image

Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.

Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu.

1. Mimba kutishia kutoka au kuharibika kabla ya kujifungua.

Kuna wakati mwingine Kuna tatizo la mimba kuharibika au kutishia kutoka ni lazima damu inatoka kwa sababu Kuna baadhi ya maambukizi ambayo yanakuwepo kwenye via vya uzazi ambayo usababisha mimba kuharibika au kutishia kutoka, na pia damu utoka kwa sababu baadhi ya mishipa ya damu ambayo inakuwa imeshikilia mtoto uachia na kusababisha damu kutoka , ila mimba inayotishia kutoka mama akiwahi hospital upewa matibabu mapema na mimba urudia kwenye hali yake ya kawaida.

 

2. Pia damu  utoka wakati wa ujauzito kwa sababu kondo la nyuma linapotaka kujishikiza kwenye mji wa uzazi usababisha kupelekea damu kutoka wakati wa ujauzito ila kwa kawaida damu hiyo huwa ni ndogo na utokea kwa mda mfupi tu na kutoweka, hali hii uwapata hasa hasa akina Mama kwenye mimba za kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa prime gravida, kwa hiyo hii ni hali ya kawaida kabisa na Haina madhara yoyote kwa mama , kwa sababu hili kondo lenyewe ndilo baadae uja kusaidia mtoto kwa chakula na vitu vingine vingi wakati mtoto akiwa tumboni.

 

3. Mimba kutungwa nje ya mfuko wa uzazi.

Kuna wakati mwingine mimba utungwa nje ya mfuko wa uzazi mbali na sehemu yake ambapo inapaswa kutungwa, kwa hiyo mimba inaweza kutungwa kwenye sehemu mbalimbali za via vya uzazi ila kwa kiasi kikubwa utungwa kwenye mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube ni mara chache sana mimba kutungwa kwenye ovaries, kwa hiyo mimba haipaswi kabisa kutungwa hapo kwa hiyo mimba inaweza kufika mpaka kwenye wiki ya kumi na mbili, kwa hiyo kitendo cha mimba kutungwa kwenye follapian tube usababisha damu kutoka na ni vizuri kabisa kumpeleka mama hospital mapema ili kuweza kumsaidia kwa sababu hii huwa ni hatari.

 

4. Wakati mwingine damu utoka wakati wa ujauzito ni kwa sababu ambazo hazijulikani kwa sababu Kuna akina Mama wengi ambao upatwa na tatizo hili na chanzo utafutwa ila hakijulikanagi kwa hiyo ni vizuri kuwa kwenye uangalizi wa wataalamu wa afya na kuweza kuhakikisha kuwa mtoto anazaliwa Salama na Mama anakuwa salama 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1706


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Faida za uzazi wa mpango kwa jamii
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii. Soma Zaidi...

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa. Soma Zaidi...

Fahamu sifa za Ute wa siku za kupata mimba yaani ovulation day
Posti hii inahusu zaidi sifa za Ute wa ovulation, ni Ute ambao utokea siku za ovulation yaani siku ambazo ni tayari kwa kubeba mimba, yaani siku za upevishaji wa yai. Soma Zaidi...

Maumivu ya Uke na Uume baada ya tendo la ndoa na wakati wa tendo la ndoa
Utajifunza sababu za maumivu ya uume na uke wakati wa tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa na matibabu yake. Soma Zaidi...

Upungufu wa homoni ya cortisol
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni hii ya cortisol,hii ni homoni ambayo utokana na tezi glang(adrenal gland) kufanya kazi kupitiliza hali ambayo mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo wa mda mrefu, yaani wale watu ambao mda mwingi huwa wenye Soma Zaidi...

Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza Soma Zaidi...

Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?
Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito? Soma Zaidi...

Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa
Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye Soma Zaidi...

Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua. Soma Zaidi...

Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.
posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot Soma Zaidi...

Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone. Soma Zaidi...

Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba. Soma Zaidi...