Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)


Download kitabu hiki hapa

Mambo yenye kufunguza Swaumu:
Huharibika funga kwa kuvunja nguzo ya funga pamoja na sharti zake. Haya yenye kubatilisha funga yamegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni:-

1.yenye kubatilisha funga na kulazimika kulipa nayo ni;-
A)kula na kunya kwa makusudi. Mtu aliyekula au kunywa kwa kusahau funga yake haita haribika. Amesema Mtume (s.a.w): mwenye kusahau na hali ya kuwa amefunga, na akala na kunywa na aendelee na funga yake kwani hakika Allah amemlisha. (Bukhari na Muslim). Mwenye kula au kunywa kwa makusudi atakujalipa funga hii.

B)Kujitapishwa kwa makusudi. Amesema Mtume (s.a.w): mwenye kutapika hana haja ya kulipa funga ila mwenye kujitapisha kwa makusudi na alipe funga.(Tirmidh)

C)Kupatwa na hedhi
D)Kupatwa na nifasi
E)Kujitoa manii kwa makusudi (punyeto)
F)Kukusudia kuvuja funga yaani kukusudia kuftari.
G)Kutoka kwenye uislamu.

2.yenye kubatilisha funga na kulazimika kulipa pamoja na kutoa kafara
Na hapa ni jambo moja tu nalo ni kufanya jimai. Amesimulia Abuu hurairah kuwa wakati tulipokuwa tumekaa na Mtume (s.a.w) ghafla akaja Mtu mmoja na akamwambia Mtume (s.a.w) ewe mtume nimeangamia Mtume akamuuliza una nini akajibu:nimefanya jimai na mke wangu na hali ya kuwa nimefunga. Mtume akamwambia je unae Mtumwa umuache huru, akasema sina, akamwambia:je unaweza kufunga kwa muda wa miezi miwili mfululizi? Akasema: siwezi. Akamwambia je unaweza kulisha masikini sitini? Akasema siwezi, basi pale Mtume akanyamaza. Akasema Abuu hurairah wakati tukiwa katika hali ile kukaletwa kwa mtume tende basi mtume akauliza yupo wapi aliyeuliza? Akasema nipo hapa, akamwambia chukuwa hizi tende ukatoe sadaka.…….” Hivyo kafara ya mwenye kufanya jimai ni kuacha huru mtumwa au kufunga miezi miwili mfululizo au kulisha masikini sitini. Na hukumu hii pia ni sawa na mwanamke.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1082

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Taratibu za kumiliki hisa na mali ya shirika

Katika Uislamu kuwa na hisa kwenye mali inaruhusiwa. Hapa utajifunza taratibu za kumiliki hisa.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Mambo yanayoharibu swala yaani yanayobatilisha swala.

Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe.

Soma Zaidi...
Namna ya kurithisgha hatuwa kwa hatuwa.

Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.

Soma Zaidi...
Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua

Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa.

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...