Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali.
- Ni vile vipengele vinavyokamilisha swala kama ifuatavyo;
Nia (dhamira moyoni).
takbiira ya kuhirimia
kusoma suratul-Fatihah
kurukuu
kujituliza katika rukuu
kuitidali
kujituliza katika itidali
kusujudu
kujituliza katika Sijda
kukaa kati ya Sijda mbili
kujituliza katika kikao kati ya sijda mbili
kusujudu mara ya pili
kujituliza katika sijda ya pili
kukaa Tahiyyatu
kusoma Tahiyyatu
kumswalia au kumtakia rehema na amani Mtume (s.a.w) na waislamu
kutoa salaam
kufuata utaratibu huu (1-17) kwa mfuatano
Makundi manne ya nguzo za swala
Nia.
Nguzo za matamshi (visomo)
Takbiira ya kuhirimia swala
Kusoma Suratul-Fatihah
Kusoma Tahiyyatu
Kumswalia Mtume (s.a.w)
Kutoa Salaam
Nguzo za vitendo
- Ukiondoa nguzo ya ‘Nia’ na ‘kufuata utaratibu’ zilizobaki ni nguzo za vitendo.
.Kufuata utaratibu
- Ni yale mambo akiyafanya mwenye kuswali, hupandisha daraja ya swala yake
Kuinua viganja vya mikono usawa wa mabega
Kusoma dua baada ya Takbiira ya kuhirimia
Kuanza kwa “Audhubillah” kabla ya kusoma Suratul-fatihah
Kuitikia “Aamin” baada ya kumaliza kusoma Suratul-Fatihah
Kusoma aya za Qur’an baada ya kusoma suratul-Fatihah rakaa mbili za mwanzo
Kusoma Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali, sijda, n.k.
Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili.
Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume (s.a.w).
Namna ya kutekeleza Nguzo na Sunnah za Swala hatua kwa hatua
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 100-110
Sijda ya kawaida katika swala
Sijdatut-Tilaawat (Sijda ya kisomo) – ni Sijda ya sunnah ailetayo msoji au msikilizaji wa Qur’an pale atakaposoma aya inayotaja sijda.
Aya za sijda ndani ya Qur’an ziko 15.
(7:206), (13:15), (16:50), (17:109), (19:58), (22:18), (22:77), (25:60), (27:26), (32:15), (38:24), (41:38), (53:62), (84:21) na (96:19).
Sijdatus-Sah-wi (Sijda ya kusahau) – ni sijda anayoileta mtu kabla ya kutoa salaam ili kufidia kitendo cha sunnah alichokisahau katika swala.
Mambo yanayobatilisha (yanayoharibu) Swala
Kutoelekea Qibla bila dharura (udhuru) wowote kisheria.
Kupatikana na hadathi kubwa (hedhi/nifasi), ndogo (kutengukwa udhu) au ya kati na kati (janaba).
Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
Kuvukwa na nguo ukawa uchi – mgongoni, kiunoni, kitovuni, n.k. (tahadhari kuvaa mashati mafupi, madogo kwa wanaume).
Kusema au kutamka makusudi walau herufi moja isiyo na mahusiano na ibada ya swala.
Kula au kunywa chochote hata kwa kusahau.
Kufanya kitendo/jambo lisilohusiana na swala mfululizo mara tatu.
Kuacha nguzo yeyote ya swala.
Kuzidisha nguzo yeyote ya swala makusudi.
Kumtangulia imamu au kumchelewa (ukiwa maamuma) kwa nguzo mbili za kimatendo mfululizo na makusudi.
Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni uikate swala au usiikate.
Kuwa na shaka kuwa umetimiza au haujatimiza sharti au nguzo yeyote ya swala.
Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
Kutoa salaam makusudi kabla ya kuisha swala.
Kuswalishwa kwa asiyekuwa muislamu.
Kukhalifu (kutofuata) utaratibu wa Nguzo za swala katika mpangilio wake.
Kuleta dua ya kuomba kitu cha haramu au muhali.
Kumshirikisha Allah (s.w) kwa kuleta dua au maombi.
Khushui (Unyenyekevu) katika Swala
Ni jambo la tatu katika kusimamisha swala
Maana ya Khushui – Ni kujituliza kimwili na kifikra na kuzingatia yale mja anayotenda na kusema katika swala.
Namna ya kupata Khushui katika Swala 1.Kuutuliza mwili
- Utulivu wa mwili hupatikana kwa kutojipapasa papasa, kutochezesha viungo na kuangalia pale tu unaposujudia.
2.Kuzituliza fikra (moyo)
- Fikra hutulia kwa kurejesha na kubakisha mawazo yote ndani ya swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.
3.Kuwa na mazingatio
- Mazingatio hupatikana kwa kujua maana pamoja na kuwa makini na kile unachokisema au unachokitenda ndani ya swala.
Namna ya kufikia Lengo la Swala
- Ni kutekeleza sharti zote za Swala kikamilifu kabla ya kuanza kuswali.
- Ni kutekeleza kikamilifu nguzo zote za swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.
Rejea Qur’an (29:45), (20:14), (7:205), (107:4-6).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali
Nyuma
Endelea
Umeionaje Makala hii.. ?
Nzuri Mbaya Save
Author:
Rajabu
Tarehe:
1970-01-01 03:33:44
Topic:
Fiqh
Main:
Dini
File:
Download PDF
Views
3205
Post zinazofanana:
Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.
Soma Zaidi...
Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.
Soma Zaidi...
Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo.
Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...
Ni kipindi au muda wa kungojea mwanamke aliyepewa talaka (aliyeachwa) au kufiwa na mumewe kabla ya kuolewa na mume mwingine.
Soma Zaidi...
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.
Soma Zaidi...