Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom
Hatari ya kupata ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito.
1. Ikitokea mtu akapata damu kwenye kipindi cha ujauzito Kuna hatari ya mimba kuharibika na kutojifungua mtoto.kwa hiyo kama Mama ana mimba na akaona damu inatoka kawaida kama yupo kwenye siku za mwezi nai vizuri kabisa kuwahi hospital Ili kuangalia zaidi kwa sababu uenda kukatokea hatari ya mimba kuharibika kwa sababu dalili hii sio nzuri kwa mama Mjamzito.
2. Pia Kuna hatari ya kujifungua mtoto kabla ya wakati wake.
Na tatizo hili la kutokwa na damu wakati wa ujauzito Kuna hatari ya kujifungua mtoto kabla ya wakati wake, kwa sababu mimba ikishatungwa hakuna mfumo wowote wa urutubishaji unaotoka na mtu akatokwa na damu kama vile Hana mimba kwa hiyo kama ikitokea Mama akatokwa na damu labda inawezekana Kuna maambukizi zaidi ambayo usababisha damu kutoka na hali hiyo usababisha mtoto kuzaliwa kabla ya wakati.
3. Vile vile kutokwa na damu wakati wa ujauzito usababisha kuzaliwa kwa mtoto mwenye uziti wa chini.
Kwa kawaida uzito wa mtoto ni kuanzia kilo mbili na nusu mpaka kilo tatu na nusu, uzito wa mtoto ukianzia kilo tatu na nukta sita na kuendelea hii nayo ni shida na ikitokea mtoto akazaliwa chini ya uzito wa kilo mbili na point nne ni uzito mdogo kwa hiyo Kuna sababu mbalimbali ambazo usababisha mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mdogo ni kwa sababu ya kuwepo kwa kitendo cha kutokwa na damu wakati wa ujauzito, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwahi hospitals endapo tatizo hili likijitokeza Ili kuepukana na changamoto hii.
4. Tatizo lingine ambalo linaweza kutokea ni kupungukiwa na damu wakati wa kujifungua.
Kwa kawaida Mama akikaribia kujifungua ni vizuri kabisa kuwa na damu ya kutosha kwenye mwili Ili kuweza kujifungua salama kwa sababu wakati wa kujifungua utokea matatizo mbalimbali kama vile kumwaga damu au pengine mtoto anaweza kuwa amekaa vibaya na wakaamua kufanya upasuaji na damu umwagika kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwepo kwa damu ya kutosha ila kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kutokwa na damu wakati wa ujauzito usababisha damu kupungua mwilini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Mapendekezo muhimu kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule
Soma Zaidi...Zijue sababu zinazosababisha kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume
Kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume kunamaanisha kuwa Majimaji (shahawa) unayotoa wakati wa kufika kileleni huwa na mbegu chache kuliko kawaida. Hesabu yako ya manii inachukuliwa kuwa chini kuliko kawaida ikiwa una chini ya mbegu milioni 15. Kuwa na idad
Soma Zaidi...Njia za uzazi wa mpango zinazomhusisha mwanaume
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango unavyofanya na mwanaume kushiriki, ni njia ambayo umfanye mwanaume awe mhusika hasa wakati wa kujamiiana.
Soma Zaidi...Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho
Wajawazito wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiungulia, makala hii itakujulisha njia za kukabiliana na kiungulia, dalili zake na dawa zake
Soma Zaidi...Njia za kiasili zilizotumika zamani kqtika kupima ujauzito
Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito
Soma Zaidi...Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi
Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.
Soma Zaidi...