Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.
Kazi za metronidazole.
1. Metronidazole ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa katika kupambana na aina mbalimbali za minyoo, dawa hii iko katika mifumo mbalimbali, kama vile vidonge vya kawaida, kwenye maji maji ambayo utumiwa sana na watoto na pengine kwenye mfumo wa gel, pamoja na kuwa kwenye mifumo mingi mfumo ambao utumika sana ni vidonge, dawa hii ya metronidazole inayotolewa kwa njia ya vidonge umengenywa na kufanya kazi kuanzia saa moja mpaka matatu.
2.Dozi ya dawa ya metronidazole kwa watu wazima ni milligram mia nne mara tatu kwa siku kwa kawaida utolewa kwa siku saba na kwa watoto ni milligram saba na nusu kwa kila maasaa manane dozi hii utolewa kwa njia ya vidonge. Na pia dawa hii inaweza kupitia kwenye njia ya haja kubwa ambayo kwa kitaalamu huitwa by rectum, ambapo gramu moja utolewa kwa masaa manane ndani ya siku tatu na baadae gram moja kila baada ya masaa kumi na mawili hii ni kwa watu wazima.
3. Na kwa watoto ni kila baada ya masaa manane kwa siku tatu, tena baadaye kila baada ya masaa kumi na mawili kwa umri kuanzia miaka zero mpaka mwaka mmoja na milligram yake ni mia ishirini na tano. Na kuanzia mwaka mmoja mpaka miaka mitano ni milligram mia mbili ishirini na tano, na kuanzia miaka mitano mpaka miaka kumi ni milligram mia tano na kuanzia miaka kumi na kuendelea ni gram moja. Hasa hasa njia ya kupitisha dawa hii kwa mgonjwa yeyote kwa njia ya haja kubwa ambayo uitwao by rectum wagonjwa hawa huwa wanashindwa kumeza au wana degedege.
4. Na kwa wakati mwingine dawa hii upitishwa kwenye mishipa ya damu ambayo kwa kitaalamu huitwa intravenous, ambapo mtu mzito upatata milligram mia tano kwa masaa manne na kwa mtoto Upata milligram saba na nusu kwa kwa masaa manne, njia hii ni nzuri kwa sababu dawa yote uenda moja kwa moja kwenye damu na kuweza kuleta matokeo mazuri mapema.
5. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo kama vile harufu mbaya kwenye mdomo, kizungu Zungu, maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo pia yanaweza kutokea na pia kuna angalisho katika kutumia dawa hii, mtumiaji hapaswi kuonja pombe hata kidogo wakati anapotumia dawa hii kwa sababu dawa hii uingiliana na pombe, kwa hiyo mtumiaji hapaswi kabisa kuonja pombe akiwa anatumia dawa ya metronidazole. Kwa hiyo dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela masharti na ushauri wa daktari unapaswa kuzingatiwa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi tofauti mbalimbali za uke, kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kuna tofauti mbalimbali za ute kutegemea na hali iliyopo.
Soma Zaidi...Kunyonyesha ni moja katika njia za asili za kuzuia upatikanaji wa miba nyingine. Hata hivyo hii haimaanishi kuwa huwezi kupata mimba ukiwa unavyonyesha.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h
Soma Zaidi...Hali ya ujauzito huanza kutabirika Mara tu ya kujamiana, pia chemikali (hormon) za mwili huanza mchakato wa kuongeza na kupunguza utendaji kazi wa kemikali hizo mfano.follical stimulating hormon (FSH) na lutenazing hormon kuivisha yai tayari kwa kutengen
Soma Zaidi...Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...Inashangaza sana, wakati wengine wanahangaika kutafutavijauzito kwa gharama yoyote ile, kuna wengine wanataka kutoa ujauzito kwa gharama yeyote ile. Unadhani njia za kienyeji sa kutoa mimba ni salama?
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.
Soma Zaidi...