Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.
1. Mimba kutishia kutoka au kuharibika kabla ya kujifungua.
Kuna wakati mwingine Kuna tatizo la mimba kuharibika au kutishia kutoka ni lazima damu inatoka kwa sababu Kuna baadhi ya maambukizi ambayo yanakuwepo kwenye via vya uzazi ambayo usababisha mimba kuharibika au kutishia kutoka, na pia damu utoka kwa sababu baadhi ya mishipa ya damu ambayo inakuwa imeshikilia mtoto uachia na kusababisha damu kutoka , ila mimba inayotishia kutoka mama akiwahi hospital upewa matibabu mapema na mimba urudia kwenye hali yake ya kawaida.
2. Pia damu utoka wakati wa ujauzito kwa sababu kondo la nyuma linapotaka kujishikiza kwenye mji wa uzazi usababisha kupelekea damu kutoka wakati wa ujauzito ila kwa kawaida damu hiyo huwa ni ndogo na utokea kwa mda mfupi tu na kutoweka, hali hii uwapata hasa hasa akina Mama kwenye mimba za kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa prime gravida, kwa hiyo hii ni hali ya kawaida kabisa na Haina madhara yoyote kwa mama , kwa sababu hili kondo lenyewe ndilo baadae uja kusaidia mtoto kwa chakula na vitu vingine vingi wakati mtoto akiwa tumboni.
3. Mimba kutungwa nje ya mfuko wa uzazi.
Kuna wakati mwingine mimba utungwa nje ya mfuko wa uzazi mbali na sehemu yake ambapo inapaswa kutungwa, kwa hiyo mimba inaweza kutungwa kwenye sehemu mbalimbali za via vya uzazi ila kwa kiasi kikubwa utungwa kwenye mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube ni mara chache sana mimba kutungwa kwenye ovaries, kwa hiyo mimba haipaswi kabisa kutungwa hapo kwa hiyo mimba inaweza kufika mpaka kwenye wiki ya kumi na mbili, kwa hiyo kitendo cha mimba kutungwa kwenye follapian tube usababisha damu kutoka na ni vizuri kabisa kumpeleka mama hospital mapema ili kuweza kumsaidia kwa sababu hii huwa ni hatari.
4. Wakati mwingine damu utoka wakati wa ujauzito ni kwa sababu ambazo hazijulikani kwa sababu Kuna akina Mama wengi ambao upatwa na tatizo hili na chanzo utafutwa ila hakijulikanagi kwa hiyo ni vizuri kuwa kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya na kuweza kuhakikisha kuwa mtoto anazaliwa Salama na Mama anakuwa salama
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazosababisha kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Utajifunza sababu za maumivu ya uume na uke wakati wa tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa na matibabu yake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza siku nzuri kushoriki tendo la ndoa kupata ujauzito, dalili za siku hiyo na kuitafuta kwa mahesabu
Soma Zaidi...Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.
Soma Zaidi...Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi vipimo muhimu wakati wa ujauzito ni vipimo ambavyo vinapaswa kupimwa na Mama ili kuangalia mambo mbalimbali katika damu au sehemu yoyote, pia vipimo hivi umsaidia sana Mama kujua afya yake.
Soma Zaidi...Je umeshawahi kujiukiza kuwa, dawa ya P2 ni kweli inaweza kuzuia mimba, ukifanya mapenzi siku hatari?
Soma Zaidi...