Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Istikhaarah maana yake ni kuomba uchaguzi au aumuzi katika jambo. Na Swalaah ya Istikhaarah hakika ni zawadi kubwa tuliyopewa sisi Umma wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwani ina faida kubwa sana kwetu kwani hatuamui jambo letu tunaloliomba katika Swalaah hii, ila baada ya kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Atuongoze Yeye hilo jambo kama lina kheri na sisi Atufanikishe nalo na kama ni la shari Atuepushe nalo. Yeye Pekee Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Mwenye kujua ya ghayb yaani yatakayotokea siku za mbele.

 

 

Na ndio ilivyokuja katika Du'aa kuwa tunasema:

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْتَخيـرُكَ بِعِلْمِك، وَأسْتَقْـدِرُكَ بِقُـدْرَتِـك، وَأَسْـألُـكَ مِنْ فَضْـلِكَ العَظـيم، فَإِنَّـكَ تَقْـدِرُ وَلا أَقْـدِر، وَتَـعْلَـمُ وَلا أَعْلَـم، وَأَنْـتَ عَلاّمُ الغُـيوب، اللّهُـمَّ إِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ (وَيُسَـمِّي حاجته) خَـيْرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، عَاجِلِهِ و آجِلِه , فَاقْـدُرْهُ لي وَيَسِّـرْهُ لي ثـمَّ بارِكْ لي فيـه، وَإِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ شَـرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، عَاجِلِهِ و آجِلِه فَاصْرِفْـهُ عَنّيِ وَاصْرِفْني عَنْـهُ وَاقْـدُرْ ليَ الخَـيْرَ حَيْـثُ كانَ ثُـمَّ أَرْضِـني بِـه.

Ee Allaah hakika mimi nakutaka (muongozo) unichagulie kwa ujuzi Wako, na nakuomba Uniwezeshe kwa uwezo Wako, na nakuomba fadhila Zako kubwa, hakika Wewe Unaweza, nami siwezi, Nawe unajua nami sijui, Nawe ni Mjuzi wa ya ghayb. Ee Allaah, iwapo jambo hili kutokana na ujuzi Wako (utalitaja jambo lako) lina kheri na mimi katika Dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu, katika Dunia yangu na Aakhirah yangu, basi nakuomba Uniwezeshe nilipate, na Unifanyie wepesi, kisha Unibariki. Na iwapo Unajua kwamba jambo hili ni shari kwangu katika Dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu, katika Dunia yangu na Aakhirah yangu, basi liepushe na mimi nami niepushe nalo, na nipangie jambo jengine lenye kheri nami popote lilipo, kisha niridhishe kwalo. [Al-Bukhaariy]

 

 

Kwa hiyo inampasa Muislamu awe anaitumia sana Swalaah hii kwa kila jambo lake, likiwa ni dogo au kubwa kwani juu ya kupata faida ya kwamba unamuachia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Mwenye Ujuzi na Mwenye Hikma kutuongoza, pia unapata thawabu za kuswali Raka'ah mbili.

 

Lakini haifai kuswali Swalaah hii kwa ajili ya maasi na maovu au hata katika ‘ibaadah za fardhi. Mfano mwizi haimpasi kuiswali Swalaah hii ili atake uamuzi kama akaibe au la. Au mwanamke asiiswali Swalaah hii ikiwa yuko katika wasiwasi wa shaytwaan unaotaka kumpelekea kufanya zinaa na kadhalika.

Vile vile asiswali mtu Swalaah hii katika kutimiza fardhi; mfano katika kutoa Zakah au jambo la kheri kama swadaqah na kadhalika, kwani huo ni wasiwasi wa shaytwaan kukuzuia kutenda hayo yanayopasa kutendwa.

 

 

Swalaah hii inaweza kutumika katika mambo yanayofaa mfano unataka kwenda safari, au umeomba kazi katika shirika fulani, au unataka kuoa au mwanamke amekuja kuposwa na kadhalika.

 

Vile vile unapokuwa na uamuzi wa mambo mawili na hujui jambo lipi mojawapo ni lenye kheri, mfano unayo akiba yako ya fedha na kuna fursa ya kufungua mojawapo ya biashara za aina mbili, sasa hujui biashara gani katika hizo ndio yenye kheri na wewe, hapo utaswali ili upate mwongozo wa biashara itakayokuwa na kheri na wewe.

 

Kisha baada ya kuswali Swalaah hii kwa mambo yanayofaa kuiswalia, inakuwa umeshamuachia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akuongoze, kwa hiyo vyovyote utakavyoamua itakuwa ndio mwongozo Wake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na itakuwa ndio kheri yako.

 

 

Si lazima mtu aote ndoto kama wanavyofikiria baadhi ya watu baada ya kuswali Swalaah hii.

 

 

Swalaah hii haiswaliwi kwa niyyah kuomba haja kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) unapotaka kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) haja yoyote, ni kuomba Du'aa mwenyewe kama kawaida ikiwa ni katika Swalaah au nje ya Swalaah

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1711

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.

Soma Zaidi...
Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Soma Zaidi...
Maana ya zakat

Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani

Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.

Soma Zaidi...
Faida na umuhimu wa ndoa katika jamii

Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi

Soma Zaidi...
Maandalizi kwa ajili ya kifo

Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo.

Soma Zaidi...