Kazi ya metronidazole

Kazi ya metronidazole

Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole.

Kazi za metronidazole.

1. Metronidazole ni mojawapo ya dawa ambayo imependekezwa katika kupambana na aina mbalimbali za minyoo, dawa hii iko katika mifumo mbalimbali, kama vile vidonge vya kawaida, kwenye maji maji ambayo utumiwa sana na watoto na pengine kwenye mfumo wa gel, pamoja na kuwa kwenye mifumo mingi mfumo ambao utumika sana ni vidonge, dawa hii ya metronidazole inayotolewa kwa njia ya vidonge  umengenywa na kufanya kazi kuanzia saa moja mpaka matatu.

 

2.Dozi ya dawa ya metronidazole kwa watu wazima ni milligram mia nne mara tatu kwa siku kwa kawaida utolewa kwa siku saba na kwa watoto ni milligram saba na nusu kwa kila maasaa manane dozi hii utolewa kwa njia ya vidonge. Na pia dawa hii inaweza kupitia kwenye njia ya haja kubwa ambayo kwa kitaalamu huitwa by rectum, ambapo gramu moja utolewa kwa masaa manane ndani ya siku tatu na baadae gram moja kila baada ya masaa kumi na mawili hii ni kwa watu wazima.

 

3. Na kwa watoto ni kila baada ya masaa manane kwa siku tatu, tena baadaye kila baada ya masaa kumi na mawili kwa umri kuanzia miaka zero mpaka mwaka mmoja na milligram yake ni mia ishirini na tano. Na kuanzia mwaka mmoja mpaka miaka mitano ni milligram mia mbili ishirini na tano, na kuanzia miaka mitano mpaka miaka kumi ni milligram mia tano na kuanzia miaka kumi na kuendelea ni gram moja. Hasa hasa njia ya kupitisha dawa hii kwa mgonjwa yeyote kwa njia ya haja kubwa ambayo uitwao by rectum wagonjwa hawa huwa wanashindwa kumeza au wana degedege.

 

4. Na kwa wakati mwingine dawa hii upitishwa kwenye mishipa ya damu ambayo kwa kitaalamu huitwa intravenous, ambapo mtu mzito upatata milligram mia tano kwa masaa manne na kwa mtoto Upata milligram saba na nusu kwa kwa masaa manne, njia hii ni nzuri kwa sababu dawa yote uenda moja kwa moja kwenye damu na kuweza kuleta matokeo mazuri mapema.

 

5. Dawa hii pia huwa na maudhi madogo madogo kama vile harufu mbaya kwenye mdomo, kizungu Zungu, maumivu ya kichwa, maumivu ya tumbo pia yanaweza kutokea na pia kuna angalisho katika kutumia dawa hii, mtumiaji hapaswi kuonja pombe hata kidogo wakati anapotumia dawa hii kwa sababu dawa hii uingiliana na pombe, kwa hiyo mtumiaji hapaswi kabisa kuonja pombe akiwa anatumia dawa ya metronidazole. Kwa hiyo dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela masharti na ushauri wa daktari unapaswa kuzingatiwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF
Views: 8189

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 web hosting     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za mimba kutoka.

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba changa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba changa

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14

Soma Zaidi...
Uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga manii nje.

Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.

Soma Zaidi...