Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.

Dalili za mama aliyepasuka mfuko wa uzazi.

1. Kwanza kabisa Mama anayepasuka mfuko wa uzazi mara nyingi anakuwa kwenye uchungu, ila mfuko wa uzazi unapopasuka tu na uchungu unapungua kabisa badala ya kuendelea hiyo inakuwa ni mojawapo ya Dalili ya kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

 

2. Pia Mama anakuwa na maumivu ya kupita kiasi , hasa hasa ukigusa kwenye tumbo la Mama ,yeye anakuwa na maumivu na analalamika sana kuhusu tumbo kwa hiyo hii ni Dalili mojawapo ya Mama mwenye tatizo la kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

 

3. Pia na msukumo wa damu unapungua na kuipima unakuta uko chini kabisa na pia mapigo ya mtoto yanayopungua au kwa upande mwingine kama mtoto amashafariki yanakuwa hayapo kabisa.

 

4. Pia kwa upande wa mama na mapigo ya moyo yanapungua yaani sauti inasikikia kwa shida sana , kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa mama kama yuko kwenye vituo vya afya apelekwe kwenye hospitali kubwa kwa uangalizi zaidi.

 

5. Pia na Mama anaay kutokwa na damu kwenye sehemu za siri kwa kawaida damu hiyo utegemea inaweza kuwa nyingi au ya kawaida.

 

6. Pia  na  mtoto ukishika kwenye tumbo ni rahisi kuhisi kwa mikono na unapokuwa unapapasa tumbo la Mama Maumivu yanakuwa ni makali mno na mama anakuwa analalamika sana.

 

7. Kwa hiyo kwa wauguzi na wataalam wa afya baada ya kuona hayo yote ni vizuri kabisa  kumsaidia Mama ili asije kupoteza maisha kwa sababu hii ni Dalili mojawapo ya hatari kwa Mama wajawazito kwa hiyo ni vizuri kabisa kugundua mapema kabisa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views: 5028

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 web hosting     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Zifahamu sifa za mtoto mchanga.

Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy

Soma Zaidi...
Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.

Soma Zaidi...
Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.

Soma Zaidi...