image

Nguzo za swala.

Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali.

- Ni vile vipengele vinavyokamilisha swala kama ifuatavyo;

  1. Nia (dhamira moyoni).
  2. takbiira ya kuhirimia
  3. kusoma suratul-Fatihah
  4. kurukuu
  5. kujituliza katika rukuu
  6. kuitidali
  7. kujituliza katika itidali
  8. kusujudu
  9. kujituliza katika Sijda
  10. kukaa kati ya Sijda mbili
  11. kujituliza katika kikao kati ya sijda mbili
  12. kusujudu mara ya pili
  13. kujituliza katika sijda ya pili
  14. kukaa Tahiyyatu
  15. kusoma Tahiyyatu
  16. kumswalia au kumtakia rehema na amani Mtume (s.a.w) na waislamu
  17. kutoa salaam
  18. kufuata utaratibu huu (1-17) kwa mfuatano
  1. Nia.
  2. Nguzo za matamshi (visomo)
  3. Takbiira ya kuhirimia swala
  4. Kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma Tahiyyatu
  6. Kumswalia Mtume (s.a.w)
  7. Kutoa Salaam
  8. Nguzo za vitendo

-    Ukiondoa nguzo ya ‘Nia’ na ‘kufuata utaratibu’ zilizobaki ni nguzo za vitendo.

.Kufuata utaratibu

-     Ni yale mambo akiyafanya mwenye kuswali, hupandisha daraja ya swala yake

  1. Kuinua viganja vya mikono usawa wa mabega
  2. Kusoma dua baada ya Takbiira ya kuhirimia
  3. Kuanza kwa “Audhubillah” kabla ya kusoma Suratul-fatihah
  4. Kuitikia “Aamin” baada ya kumaliza kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma aya za Qur’an baada ya kusoma suratul-Fatihah rakaa mbili za mwanzo
  6. Kusoma Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali, sijda, n.k.
  7. Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili.
  8. Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume (s.a.w).

Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 100-110

Aya za sijda ndani ya Qur’an ziko 15. 

(7:206), (13:15), (16:50), (17:109), (19:58), (22:18), (22:77), (25:60), (27:26), (32:15), (38:24), (41:38), (53:62), (84:21) na (96:19).

 

 

  1. Kutoelekea Qibla bila dharura (udhuru) wowote kisheria.
  2. Kupatikana na hadathi kubwa (hedhi/nifasi), ndogo (kutengukwa udhu) au ya kati na kati (janaba).
  3. Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
  4. Kuvukwa na nguo ukawa uchi – mgongoni, kiunoni, kitovuni, n.k. (tahadhari kuvaa mashati mafupi, madogo kwa wanaume).
  5. Kusema au kutamka makusudi walau herufi moja isiyo na mahusiano na ibada ya swala.
  6. Kula au kunywa chochote hata kwa kusahau.
  7. Kufanya kitendo/jambo lisilohusiana na swala mfululizo mara tatu.
  8. Kuacha nguzo yeyote ya swala.
  9.  Kuzidisha nguzo yeyote ya swala makusudi.
  10. Kumtangulia imamu au kumchelewa (ukiwa maamuma) kwa nguzo mbili za kimatendo mfululizo na makusudi.
  11. Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni uikate swala au usiikate.
  12. Kuwa na shaka kuwa umetimiza au haujatimiza sharti au nguzo yeyote ya swala.
  13. Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
  14. Kutoa salaam makusudi kabla ya kuisha swala.
  15. Kuswalishwa kwa asiyekuwa muislamu.
  16. Kukhalifu (kutofuata) utaratibu wa Nguzo za swala katika mpangilio wake.
  17. Kuleta dua ya kuomba kitu cha haramu au muhali.
  18. Kumshirikisha Allah (s.w) kwa kuleta dua au maombi.

 

Ni jambo la tatu katika kusimamisha swala

 

Maana ya Khushui – Ni kujituliza kimwili na kifikra na kuzingatia yale mja   anayotenda na kusema katika swala.

-     Utulivu wa mwili hupatikana kwa kutojipapasa papasa, kutochezesha viungo na kuangalia pale tu unaposujudia.

 

2.Kuzituliza fikra (moyo)

-     Fikra hutulia kwa kurejesha na kubakisha mawazo yote ndani ya swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

 

3.Kuwa na mazingatio

-  Mazingatio hupatikana kwa kujua maana pamoja na kuwa makini na kile unachokisema au unachokitenda ndani ya swala.       

 

-     Ni kutekeleza sharti zote za Swala kikamilifu kabla ya kuanza kuswali.

-     Ni kutekeleza kikamilifu nguzo zote za swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

      Rejea Qur’an (29:45), (20:14), (7:205), (107:4-6).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1804


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Sanda ya mwanaume na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hii ndio namna ya kuswali kama alivyoswali Mtume s.a.w
Mtume (s. Soma Zaidi...

Umuhimu wa funga ya ramadhan
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Vituo vya kunuia hijjah au umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

Je ni nani mwenye haki ya kutaliki
Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye. Soma Zaidi...

Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo. Soma Zaidi...

Hukumu na taratibu za ndoa katika uislamu
Soma Zaidi...

umuhimu wa swala katika uislamu
Soma Zaidi...

benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato
Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba. Soma Zaidi...

Tofauti kati ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Funga za kafara, aina zake na sababu za funga hizi za kafara na hukumu zake
Soma Zaidi...