Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
Haki za Maadui Katika Vita (mateka wa Kivita).
Uislamu unajali, kusimamia na kulinda haki ya kila mtu hata kwa maadui waliokamatwa katika vita (mateka) walifanyiwa haki na uadilifu kama ifuatavyo;
Kuhurumiwa na kutofanyiwa ukatili wowote maadamu wamedhibitiwa.
Kuwapa mahitaji yao ya lazima ya kibinaadamu na kimaisha pia.
Kulinda uhai na usalama wa maisha yao mpaka mwisho wa uhasama.
Mateka wa kivita walikuwa na haki ya kujikomboa kwa njia zifuatazo;
Kulipa kiasi fulani cha pesa au mali yeyote inayokubalika.
Kubadilishana na mateka Waislamu waliokamatwa na maadui.
Kulipa fidia kwa kufanya jambo fulani lenye manufaa kwa jamii ya waislamu.
Rejea Quran (47:4).
Masuria na mateka wanawake walikuwa na haki ya kulindwa na kuhifadhiwa kwa kupewa wanaume waliokwenda vitani na kuishi nao katika maisha ya ndoa ili kupata mahitaji yao ya msingi.
Haki ya kumiliki mali au uchumi ulio wa halali na usio leta madhara yeyote katika Dola ya Kiislamu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 web hosting 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Hutuba ya Ndoa - Khutbat nikah
Hii ni hutuba ya ndoa kwa ufupi, Imekusanya mambo ya msingi yanayohitajika katika hutuba ya ndoa
Soma Zaidi...Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu
(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.
Soma Zaidi...