua na kuambukizwa bila yeye kujua. Makala haya yanakupa mwongozo wa jinsi ya kulinda miguu yako na nini cha kufanya jeraha linapotokea.
Soma Zaidi...