Post hii inahusu zaidi dawa ya cloxacillin ambayo Iko kwenye kundi mojawapo la penicillin ambalo uzuia enzymes zinazotengenezwa na bakteria.
1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba Kuna kundi mojawapo la penicillin ambalo usaidia kuzuia kazi ya bakteria ambao utoa enzymes Ili kuweza kuzuia kazi ya dawa kufanya kazi ipasavyo, hili kundi kwa kitaamu huiitwa penicillin resistance penicillase, kwa hiyo kwenye kundi hili Kuna dawa mojawapo ambayo huitwa cloxacillin, ni dawa ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kupambana na bakteria hao .
2. Dawa hii ya cloxacillin imo kwenye makundi ya penicillin na pia dawa hii usaidia kutibu au kuzuia kukua kwa bakteria kwenye seli, ambapo Kuna bakteria ambao ukua na kuzaliana kwenye seli kwa ajili ya kazi hii ya cloxacillin uzuia kukua na kuongezeka kwa bakteria kwenye seli na hivyo usaidia seli kuendelea na kazi zake za kuulinda na kuutunza mwili.
3. Vile vile dawa hii ya cloxacillin usaidia katika matibabu ya kwenye Koo , na pia usaidia kwenye matibabu ya mafua na vikohozi kwa ujumla, pia kwenye damu usaidia kuuua kila aina yeyote ya bakteria ambao ufanya kazi ya kuudhuru mwili kwa hiyo ni dawa nzuri kwa maambukizi ya bakteria kwenye damu.
4. Pia dawa hii huwa kwenye unga ambapo unga huo uchanganywa na maji rasmi ambayo Kwa kitaamu huiitwa water for injection na pia maji hayo na unga uchanganywa mpaka kuhakikisha hiyo poda haionekani kwa macho ila maji tu yaliyochanganyikana na dawa na pia dozi upewa kutegemea a na umri, kwa mtoto na mtu mzima na uzito pia. Kwa kawaida makasha ya dawa huwa na milligrams tofauti Kuna mengine Yana milligrams mia mbili hamsini na mengine milligrams mia tano zote utolewaa kulingana na wataalamu wa afya.
5. Dawa hizo utolewa kwa kupitia kwenye paja au Tako na utolewa kila masaa manane mpaka sita kadri ya maagizo ya wataalamu wa afya, na pia dawa hizi zinaweza kupitia kwenye damu , za kwenye damu utolewa taratibu na zenyewe utolewa kuanzia masaa manne mpaka matano kadri ya wataalamu wa afya. Vile vile Kuna nyingine uweza kuwa kwenye mfumo wa maji maji na pia kwenye vidonge kwa hiyo zote utolewa kwa mgonjwa kwa kadri ya uhitaji au tatizo kwa sababu dawa hii utibu magonjwa mengi.
6. Dawa hii ya cloxacillin utolewa na watu mbalimbali ila wale wenye aleji na dawa hii hawapaswi kuitumia, na pia wakati wa kutumia dawa hii umaskini unahitajika kwa sababu dawa Ina tabia ya kupunguza damu kwa hiyo wale wenye tatizo la upungufu wa damu wanapaswa kuitumia kwa taahadhari au kwenye uangalizi maalumu Ili kuweza kuzuia kuwepo kwa tatizo jingine au kusababisha Anaemia.
7. Dawa hii ya cloxacillin Ina maudhi madogo madogo wakati wa kutumia na maudhi hayo ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, maumivu ya tumbo kuhisi kizunguzungu na wakati mwingine kuishiwa hamu ya kula, kupungukiwa damu, kwa hiyo kwa watumiaji baada ya kuitumia dawa hii mambo kama haya yanaweza kutokea kwa hiyo taahadhari ni muhimu ila hali ikiwa mbaya ni vizuri kuwaona wataalamu wa afya hasa kwa upande wa upungufu wa damu.
8. Pamoja na hayo yote ikumbukwe kwamba dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela ila kinapaswa kuwepo kwa wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara amabayo ya aweza kutokea , kwa sababu ikitumiwa nyumbani na mgonjwa mweye upungufu wa damu na dawa ikaendelea kupunguza damu ,hali inawezekana kuwa mbaya badala ya kutibu tunaleta tatizo juu ya tatizo.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi dawa ya aminophylline katika kutuliza maambukizi kwenye mfumo wa upumuaji.
Soma Zaidi...PoPosti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo unaweza kutumia iwapo umepata tatizo la kiungulia
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya paracetamol katika kutuliza maumivu, ni Aina ya dawa ambayo utumiwa sana katika kutuliza maumivu kwa wagonjwa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa za Doxorubicin and Daunorubicin katika kupambana na kansa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu dawa za kifua kikuu ni dawa ambazo utumika kutibu kifua kikuu, kwanza kabisa kabla ya kuanza kufahamu dawa hizo ni vizuri kabisa kufahamu kifua kikuu nini hili kuweza pia kufahamu dawa zake.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya cardiac glycoside katika matibabu ya magonjwa ya moyo,dawa maalum ambayo imo kwenye kundi hili la cardiac glycoside ni digoxin, ni dawa muhimu ambayo utumika kwenye mfumo wa vidonge mara nyingi.
Soma Zaidi...