Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.
Dalili za mama aliyepasuka mfuko wa uzazi.
1. Kwanza kabisa Mama anayepasuka mfuko wa uzazi mara nyingi anakuwa kwenye uchungu, ila mfuko wa uzazi unapopasuka tu na uchungu unapungua kabisa badala ya kuendelea hiyo inakuwa ni mojawapo ya Dalili ya kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
2. Pia Mama anakuwa na maumivu ya kupita kiasi , hasa hasa ukigusa kwenye tumbo la Mama ,yeye anakuwa na maumivu na analalamika sana kuhusu tumbo kwa hiyo hii ni Dalili mojawapo ya Mama mwenye tatizo la kupasuka kwa mfuko wa uzazi.
3. Pia na msukumo wa damu unapungua na kuipima unakuta uko chini kabisa na pia mapigo ya mtoto yanayopungua au kwa upande mwingine kama mtoto amashafariki yanakuwa hayapo kabisa.
4. Pia kwa upande wa mama na mapigo ya moyo yanapungua yaani sauti inasikikia kwa shida sana , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa mama kama yuko kwenye vituo vya afya apelekwe kwenye hospitali kubwa kwa uangalizi zaidi.
5. Pia na Mama anaay kutokwa na damu kwenye sehemu za siri kwa kawaida damu hiyo utegemea inaweza kuwa nyingi au ya kawaida.
6. Pia na mtoto ukishika kwenye tumbo ni rahisi kuhisi kwa mikono na unapokuwa unapapasa tumbo la Mama Maumivu yanakuwa ni makali mno na mama anakuwa analalamika sana.
7. Kwa hiyo kwa wauguzi na wataalam wa afya baada ya kuona hayo yote ni vizuri kabisa kumsaidia Mama ili asije kupoteza maisha kwa sababu hii ni Dalili mojawapo ya hatari kwa Mama wajawazito kwa hiyo ni vizuri kabisa kugundua mapema kabisa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.
Soma Zaidi...Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako.
Soma Zaidi...Malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inahusu malengo ya kuwahudumia watoto chini ya miaka mitano, huduma hii ilianzishwa na WHO na UNICEF mwaka 1990 ili kuweza kuzuia Magonjwa na kuwapatia watoto lishe pamoja na hayo walikuwa na malengo yafuatayo.
Soma Zaidi...Mambo muhimu kuhusu mbegu za kiume
Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa s
Soma Zaidi...Kiwango cha juu cha Androgen
Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.
Soma Zaidi...