Kazi ya metronidazole

Kazi ya metronidazole

Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.

Kazi za metronidazole.

1. Metronidazole ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa katika kupambana na aina mbalimbali za minyoo, dawa hii iko katika mifumo mbalimbali, kama vile vidonge vya kawaida, kwenye maji maji ambayo utumiwa sana na watoto na pengine kwenye mfumo wa gel, pamoja na kuwa kwenye mifumo mingi mfumo ambao utumika sana ni vidonge, dawa hii ya metronidazole inayotolewa kwa njia ya vidonge  umengenywa na kufanya kazi kuanzia saa moja mpaka matatu.

 

2.Dozi ya dawa ya metronidazole kwa watu wazima ni milligram mia nne mara tatu kwa siku kwa kawaida utolewa kwa siku saba na kwa watoto ni milligram saba na nusu kwa kila maasaa manane dozi hii utolewa kwa njia ya vidonge. Na pia dawa hii inaweza kupitia kwenye njia ya haja kubwa ambayo kwa kitaalamu huitwa by rectum, ambapo gramu moja utolewa kwa masaa manane ndani ya siku tatu na baadae gram moja kila baada ya masaa kumi na mawili hii ni kwa watu wazima.

 

3. Na kwa watoto ni kila baada ya masaa manane kwa siku tatu, tena baadaye kila baada ya masaa kumi na mawili kwa umri kuanzia miaka zero mpaka mwaka mmoja na milligram yake ni mia ishirini na tano. Na kuanzia mwaka mmoja mpaka miaka mitano ni milligram mia mbili ishirini na tano, na kuanzia miaka mitano mpaka miaka kumi ni milligram mia tano na kuanzia miaka kumi na kuendelea ni gram moja. Hasa hasa njia ya kupitisha dawa hii kwa mgonjwa yeyote kwa njia ya haja kubwa ambayo uitwao by rectum wagonjwa hawa huwa wanashindwa kumeza au wana degedege.

 

4. Na kwa wakati mwingine dawa hii upitishwa kwenye mishipa ya damu ambayo kwa kitaalamu huitwa intravenous, ambapo mtu mzito upatata milligram mia tano kwa masaa manne na kwa mtoto Upata milligram saba na nusu kwa kwa masaa manne, njia hii ni nzuri kwa sababu dawa yote uenda moja kwa moja kwenye damu na kuweza kuleta matokeo mazuri mapema.

 

5. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo kama vile harufu mbaya kwenye mdomo, kizungu Zungu, maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo pia yanaweza kutokea na pia kuna angalisho katika kutumia dawa hii, mtumiaji hapaswi kuonja pombe hata kidogo wakati anapotumia dawa hii kwa sababu dawa hii uingiliana na pombe, kwa hiyo mtumiaji hapaswi kabisa kuonja pombe akiwa anatumia dawa ya metronidazole. Kwa hiyo dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela masharti na ushauri wa daktari unapaswa kuzingatiwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views: 8207

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za Maambukizi na Uvimbe katika mirija ya uzazi

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika  mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya hedhi

Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine,&nbsp

Soma Zaidi...
Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.

Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na maradhi ya ini

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ambavyo utaweza kujiepusha na maradhi ya ini

Soma Zaidi...
Ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.

Soma Zaidi...