Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali.
- Ni vile vipengele vinavyokamilisha swala kama ifuatavyo;
- Nia (dhamira moyoni).
- takbiira ya kuhirimia
- kusoma suratul-Fatihah
- kurukuu
- kujituliza katika rukuu
- kuitidali
- kujituliza katika itidali
- kusujudu
- kujituliza katika Sijda
- kukaa kati ya Sijda mbili
- kujituliza katika kikao kati ya sijda mbili
- kusujudu mara ya pili
- kujituliza katika sijda ya pili
- kukaa Tahiyyatu
- kusoma Tahiyyatu
- kumswalia au kumtakia rehema na amani Mtume (s.a.w) na waislamu
- kutoa salaam
- kufuata utaratibu huu (1-17) kwa mfuatano
- Makundi manne ya nguzo za swala
- Nia.
- Nguzo za matamshi (visomo)
- Takbiira ya kuhirimia swala
- Kusoma Suratul-Fatihah
- Kusoma Tahiyyatu
- Kumswalia Mtume (s.a.w)
- Kutoa Salaam
- Nguzo za vitendo
- Ukiondoa nguzo ya ‘Nia’ na ‘kufuata utaratibu’ zilizobaki ni nguzo za vitendo.
.Kufuata utaratibu
- Ni yale mambo akiyafanya mwenye kuswali, hupandisha daraja ya swala yake
- Kuinua viganja vya mikono usawa wa mabega
- Kusoma dua baada ya Takbiira ya kuhirimia
- Kuanza kwa “Audhubillah” kabla ya kusoma Suratul-fatihah
- Kuitikia “Aamin” baada ya kumaliza kusoma Suratul-Fatihah
- Kusoma aya za Qur’an baada ya kusoma suratul-Fatihah rakaa mbili za mwanzo
- Kusoma Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali, sijda, n.k.
- Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili.
- Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume (s.a.w).
- Namna ya kutekeleza Nguzo na Sunnah za Swala hatua kwa hatua
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 100-110
- Sijda ya kawaida katika swala
- Sijdatut-Tilaawat (Sijda ya kisomo) – ni Sijda ya sunnah ailetayo msoji au msikilizaji wa Qur’an pale atakaposoma aya inayotaja sijda.
Aya za sijda ndani ya Qur’an ziko 15.
(7:206), (13:15), (16:50), (17:109), (19:58), (22:18), (22:77), (25:60), (27:26), (32:15), (38:24), (41:38), (53:62), (84:21) na (96:19).
- Sijdatus-Sah-wi (Sijda ya kusahau) – ni sijda anayoileta mtu kabla ya kutoa salaam ili kufidia kitendo cha sunnah alichokisahau katika swala.
- Mambo yanayobatilisha (yanayoharibu) Swala
- Kutoelekea Qibla bila dharura (udhuru) wowote kisheria.
- Kupatikana na hadathi kubwa (hedhi/nifasi), ndogo (kutengukwa udhu) au ya kati na kati (janaba).
- Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
- Kuvukwa na nguo ukawa uchi – mgongoni, kiunoni, kitovuni, n.k. (tahadhari kuvaa mashati mafupi, madogo kwa wanaume).
- Kusema au kutamka makusudi walau herufi moja isiyo na mahusiano na ibada ya swala.
- Kula au kunywa chochote hata kwa kusahau.
- Kufanya kitendo/jambo lisilohusiana na swala mfululizo mara tatu.
- Kuacha nguzo yeyote ya swala.
- Kuzidisha nguzo yeyote ya swala makusudi.
- Kumtangulia imamu au kumchelewa (ukiwa maamuma) kwa nguzo mbili za kimatendo mfululizo na makusudi.
- Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni uikate swala au usiikate.
- Kuwa na shaka kuwa umetimiza au haujatimiza sharti au nguzo yeyote ya swala.
- Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
- Kutoa salaam makusudi kabla ya kuisha swala.
- Kuswalishwa kwa asiyekuwa muislamu.
- Kukhalifu (kutofuata) utaratibu wa Nguzo za swala katika mpangilio wake.
- Kuleta dua ya kuomba kitu cha haramu au muhali.
- Kumshirikisha Allah (s.w) kwa kuleta dua au maombi.
- Khushui (Unyenyekevu) katika Swala
Ni jambo la tatu katika kusimamisha swala
Maana ya Khushui – Ni kujituliza kimwili na kifikra na kuzingatia yale mja anayotenda na kusema katika swala.
- Namna ya kupata Khushui katika Swala1.Kuutuliza mwili
- Utulivu wa mwili hupatikana kwa kutojipapasa papasa, kutochezesha viungo na kuangalia pale tu unaposujudia.
2.Kuzituliza fikra (moyo)
- Fikra hutulia kwa kurejesha na kubakisha mawazo yote ndani ya swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.
3.Kuwa na mazingatio
- Mazingatio hupatikana kwa kujua maana pamoja na kuwa makini na kile unachokisema au unachokitenda ndani ya swala.
- Namna ya kufikia Lengo la Swala
- Ni kutekeleza sharti zote za Swala kikamilifu kabla ya kuanza kuswali.
- Ni kutekeleza kikamilifu nguzo zote za swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.
Rejea Qur’an (29:45), (20:14), (7:205), (107:4-6).
Download App Yetu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download Now
Nyuma
Endelea
Je umeipenda post hii ?
Ndio Hapana Save post
Author:
Rajabu 
Tarehe:
1970-01-01 03:33:44
Topic:
Fiqh
Main:
Dini
File:
Download PDF
Views
2353
Post zinazofanana:
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.
Soma Zaidi...
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi
Soma Zaidi...
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga.
Soma Zaidi...