Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA TENDO LA NDOA

 

Maumivu wakati wa tendo la ndoa hutokea sana na pengine ni kawaida hasa kwa wanawake. Ijapokuwa kwa wanaume sio sana. Maumivu haya yanaweza kuwa ya tumbo, ya kiuno, ama viungo vya siri yaani uume na uke. Pia maumivu haya yanaweza kutokea wakati wa tendo la ndoa ama baada.

 

Je na wewe ni katika wanaopatwa na maumivu makali wakati wa tendo la ndoa. Na je umepata kujuwa chanzo cha tatizo lako?. makala hii ni kwa ajili yako. Katika makala hii tutakwenda kuona maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.

 

Sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.1.Mkao uliotumika. Ipo baadhi ya mikao inaongeza uwezekano wa kupatwa na maumivu ya tumbo wakati wa tendo. Mikao hii ni ile ambayo inaruhusu uume kuingia ndani zaidi. Kama unasumbuliwa na tatizo hili jaribu kutumia mikao ambayo utaweza kudhibiti uingiaji wa uume.

 

2.Kama tumbo la uzazi (uterus) limeinama kidogo. Hii hutokea pale tumbo la uzazi linapolalia nyuma kidogo kuelekea kwenye shingo ya uzazi. Hali hii huwewa kupelekea maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.

 

3.Maka una tatizo la kuota tishu zinazopaswa kuota kwenye tumbo la uzazi zikaota sehemu nyingine. Hali hii hutambulika kama endometruisis. Haki hii huweza kupelekea maumivu ya mgongo, nyonga na tumbo wakati wa tendo la ndoa. Dalili za hali hii ni pamoja na:-

 

A.Maumivu makali zaidi wakati wa tendo la ndoaB.Kupata hedhi yenye damu nyingiC.Kutokwa na damu kabla na baada ya kumaiza hedhiD.Maumivu ya tumbo

 

4.Kama ovari ina matatizo yaani inajaa maji, hali hii hutambulika kama ovarian cysts. Hii hutokea endapo juu y aovari ama ndani kunkuwa na kama vijifuko vijidogo vinajaa maji. Sasa vikiwa vidogo havinaga maumivu ila vikiwa ni vikubwa vinaweza kupelekea maumivu ya chini ya tumbo. Maumivu haya yanaweza kuwa makali zaidi wakati wa tendola ndoa. Pia mtu anaweza kupata dalili zifuatazo:-

 

A.Maumivu ya mgongo wa chini ama kwenye mapajaB.Unahisi tumbo limejaa ama kushiba, ama tumbo linakuwa zitoC.Tumbo kujaa gezi na kucheua gesi kwa mdomoni.

 

5.Kama kuna mashambulizi kwenye kibofu kitaalamu hali hii huitwa interstial cystitis. Misuli ya kwenye kibofu inashambuliwa na kuvimba na baadaye kutoa dalili kama:-A.Maumivu ya tumbo na nyongaB.Kukojoa mara kwa maraC.Kujihisi kukojoa tena punde baada ya kukojoaD.Kuvuja kwa mkojo yaani kutoka mkojo bila ya wewe kujuwa.E.Maumivu kwenye uke na mashavu ya uke (papa)

 

6.Kuwa na uvimbe kwenye tumbo la mimba kitaalamu huitwa fibroid. Huu ni uvimbe usiosabababishwa na saratani. Uvimbe huuu huweza kuleta dalili kama:-A.maumivu ya tumbo na mgongo sehemu ya chiniB.Kupata damu nyingi ya hedhi pamoja na maumivu makaliC.Maumivu wakati wa tendo la ndoaD.Kukosa choo.

 

7.Kama mtu ana maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Hapa mtu anaweza kuona dalili kama:-A.Kutokwa na uchafu ukeniB.Kutoka na harufu mbaya ukeniC.Maumivu wakati wa kukojoa na kuhisi kama unaunguwaD.Maumivu ya tumbo kwa chini pamoja na nyongaE.Maumivu na kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada ya hedi

 

8.UTI na PID; kwa pamoja haya ni mashambuizi ya bakteria ama fangasi ama virusi. Mashambulizi haya huathiri mfumo wa uzazi hapa itakuwa na PID na endapo yatashambulia mfumo wa mkojo itakuwa ni UTI. ugonjwa wa UTI na PID huweza kusababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa.

 

Dalili za PIDA.Maumivu makali ya nyonga wakatii wa tendo la ndoaB.Maumivu wakati wa kukojoaC.Kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada

 

Dalili za UTIA.Maumivu ya tumbo ambayo huongezeka wakati wa tendo la ndoaB.Maumivu wakati wa kukojoaC.Kukojoa mra kwa maraD.Mkojo mchafu na wenye harufu kali.

 

9.kama kuna uvimbe katika tezi dume.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1980

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za maumivu ya hedhi
Dalili za maumivu ya hedhi

Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine,&nbsp

Soma Zaidi...
Sababu za uke kuwa na harufu mbaya.
Sababu za uke kuwa na harufu mbaya.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa harufu mbaya kwenye uke ukizingatia usafi huwa unafanyika mara kwa mara ila harufu bado inaendelea kuwa mbaya kwa hiyo tutaona sababu hapo chini.

Soma Zaidi...
Njia za kuondoa fangasi sehemu za siri
Njia za kuondoa fangasi sehemu za siri

Makala hii itakujuza baadhi ya njia utakaoweza kuzifuata ili kukabiliana na fangasi sehemu za siri kwa wanaume

Soma Zaidi...
Namna za kujilinda na  fangasi  ukeni
Namna za kujilinda na fangasi ukeni

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
 Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa
Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa

Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mar

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

Utajifunza sababua zinazopelekea kuhisi maumivu makali ya tumbo baada ya kumaliza tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa kondo la nyuma
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa kondo la nyuma

Kondo la nyuma ni sehemu ya mwili wa mama anapokuwa mjamziti,kondo la nyuma husaidia katika kazi mbalimbali katika ukuaji wa mtoto.

Soma Zaidi...
Dawa hatari kwa mwenye ujauzito
Dawa hatari kwa mwenye ujauzito

Hii ni orodha ya dawa ambazo hutumiwa sana na watu kutoka maduka ya dawa lakini sio salama kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Kazi za homoni katika  Mzunguko hedhi.
Kazi za homoni katika Mzunguko hedhi.

Post hii inahusu zaidi kazi za homoni katika Mzunguko wa hedhi, katika kipindi hiki kuna homoni mbalimbali ambazo ufanya kazi kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...