image

Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume

Imepokelewa toka kwa Humraan mwachwa huru wa ‘Uthmaan kwamba alimwona ‘Uthmaan bin ‘Affaan akiagiza chombo, kisha akamimina (maji) juu ya viganja vyake mara tatu na kuviosha.

 

Kisha akauingiza mkono wake wa kuume kwenye chombo, akasukutua na kupaliza  maji puani. Kisha akaosha uso wake mara tatu, na mikono yake hadi kwenye viwiko mara tatu.

 

Halafu akapukusa (akapangusa/ akafuta) kichwa chake, kisha akaosha miguu yake mara tatu hadi kwenye vifundo, kisha akasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

(( من توضأ نحو وضوئي هذا، ثم صلى ركعتين لا يحدث فيهما نفسه، غفر له ما تقدم من ذنبه))

((Mwenye kutawadha mfano wa wudhuu wangu huu, kisha akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, hughufiriwa (atafutiwa) madhambi yake yaliyopita)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (158) na Muslim (226)].

 

 

Na kutokana na Hadiyth hii na nyinginezo zitakazokuja kuzungumziwa kwa ufafanuzi, tunaweza kuiweka sifa ya wudhuu katika haya yafuatayo:

 

 

1-Atanuwia wudhuu kwa ajili ya kuondosha hadathi.

 

2-Atalidhukuru Jina la Allaah Mtukufu (yaani kusema Bismillah).

 

3-Ataviosha viganja vyake mara tatu.

 

4-Atateka maji kwa mkono wake wa kuume, kisha atayaweka mdomoni na puani kwa teko moja, atasukutua na kupaliza.

 

5-Atapenga kwa kutumia mkono wake wa kushoto. Atafanya hivi mara tatu.

 

6-Ataosha uso wake wote mara tatu pamoja na kupachanyisha ndevu.

 

7-Ataiosha mikono yake miwili – wa kulia kisha wa kushoto – mpaka juu ya viwiko viwili pamoja na kupachanyisha vidole vya mikono miwili.

 

8-Atapukusa (pangusa/futa) kichwa chake chote kwenda nyuma na mbele mara moja.

 

9-Atapukusa (pangusa/futa) masikio yake mawili nje na ndani.

 

10-Ataosha miguu yake miwili pamoja na vifundo vyake viwili - wa kulia kisha wa kushoto - pamoja na kupachanyisha vidole vya miguu miwili.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 769


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mifano na namna ya kurithisha
Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi. Soma Zaidi...

Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...

Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu
Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...

Namna ya Safari ya Hija inavyoanza
Soma Zaidi...

Mali zinazojuzu kutolewa zaka, nisaab yake na viwango vyake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni yapi masharti ya Udhu na kujitwaharisha
Soma Zaidi...

Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea
Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya vitani
Soma Zaidi...

Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake
Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada. Soma Zaidi...

Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hili ndio lengo la kufunga.
Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga. Soma Zaidi...