Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.

Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu.

1. Mimba kutishia kutoka au kuharibika kabla ya kujifungua.

Kuna wakati mwingine Kuna tatizo la mimba kuharibika au kutishia kutoka ni lazima damu inatoka kwa sababu Kuna baadhi ya maambukizi ambayo yanakuwepo kwenye via vya uzazi ambayo usababisha mimba kuharibika au kutishia kutoka, na pia damu utoka kwa sababu baadhi ya mishipa ya damu ambayo inakuwa imeshikilia mtoto uachia na kusababisha damu kutoka , ila mimba inayotishia kutoka mama akiwahi hospital upewa matibabu mapema na mimba urudia kwenye hali yake ya kawaida.

 

2. Pia damu  utoka wakati wa ujauzito kwa sababu kondo la nyuma linapotaka kujishikiza kwenye mji wa uzazi usababisha kupelekea damu kutoka wakati wa ujauzito ila kwa kawaida damu hiyo huwa ni ndogo na utokea kwa mda mfupi tu na kutoweka, hali hii uwapata hasa hasa akina Mama kwenye mimba za kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa prime gravida, kwa hiyo hii ni hali ya kawaida kabisa na Haina madhara yoyote kwa mama , kwa sababu hili kondo lenyewe ndilo baadae uja kusaidia mtoto kwa chakula na vitu vingine vingi wakati mtoto akiwa tumboni.

 

3. Mimba kutungwa nje ya mfuko wa uzazi.

Kuna wakati mwingine mimba utungwa nje ya mfuko wa uzazi mbali na sehemu yake ambapo inapaswa kutungwa, kwa hiyo mimba inaweza kutungwa kwenye sehemu mbalimbali za via vya uzazi ila kwa kiasi kikubwa utungwa kwenye mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube ni mara chache sana mimba kutungwa kwenye ovaries, kwa hiyo mimba haipaswi kabisa kutungwa hapo kwa hiyo mimba inaweza kufika mpaka kwenye wiki ya kumi na mbili, kwa hiyo kitendo cha mimba kutungwa kwenye follapian tube usababisha damu kutoka na ni vizuri kabisa kumpeleka mama hospital mapema ili kuweza kumsaidia kwa sababu hii huwa ni hatari.

 

4. Wakati mwingine damu utoka wakati wa ujauzito ni kwa sababu ambazo hazijulikani kwa sababu Kuna akina Mama wengi ambao upatwa na tatizo hili na chanzo utafutwa ila hakijulikanagi kwa hiyo ni vizuri kuwa kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya na kuweza kuhakikisha kuwa mtoto anazaliwa Salama na Mama anakuwa salama 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2745

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili za kujifungua hatua kwa hatua

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.

posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya Matiti kwa Mama mjamzito

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Je mjamzito Uchungu ukikata inakuwaje

Hutokea uchungu wa kujifunguwa ukakati. Unadhani ni kitugani kinatokea.

Soma Zaidi...
Sababu za kutoka mimba yenye miezi Saba na nane

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha.

Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v

Soma Zaidi...
Uchunguzi wa Nimonia kwa mtoto na Tiba

Posti hii inahusu namna unavyoweza kumtambua mtoto mwenye Ugonjwa wa Nimonia na tiba anayopaswa kupata mtoto mwenye Nimonia

Soma Zaidi...
Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo

Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini

Soma Zaidi...
Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza

Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.

Soma Zaidi...