Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume

Imepokelewa toka kwa Humraan mwachwa huru wa ‘Uthmaan kwamba alimwona ‘Uthmaan bin ‘Affaan akiagiza chombo, kisha akamimina (maji) juu ya viganja vyake mara tatu na kuviosha.

 

Kisha akauingiza mkono wake wa kuume kwenye chombo, akasukutua na kupaliza  maji puani. Kisha akaosha uso wake mara tatu, na mikono yake hadi kwenye viwiko mara tatu.

 

Halafu akapukusa (akapangusa/ akafuta) kichwa chake, kisha akaosha miguu yake mara tatu hadi kwenye vifundo, kisha akasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

(( من توضأ نحو وضوئي هذا، ثم صلى ركعتين لا يحدث فيهما نفسه، غفر له ما تقدم من ذنبه))

((Mwenye kutawadha mfano wa wudhuu wangu huu, kisha akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, hughufiriwa (atafutiwa) madhambi yake yaliyopita)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (158) na Muslim (226)].

 

 

Na kutokana na Hadiyth hii na nyinginezo zitakazokuja kuzungumziwa kwa ufafanuzi, tunaweza kuiweka sifa ya wudhuu katika haya yafuatayo:

 

 

1-Atanuwia wudhuu kwa ajili ya kuondosha hadathi.

 

2-Atalidhukuru Jina la Allaah Mtukufu (yaani kusema Bismillah).

 

3-Ataviosha viganja vyake mara tatu.

 

4-Atateka maji kwa mkono wake wa kuume, kisha atayaweka mdomoni na puani kwa teko moja, atasukutua na kupaliza.

 

5-Atapenga kwa kutumia mkono wake wa kushoto. Atafanya hivi mara tatu.

 

6-Ataosha uso wake wote mara tatu pamoja na kupachanyisha ndevu.

 

7-Ataiosha mikono yake miwili – wa kulia kisha wa kushoto – mpaka juu ya viwiko viwili pamoja na kupachanyisha vidole vya mikono miwili.

 

8-Atapukusa (pangusa/futa) kichwa chake chote kwenda nyuma na mbele mara moja.

 

9-Atapukusa (pangusa/futa) masikio yake mawili nje na ndani.

 

10-Ataosha miguu yake miwili pamoja na vifundo vyake viwili - wa kulia kisha wa kushoto - pamoja na kupachanyisha vidole vya miguu miwili.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1167

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Sera ya uchumi katika uislamu

Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.

Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii

Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?

Soma Zaidi...
Mambo ambayo hayafunguzi funga

Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya.

Soma Zaidi...
Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea

Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina au migawanyo mbalimbali ya haki katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...