Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini

Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha.

Namna ya Kumkafini Maiti

Kumkafini maiti au kumvalisha sanda ni Faradhi Kifaya. Nguo nzuri ya kutumia kwa ajili ya sanda ni nguo nyeupe ya pamba kama tunavyofahamishwa katika Hadithi ifuatayo:


Ibn Abbas amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema: Vaeni nguo nyeupe, kwa sababu hilo ni vazi lenu lililo bora kuliko yote, na wakafinini maiti wenu nguo (nyeupe). (Abu Daud, Tirmidh na Ibn Majah).

 


Pia ni vyema nguo hiyo isiwe ya gharama kubwa na nguo iliyotumika ni bora zaidi kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifu atayo:

 


Ali (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Msigharamie sana nguo ya sanda, kwani inakwenda kuozeana (kaburini)”. (Abu Daud).

 

Hajj (mwenye kuhiji) akifa wakati wa Hija, akiwa bado kwenye “Ihram” (vazi rasmi la kuhijia - shuka mbili nyeupe zisizo shonwa), Ihram yake huwa ndio sanda na kichwa chake kubakia wazi bila ya kufunikwa kama tunavyofahamishwa katika Hadithi:

 


Abdullah bin Abbas(r.a) amesimulia kuwa mtu mmoja alikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) ngamia wake alimkanyaga, wakati akiwa anahiji mpaka akafa, Mtume wa Allah akasema:“Muosheni na maji na majani ya mkunazi na mumkafini kwa hayo mashuka yake mawili, msimpake manukato na msimfunike kichwa chake, na hakika siku ya Kiyama atafufuliwa akiitikia Labbaika. (Bukhari na Muslim).

 


Ukubwa wa kitambaa cha sanda utategemea ukubwa wa maiti. Sanda ya mwanamume ina vipande vitatu vilivyo sawa sawa na sanda ya mwanamke ina vipande vitano.

 


Sanda ya Mwanamume na Namna ya Kuivika

 


Sanda ya mwanamume ina vipande (majamvi) vitatu. Utaratibu wa kutayarisha sanda na kukafini ni kama ifuatavyo:
1. Weka kipande cha kwanza juu ya mkeka au jamvi, kisha cha pili na cha tatu na kila kipande kifukizwe ubani na kupakwa marashi. Vipande vyote hivi vitatu vishikizwe na uzi katikati.

 


2. Pasua kamba katika pembe mbili za jamvi la kwanza, kamba moja kwa ajili ya kufungia kichwani na nyingine ya kufungia miguuni. Kamba nyingine ya kumfungia maiti katikati itatolewa kwenye jamvi la pili. Kamba nyingine tatu za kufungia juu ya mkeka zitatoka kwenye jamvi la pili na la tatu.

 


3. Maiti italazwa juu ya vipande vyote vitatu. Ichukuliwe pamba iwekwe manukato kisha iwekwe juu ya viungo vyote vya sijda - kipaji cha uso, viganja vya mikono, magotini na kwenye vidole vya miguu; pia pamba hiyo itumike kuzibia matundu yote mwilini - mdomo, pua, masikio na makalio.

 

4. Maiti itatatizwa na kipande cha kwanza mpaka kimuenee - kwa kuanza kutatiza kunjo la kushoto, kisha kunjo la kulia lije juu. Vipande viwili vilivyobaki vitatizwe kama hicho cha kwanza. Kisha zile kamba zitumike kufunga vitanzi kichwani, miguuni na tumboni ili sanda isije vuka na kumuacha maiti uchi. Katika hali hii maiti itakuwa tayari kwa kuswaliwa. Inaweza kuwekwa kwenye jeneza hivyo hivyo au inaweza kuzungushiwa mkeka kwanza ndio iwekwe kwenye jeneza.

 


Sanda ya Mwanamke na Namna ya Kumvika

 


Sanda ya mwanamke kawaida inavipande vitano. Vipande vikubwa viwili sawa na vile vya sanda ya mwanamume. Kipande cha tatu ni shuka au gagulo (under skirt), kipande cha nne ni kanzu na kipande cha tano ni ukaya au kipande cha nguo cha kufunikia kichwa na uso. Utaratibu wa kutayarisha sanda na kukafini ni kama ifuatavyo:
1. Vipande vikubwa viwili vitatandikwa kimoja hadi kingine kama inavyofanywa kwa sanda ya mwanamume.

 


2. Kikatwe kitambaa cha ukubwa wa shuka ya kawaida ya kufunga kiunoni. Kisha kipande hiki kiwekwe juu ya vipande viwili vikubwa katika sehemu ya chini atakapolazwa maiti ili shuka hii itatizwe kiunoni kama mtu anayefunga shuka ya kawaida.

 


3. Kisha ikatwe kanzu ambayo haishonwi vizuri, kwa kukunja kitambaa na kutoboa katikati ili iwe sehemu ya kuingiza kichwa wakati wa kuvalisha na kushikiza pembeni kwa uzi kufanya mfano wa kanzu kata mikono. Kanzu itatandikwa juu ya kipande kikubwa cha pili katika sehemu ya juu na sehemu ya chini itakuwa juu ya ile shuka (gagulo) baada ya kuwekwa manukato na kufukizwa ubani.

 


4. Kitambaa cha ukaya cha kutosha kufunika kichwa na uso kitaingizwa ndani ya shingo ya kanzu na kunyooshwa kwa juu. Baada ya hapo matayarisho ya sanda ya mwanamke yatakuwa yamekamilika.

 

5. Maiti ataanza kuvalishwa kanzu, kisha juu yake atafungwa shuka. Kisha atawekwa pamba yenye manukato viungo vyote vya sijda pamoja na sehemu zote za matundu kama inavyofanywa kwa maiti ya mwanamume. Baada ya hapo, maiti itatatizwa na vipande vikubwa viwili kimoja baada ya kingine, kila mara kunjo la kulia likiwa juu na itafungwa vile vile kwa kamba tatu - miguuni, tumboni na kichwani na kuwa tayari kuingizwa kwenye jeneza na kuswaliwa.

 


Sanda ya Watoto
Sanda ya watoto wadogo, wa kike au wa kiume ni vipande vitatu tu kama ile ya wanaume wakubwa.
Namna ya kumswalia Maiti
Swala ya maiti au swala ya jeneza ni faradhi kifaya. Ni faradhi kifaya kwa sababu ikifanywa na wachache au na mtu mmoja tu katika jamii inatosheleza na Waislamu wote wanasalimika na ghadhabu za Allah (s.w).

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/15/Monday - 08:25:26 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 963


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Fadhila za kusoma Quran na umuhimu wa kusoma Quran
Unazijua faida za kusoma Quran, na je ni faida gani utapata ukisoma Quran? Soma Zaidi...

Jinsi ya kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii itakufundisha taratibu za kuzika maiti wa kiislamu hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Baqarah
Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii. Soma Zaidi...

Nini kifanyike baada ya mazishi ya kiislamu
Huu ni utaratibu unaotakiwa kufanyika baada ya kuzika. Soma Zaidi...

Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa
Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki. Soma Zaidi...

Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea
Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir Soma Zaidi...

Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno
Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Fatiha (Alhamdu)
Post hii inakwenda kufundisha fadhila na faida za kusoma Alhamdu. Soma Zaidi...

Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini
Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha. Soma Zaidi...

Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...

Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia
Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi. Soma Zaidi...

Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...