Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.
1. Kwanza kabisa Mama anayepasuka mfuko wa uzazi mara nyingi anakuwa kwenye uchungu, ila mfuko wa uzazi unapopasuka tu na uchungu unapungua kabisa badala ya kuendelea hiyo inakuwa ni mojawapo ya Dalili ya kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
2. Pia Mama anakuwa na maumivu ya kupita kiasi , hasa hasa ukigusa kwenye tumbo la Mama ,yeye anakuwa na maumivu na analalamika sana kuhusu tumbo kwa hiyo hii ni Dalili mojawapo ya Mama mwenye tatizo la kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
3. Pia na msukumo wa damu unapungua na kuipima unakuta uko chini kabisa na pia mapigo ya mtoto yanayopungua au kwa upande mwingine kama mtoto amashafariki yanakuwa hayapo kabisa.
4. Pia kwa upande wa mama na mapigo ya moyo yanapungua yaani sauti inasikikia kwa shida sana , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa mama kama yuko kwenye vituo vya afya apelekwe kwenye hospitali kubwa kwa uangalizi zaidi.
5. Pia na Mama anaay kutokwa na damu kwenye sehemu za siri kwa kawaida damu hiyo utegemea inaweza kuwa nyingi au ya kawaida.
6. Pia na mtoto ukishika kwenye tumbo ni rahisi kuhisi kwa mikono na unapokuwa unapapasa tumbo la Mama Maumivu yanakuwa ni makali mno na mama anakuwa analalamika sana.
7. Kwa hiyo kwa wauguzi na wataalam wa afya baada ya kuona hayo yote ni vizuri kabisa kumsaidia Mama ili asije kupoteza maisha kwa sababu hii ni Dalili mojawapo ya hatari kwa Mama wajawazito kwa hiyo ni vizuri kabisa kugundua mapema kabisa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube, ni sababu ambazo ufanya mirija ya follapian tube kuziba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Soma Zaidi...Miongoni mwa dalili zamwanzo za ujauzito ni maumivu ya tumbo ama kupatwa na damu kidogo. Mabadiliko ya ute ute sehemu za siri ni katika baadhi ya dalili. Endelea na makala hii utajifunza zaidi.
Soma Zaidi...Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...