Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.
Njia za kupunguza tatizo la kuvimba kwa tezi dume.
1.Kwanza kabisa tunajua kubwa Ugonjwa huu umeweza kusambaa kwa kiasi kikubwa na kusababisha madhara kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili
2. Tunapaswa kula vizuri.
Kula vizuri kwa maana ya kula mchanganyiko wa vyakula sio kula chakula kimoja hata kama una uwezo wa kawaida unaweza leo kula viazi kesho ugali, siku nyingine wali na pia kutumia mboga za majani na matunda hata sio lazima kuwa na mafuta ili utumie mboga za majani au kama una uwezo kula chakula kadri ya uwezo wako maana katika vyakula tunaweza kutibu mambo mengi bila kujua.
3. Jaribu kupunguza sumu mwilini.
Kwa wakati huu tunakula sana vyakula vyenye sumu kama vile mafuta mengi kwenye chakula, vyakula vya Makopo, chips, baga na vyakula vingine vya namna hiyo na pia kuna unywaji wa pombe kali kupita kiasi na pia kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu , mambo hayo yote uongeza sumu mwilini kwa hiyo tunapaswa kuepuka vyakula hivyo kuvila kwa muda mrefu badala yake punnguza matumizi ya mafuta na kunywa sana maziwa.
4. Daima epukana na ngono zembe.
Kwa wakati huu kuna mlipuko wa magonjwa ya zinaa kila wakati kama vile kaswende, kisonono na mengine mengi kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana au kutibu maambukizi ili kuweza na kuendelea kuwepo kwa kuvimba kwa tezi dume.
5. Pia wanaume wanapaswa kufanya mazoezi.
Kwa kufanya mazoezi tunaweza kuna vitu vingi tunapata kwa sababu pale mtu akitoa jasho uchafu mwingi utoka na mwili huwa huru na kutokana na mazoezi tunaweza kuepusha Magonjwa mengi tusiyotafahamu.
6. Kuepuka Matumizi ya pombe kali na sigara.
Kwa matumizi ya pombe kali na sigara usababisha viungo mbalimbali vya mwili kulegea na kutofanya kazi vizuri hali hii inaweza kusababisha maambukizi sehemu mbalimbali za mwili na mwili kuwa dhaifu hatimaye Magonjwa mengi yanaweza kutokea hata kuvimba tezi dume.
7. Kuepuka na msongo wa mawazo.
Siku hizi kuna tatizo hili la kuwa na msingi wa mawazo kwa walio wengi hali ambayo uwafanya eatu kubwa na matatizo mengi ya kiafya. Kama kuna shida yoyote shirikisha rafiki, angalia mpira, au kitu chochote unachokipenda ili mradi kupunguza mawazo.
8.Katika maisha yetu tuwe na tabia ya kuchukua vipimo kwa ajili ya kuangalia afya zetu na tabia ya kuwahi hospitali unapohisi kubwa kuna kitu ambacho hakipo sawa kwa sababu, Ugonjwa wowote kama hata hauna tiba ukiwahi hospitalini madhara yanakuwa madogo kuliko pale ukienda umechelewa,
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi tofauti mbalimbali za uke, kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kuna tofauti mbalimbali za ute kutegemea na hali iliyopo.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza siku nzuri kushoriki tendo la ndoa kupata ujauzito, dalili za siku hiyo na kuitafuta kwa mahesabu
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na hatua za kujikinga na Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na kwenye mirija ya uzazi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kupasuka kwa mfuko wa uzazi hasa mama anapokalibia kujifungua.
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kukuletea orodha ya vyakla vinavyoaminika kuongeza nguvu za kiume.
Soma Zaidi...