Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kitunguu thaumu
FAIDA ZA KITUNGUU THAUMU
Kitunguu thaumu ni katika viungo vya mboga na chakula. Karibia maeneo yote duniani wanatumia kitungiuu thaumu. Kitunguu thaumu huweza kutumika kikiwa kibichi. Wataalamu wa afya wanaeleza faida nyingi za kiafya. Wataalmu wa afya wametengeneza kidonge kwa kutumia vitunguu thaumu ili kuwezesha upatikanaji wa virutubisho vya mmea huu.
Kitunguu thaumu kina chembechembe nyingi ambazo ndizo husaidia katika tiba. Miongoni mwa chembechembe hizo ni chembechembe za salfa ziitwazo allicin. Allicin hupatikana kwenye kitunguu kibichi pindi kinapopondwa ama kutafunwa. Chembechembe nyingine ni kama diallyl disalfide na s-allyl cysteine.
Zifuatazo ni faida za kiafya za kitunguu thaumu
1. Kunapatikana virutubisho vingi ndani ya kitunguu thaumu kama vitamini B6, B1 na vitamini C. madini ya calcium, copper, phosphoros, potassiumna selium.
2. Hushusha presha ya damu (hypertsnsion). kitunguu thaumu sio kizuri kwa wenye presha ya kushuka, kwani itashuka sana.
3. Hudhibiti cholesterol (kolesto) hivyo husaidia katika kuzuia hatari ya kupata maradhi ya moyo.
4. Kitunguu thaumu kina antioxidant ambazo husaidia kupunguza hatari ya kupata maradhi ya kusahausahau
5. Huimarisha mfumo wa kinga mwilini.
6. Huondoa sumu za vyakula mwilini.
7. Huimarisha afya ya mifupa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Umeshawahi kuumwa na dawa yako ikawa maji? Huwenda bado basi hapa nitakujuza kidogo tu, juu ya jambo hili.
Soma Zaidi...Hivi ni vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo. mwenye vidonda vya tumbo hatakiwi kula vyakula hivi
Soma Zaidi...Hpa utafahamu faida za maji mwilini pamoja na athari za upungufu wa maji mwilini na dalili zake
Soma Zaidi...Nashukuru kwa ushauri, Je!
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukutajia mahonjwa matano ambayo hutokana na utapia mlo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula viazi vitamin
Soma Zaidi...Kama tulivyosema hapo juu kuwa afya ni kuwa mzima kimwili na kiakili.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya vyakula vyenye vitamini C kwa wingi
Soma Zaidi...