Mambo yenye kufunguza Swaumu:
Huharibika funga kwa kuvunja nguzo ya funga pamoja na sharti zake. Haya yenye kubatilisha funga yamegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni:-
1.yenye kubatilisha funga na kulazimika kulipa nayo ni;-
A)kula na kunya kwa makusudi. Mtu aliyekula au kunywa kwa kusahau funga yake haita haribika. Amesema Mtume (s.a.w): mwenye kusahau na hali ya kuwa amefunga, na akala na kunywa na aendelee na funga yake kwani hakika Allah amemlisha. (Bukhari na Muslim). Mwenye kula au kunywa kwa makusudi atakujalipa funga hii.
B)Kujitapishwa kwa makusudi. Amesema Mtume (s.a.w): mwenye kutapika hana haja ya kulipa funga ila mwenye kujitapisha kwa makusudi na alipe funga.(Tirmidh)
C)Kupatwa na hedhi
D)Kupatwa na nifasi
E)Kujitoa manii kwa makusudi (punyeto)
F)Kukusudia kuvuja funga yaani kukusudia kuftari.
G)Kutoka kwenye uislamu.
2.yenye kubatilisha funga na kulazimika kulipa pamoja na kutoa kafara
Na hapa ni jambo moja tu nalo ni kufanya jimai. Amesimulia Abuu hurairah kuwa wakati tulipokuwa tumekaa na Mtume (s.a.w) ghafla akaja Mtu mmoja na akamwambia Mtume (s.a.w) ewe mtume nimeangamia Mtume akamuuliza una nini akajibu:nimefanya jimai na mke wangu na hali ya kuwa nimefunga. Mtume akamwambia je unae Mtumwa umuache huru, akasema sina, akamwambia:je unaweza kufunga kwa muda wa miezi miwili mfululizi? Akasema: siwezi. Akamwambia je unaweza kulisha masikini sitini? Akasema siwezi, basi pale Mtume akanyamaza. Akasema Abuu hurairah wakati tukiwa katika hali ile kukaletwa kwa mtume tende basi mtume akauliza yupo wapi aliyeuliza? Akasema nipo hapa, akamwambia chukuwa hizi tende ukatoe sadaka.…….” Hivyo kafara ya mwenye kufanya jimai ni kuacha huru mtumwa au kufunga miezi miwili mfululizo au kulisha masikini sitini. Na hukumu hii pia ni sawa na mwanamke.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii itakufundishabkuhusu mirathi ya kiislamu, maana yake.
Soma Zaidi...KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.
Soma Zaidi...(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.
Soma Zaidi...Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu
Soma Zaidi...(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.
Soma Zaidi...عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُ?...
Soma Zaidi...