Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.
Njia za kupunguza tatizo la kuvimba kwa tezi dume.
1.Kwanza kabisa tunajua kubwa Ugonjwa huu umeweza kusambaa kwa kiasi kikubwa na kusababisha madhara kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili
2. Tunapaswa kula vizuri.
Kula vizuri kwa maana ya kula mchanganyiko wa vyakula sio kula chakula kimoja hata kama una uwezo wa kawaida unaweza leo kula viazi kesho ugali, siku nyingine wali na pia kutumia mboga za majani na matunda hata sio lazima kuwa na mafuta ili utumie mboga za majani au kama una uwezo kula chakula kadri ya uwezo wako maana katika vyakula tunaweza kutibu mambo mengi bila kujua.
3. Jaribu kupunguza sumu mwilini.
Kwa wakati huu tunakula sana vyakula vyenye sumu kama vile mafuta mengi kwenye chakula, vyakula vya Makopo, chips, baga na vyakula vingine vya namna hiyo na pia kuna unywaji wa pombe kali kupita kiasi na pia kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu , mambo hayo yote uongeza sumu mwilini kwa hiyo tunapaswa kuepuka vyakula hivyo kuvila kwa muda mrefu badala yake punnguza matumizi ya mafuta na kunywa sana maziwa.
4. Daima epukana na ngono zembe.
Kwa wakati huu kuna mlipuko wa magonjwa ya zinaa kila wakati kama vile kaswende, kisonono na mengine mengi kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana au kutibu maambukizi ili kuweza na kuendelea kuwepo kwa kuvimba kwa tezi dume.
5. Pia wanaume wanapaswa kufanya mazoezi.
Kwa kufanya mazoezi tunaweza kuna vitu vingi tunapata kwa sababu pale mtu akitoa jasho uchafu mwingi utoka na mwili huwa huru na kutokana na mazoezi tunaweza kuepusha Magonjwa mengi tusiyotafahamu.
6. Kuepuka Matumizi ya pombe kali na sigara.
Kwa matumizi ya pombe kali na sigara usababisha viungo mbalimbali vya mwili kulegea na kutofanya kazi vizuri hali hii inaweza kusababisha maambukizi sehemu mbalimbali za mwili na mwili kuwa dhaifu hatimaye Magonjwa mengi yanaweza kutokea hata kuvimba tezi dume.
7. Kuepuka na msongo wa mawazo.
Siku hizi kuna tatizo hili la kuwa na msingi wa mawazo kwa walio wengi hali ambayo uwafanya eatu kubwa na matatizo mengi ya kiafya. Kama kuna shida yoyote shirikisha rafiki, angalia mpira, au kitu chochote unachokipenda ili mradi kupunguza mawazo.
8.Katika maisha yetu tuwe na tabia ya kuchukua vipimo kwa ajili ya kuangalia afya zetu na tabia ya kuwahi hospitali unapohisi kubwa kuna kitu ambacho hakipo sawa kwa sababu, Ugonjwa wowote kama hata hauna tiba ukiwahi hospitalini madhara yanakuwa madogo kuliko pale ukienda umechelewa,
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.
Soma Zaidi...Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...Ikiwa mtoto wako ana kasoro ya moyo wa kuzaliwa, ina maana kwamba mtoto wako alizaliwa na tatizo katika muundo wa moyo wake. Baadhi ya kasoro za moyo za kuzaliwa kwa watoto ni rahisi na hazihitaji matibabu, kama vile tundu dogo kati ya chemba za moyo amb
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa harufu mbaya kwenye uke ukizingatia usafi huwa unafanyika mara kwa mara ila harufu bado inaendelea kuwa mbaya kwa hiyo tutaona sababu hapo chini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika.
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata mimba na dalili za siku hizo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji.
Soma Zaidi...Chuchu kubadilika range ni mojavkatika mabadiliko ambayo huwapa shoka wengi katika wasichana. Lucinda nikwambie tu kuwa katika hali ya kawaida hilo sio tatizo kiafya.
Soma Zaidi...