hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna

Nguzo za Swala



Utekelezaji wa nguzo za swala ni hatua ya pili katika harakati za kusimamisha Swala. Baada ya kutekeleza kwa ukamilifu sharti za swala, Muislamu huwa tayari kumkabili Mola wake na kuzungumza naye katika swala.Vipi tuzungumze na Mola wetu katika swala, tumeonyeshwa kinadharia na matendo na Mtume Muhammad (s.a.w) ambaye ametuusia: “Swalini kama mlivyoniona mimi nikiswali”. Tunafahamu Mtume (s.a.w) aliswali vipi kwa kurejea Hadith zifuatazo:



Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akianza swala kwa takbira na kusoma Qur-an - Alhamdullilaahi Rabil-alamiina (Suratul Fatiha). Alipoinama (kurukuu) hakuwa anaweka kichwa chake juu wala hakuwa anakiinamisha sana bali alikuwa akikiweka katikati ya hali hizo mbili, na alipoinuka kutoka kwenye rukuu hakuwa anakwenda


kwenye sijda mpaka asimame kwanza wima na alipoinua kichwa chake kutoka kwenye sijda, hakusujudu mpaka baada ya kukaa wima; na alikuwa akisoma tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, na (katika hiyo tahiyyatu) alikuwa anakaa kwa kuulaza mguu wa kushoto na kuusimamisha wima mguu wa kulia. Alikataza kukaa mkao wa shetani (kunyoosha miguu) na kunyoosha mikono kama mnyama, na alikuwa akifunga (akimaliza) Swala kwa Salaam”. (Muslim)



Abu Humid Sayid(r.a) aliwaambia Masw ahaba wa Mtume (s.a.w) alitaka kuwakumbusha jinsi Mtume wa Mwenyezi alivyokuwa akisw ali. Alisema (Abu Humaid) kwamba wakati alipokuwa akisoma takbira Mtume alikuwa akiweka mikono yake mkabala na mabega yake na alipokuw a akirukuu, aliweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kuupinda mgongo wake; wakati alipoinua kichwa (alipoinuka) alijinyoosha (alinyoosha shingo yake) wima mpaka kila kiungo kinarudia nafasi yake; wakati alipokwenda Sijda (aliposujudu) mikono yake ilikuwa kati na kati (haikuwa mbali sana wala haikuwa pamoja), na vidole vyake (ncha za vidole vyake) vya miguu vilielekea (alivielekeza) Ka ’aba, alipokaa baada ya rakaa mbili alikuwa akiukalia mguu wake wa kushoto na kusimamisha mguu wa kulia. Wakati alipokaa katika rakaa ya mwisho aliutanguliza (hakuukalia) mguu w a kushoto na kuusimamisha w a kulia, alikaa kwa makalio. (Bukhari).



Abu Hamaid Sayid aliwaambia Maswahaba kumi wa Mtume(s.a.w), kwamba yeye anajua vizuri zaidi jinsi Mtume (s.a.w) alivyokuwa akiswali. Alisema (Abu Hamid) kwamba: Wakati Mtume (s.a.w) aliposimama kuswali, aliinua mikono yake juu mpaka ilipokuwa mkabala na mabega yake. Halafu alisoma takbira na baadaye alisoma Qur-an. Halafu alisoma takbira na kuinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake.Halafu aliinama (alirukuu) akiweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kujiweka mwenyewe sawa sawa (bila ya kuinamisha kichwa wala kukiinua juu). Baadaye aliinua kichwa chake (aliinuka kutoka rukuu) na kusema: “Mwenyezi Mungu anamsikia (humsikia) yule anayemsifu ”. Halafu aliinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake akiwa wima sawa sawa na kusema:“Mwenyezi Mungu ni mkubwa ”. Baadaye alikw enda (chini alikw enda sijda) akiw eka mikono yake mbali na usawa wake na mwili na kupinda vidole vyake vya miguu. Aliinua kichwa chake na aliukunja mguu wake wa kushoto na kuukalia. Alikaa sawasawa (wima) mpaka kila kiungo cha mwili kimerudia mahali pake, na alikwenda tena sijda na kusema:“Mwenyezi Mungu ni mkubwa ”. Aliinuka (alijiinua) kutoka Sijda na kukalia mguu wake wa kushoto. Alikaa sawa sawa mpaka kila kiungo cha mwili kikarudia nafasi yake (mahali pake). Baadaye alisimama juu (wima) na kufanya yote kama alivyofanya


katika rakaa ya kwanza. Mw is ho wa rakaa hizi mbili alisimama na kusoma takbira.ya kwanza na aliinua mikono yake hadi ikawa mkabala na mabega yake kama alivyosoma takbira ya kufungulia swala na baadaye alifanya hivyo hivyo katika sehemu ya swala iliyobakia mpaka kufikia Sijda ambamo mlikuwa na (Taslimu). Aliondoa mguu wake wa kushoto (hakuukalia). Alikaa kwa makalio zaidi upande wa kushoto (alikalia mfupa wa kalio la upande wa kushoto) baadaye alitoa Salaam (Taslim). Maswahaba wote `walikubali kuwa Abu Hamid amesema ukweli. (Abu Daud).



Hadithi hizi zinatufahamisha kuwa swala ya Mtume(s.a.w) ambaye ametuamrisha tumuigize ina vipengele vilivyogawanyika katika mafungu makubwa mawili. Nguzo za Swala na Sunnah za Swala.



Nguzo za Swala



Nguzo za swala ni vile vipengele vya swala ambavyo lazima mtu avitekeleze ndio swala yake iweze kukamilika. Nguzo moja tu ikikosekana swala haisihi (haikamiliki). Hivyo ili mwenye kuswali awe na matarajio ya kupata matunda ya Swala hana budi kutekeleza nguzo zake zote kwa ukamilifu. Zifuatazo ni nguzo za Swala:



1. Nia - dhamira moyoni.
2. Takbira ya kuhirimia (au Takbira ya kufungulia Swala).
3. Kusoma suratul-Fatiha.
4.Kurukuu.
5.Kujituliza katika rukuu.
6.Kuitidali (kusimama kutoka katika rukuu).
7.Kujituliza katika itidali.
8.Kusujudu.
9.Kujituliza katika sijda.
10.Kukaa kati ya sijda mbili.
11.Kujituliza katika kikao cha kati ya sijda mbili.
12Kusujudu mara ya pili.
13.Kujituliza katika sijda ya pili.
14.Kukaa Tahiyyatu.
15.Kusoma Tahiyyatu.
16.Kumswalia na kumtakia rehema Mtume (s.a.w) na Waislamu.
17.Kutoa Salaam.
18.Kuswali kwa kufuata utaratibu huu (1 - 17).



hizi za swala tunaweza kuzigawanya kwenye makundi
(a)Nia.
(b)Nguzo za matamshi (visomo)
(c)Nguzo za vitendo.
(d)Kufuata utaratibu.



Katika nguzo 18, nguzo za matamshi ni hizi tano zifuatazo:
(i)Takbira ya kuhirimia swala.
(ii)Ku soma suratul-Fatiha (Al-hamdu).
(iii)Kusoma Tahiyyatu.
(iv)Kumswalia Mtume.
(v)Kutoa Salaam.



Nguzo zote zilizobakia, ukiacha nia na kufuata utaratibu ni nguzo za vitendo.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 461


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

Nadharia ya uchumi kiislamu
1. Soma Zaidi...

Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkuchunga nyakatibza swala tano. Soma Zaidi...

TAKBIRA YA KWANZA, DUA BAADA YA TAKBIRA YA KUHIRIMIA SWALA NA KUSOMA ALHAMDU (SURAT AL-FATIHA KWENYE SWALA
2. Soma Zaidi...

Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE
NGUZO ZA UISLAMU. Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa mayatima
Soma Zaidi...

MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA
*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko. Soma Zaidi...

Wanaowajibika kuhijji
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali swala vitani
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani. Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...