picha

Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.

Dalili za mama aliyepasuka mfuko wa uzazi.

1. Kwanza kabisa Mama anayepasuka mfuko wa uzazi mara nyingi anakuwa kwenye uchungu, ila mfuko wa uzazi unapopasuka tu na uchungu unapungua kabisa badala ya kuendelea hiyo inakuwa ni mojawapo ya Dalili ya kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

 

2. Pia Mama anakuwa na maumivu ya kupita kiasi , hasa hasa ukigusa kwenye tumbo la Mama ,yeye anakuwa na maumivu na analalamika sana kuhusu tumbo kwa hiyo hii ni Dalili mojawapo ya Mama mwenye tatizo la kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

 

3. Pia na msukumo wa damu unapungua na kuipima unakuta uko chini kabisa na pia mapigo ya mtoto yanayopungua au kwa upande mwingine kama mtoto amashafariki yanakuwa hayapo kabisa.

 

4. Pia kwa upande wa mama na mapigo ya moyo yanapungua yaani sauti inasikikia kwa shida sana , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa mama kama yuko kwenye vituo vya afya apelekwe kwenye hospitali kubwa kwa uangalizi zaidi.

 

5. Pia na Mama anaay kutokwa na damu kwenye sehemu za siri kwa kawaida damu hiyo utegemea inaweza kuwa nyingi au ya kawaida.

 

6. Pia  na  mtoto ukishika kwenye tumbo ni rahisi kuhisi kwa mikono na unapokuwa unapapasa tumbo la Mama Maumivu yanakuwa ni makali mno na mama anakuwa analalamika sana.

 

7. Kwa hiyo kwa wauguzi na wataalam wa afya baada ya kuona hayo yote ni vizuri kabisa  kumsaidia Mama ili asije kupoteza maisha kwa sababu hii ni Dalili mojawapo ya hatari kwa Mama wajawazito kwa hiyo ni vizuri kabisa kugundua mapema kabisa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 4519

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba

Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi?

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa

Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba

Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.

Soma Zaidi...
Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?

Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito.

Soma Zaidi...