Njia za kupunguza tatizo la kutanuka kwa tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.
Njia za kupunguza tatizo la kuvimba kwa tezi dume.
1.Kwanza kabisa tunajua kubwa Ugonjwa huu umeweza kusambaa kwa kiasi kikubwa na kusababisha madhara kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili
2. Tunapaswa kula vizuri.
Kula vizuri kwa maana ya kula mchanganyiko wa vyakula sio kula chakula kimoja hata kama una uwezo wa kawaida unaweza leo kula viazi kesho ugali, siku nyingine wali na pia kutumia mboga za majani na matunda hata sio lazima kuwa na mafuta ili utumie mboga za majani au kama una uwezo kula chakula kadri ya uwezo wako maana katika vyakula tunaweza kutibu mambo mengi bila kujua.
3. Jaribu kupunguza sumu mwilini.
Kwa wakati huu tunakula sana vyakula vyenye sumu kama vile mafuta mengi kwenye chakula, vyakula vya Makopo, chips, baga na vyakula vingine vya namna hiyo na pia kuna unywaji wa pombe kali kupita kiasi na pia kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu , mambo hayo yote uongeza sumu mwilini kwa hiyo tunapaswa kuepuka vyakula hivyo kuvila kwa muda mrefu badala yake punnguza matumizi ya mafuta na kunywa sana maziwa.
4. Daima epukana na ngono zembe.
Kwa wakati huu kuna mlipuko wa magonjwa ya zinaa kila wakati kama vile kaswende, kisonono na mengine mengi kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana au kutibu maambukizi ili kuweza na kuendelea kuwepo kwa kuvimba kwa tezi dume.
5. Pia wanaume wanapaswa kufanya mazoezi.
Kwa kufanya mazoezi tunaweza kuna vitu vingi tunapata kwa sababu pale mtu akitoa jasho uchafu mwingi utoka na mwili huwa huru na kutokana na mazoezi tunaweza kuepusha Magonjwa mengi tusiyotafahamu.
6. Kuepuka Matumizi ya pombe kali na sigara.
Kwa matumizi ya pombe kali na sigara usababisha viungo mbalimbali vya mwili kulegea na kutofanya kazi vizuri hali hii inaweza kusababisha maambukizi sehemu mbalimbali za mwili na mwili kuwa dhaifu hatimaye Magonjwa mengi yanaweza kutokea hata kuvimba tezi dume.
7. Kuepuka na msongo wa mawazo.
Siku hizi kuna tatizo hili la kuwa na msingi wa mawazo kwa walio wengi hali ambayo uwafanya eatu kubwa na matatizo mengi ya kiafya. Kama kuna shida yoyote shirikisha rafiki, angalia mpira, au kitu chochote unachokipenda ili mradi kupunguza mawazo.
8.Katika maisha yetu tuwe na tabia ya kuchukua vipimo kwa ajili ya kuangalia afya zetu na tabia ya kuwahi hospitali unapohisi kubwa kuna kitu ambacho hakipo sawa kwa sababu, Ugonjwa wowote kama hata hauna tiba ukiwahi hospitalini madhara yanakuwa madogo kuliko pale ukienda umechelewa,
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi
Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.
Soma Zaidi...Madhara ya vidonge vya P2
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutumia mara kwa mara vidonge vya P2,
Soma Zaidi...Ujue Ute kwenye uke
Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.
Soma Zaidi...Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.
Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.
Soma Zaidi...Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia
Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali?
Soma Zaidi...Dalili za upungufu wa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Soma Zaidi...