Athari za ugonjwa wa Dondakoo
Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.
1. Kupumua vibaya kwa mtoto na pengine mtoto anashindwa kumeza au anameza kwa shida.
Ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtoto zinaweza kuwa za kudumu au kwa mda tunajua kuwa ugonjwa huu ushambulia Koo mara nyingine Koo linapata maambukizi makubwa ambayo usababisha mtoto kushindwa kabisa kumeza au wengine wanafaulu kumeza Ila kwa shida kwa hiyo tunapaswa kutibu ugonjwa huu mapema na Tiba yenyewe ni kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa kufanya hivyo tutapunguza shida kwenye jamii na watoto tunawaandalia maisha mazuri na yenye natumaini.
2. Kupooza kuanzia kwenye paji la uso mpaka shingoni, kwa sababu ya kuenea kwa bakteria katika sehemu mbalimbali za mfumo wa hewa maambukizi hayo ufanya sehemu hizo kupooza yaani kuanzia kwenye sehemu ya paji la uso mpaka shiy kwa hiyo tunaona hali hii ni ya kuuumiza hasa kwa mtoto na kumsababishis ulemavu wa kudumu kwa sababu zisizi za msingi kama vile Imani potofu juu ya chanjo au kufanya uzembe katika kumpeleka mtoto kupata chanjo kwa hiyo mtoto anakosa furaha na kupata ulemavu wa kudumu katika maisha yake.
3. Maambukizi yanaenea sana .
Kama ugonjwa huu haujadhibituwa usababisha maambukizi kwa watu wengine na kuleta madhara makubwa ambayo yanawaletea wengine ulemavu wa kudumu ambapo kama na wenyewe hawajatambua dalili mapema wanaweza kuendelea kuishi nao, basi jamii inapaswa kujua wazi dalili za ugonjwa huu wa Donda Koo na kujiadhari mapema kuhusu ugonjwa huu.
4. Kwa Sababu ya kuwepo kwa maumivu makali kwenye shingo, kushindwa kumeza na kupumua kwa mtoto, kuvimba shingo kwa mtoto na kupooza kwa mtoto kifo kinaweza kutokea ikiwa mamb o haya haya kutibiwa mapema, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa Dondakoo ni hatari kwa watoto na kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata chanjo na kama Kuna Imani potofu kuhusu chanjo jamii inabidi kuwa macho Ili kuondoa Imani hizi potofu.
5. Chanjo ambayo utolewa ni mchanganyiko wa chanjo ya kuzuia kifaduro, Pepopunda, Homa ya inni, hima ya uti wa mgongo, kwa Jina Moja huitwa pentavalent. Kwa hiyo mama au walezi wanaweza kuuliza wataalamu wa afya Ili kuhakikisha kama watoto wao wamepata chanjo ya Dondakoo Ili kuepusha madhara mbalimbali katika jamii yetu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 kitabu cha Simulizi ๐2 ai web app ๐3 Madrasa kiganjani ๐4 web hosting ๐5 Dua za Mitume na Manabii ๐6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Sababu za ugonjwa wa mkojo kuwa na damu
Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu.
Soma Zaidi...Dalili za Ugonjwa wa Ebola.
Virusi vya Ebola ni virusi vinavyohusiana vinavyosababisha Homa zaรย hemorrhagic magonjwa yanayoambatana na kutokwa na damu nyingi (kuvuja damu), viungo kushindwa kufanya kazi na, mara nyingi, kifo. Virusi vya Ebola na virusi huishi kwa wanyama, na wanad
Soma Zaidi...Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu
Soma Zaidi...Dalili za minyoo ya tumbo
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.
Soma Zaidi...Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa wanawake na wanaume
Somo hili linakwenda kukueleza vitu vinavyosababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu
Soma Zaidi...