Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kuadhiri Uponyaji wa jeraha.jeraha huleta maumivu makali sana, vilevile Uvimbe, kutoa usaha. Pia jeraha hutofautiana katika kupona kwa mtu mzima na Mtoto.
Mambo Yanayoathiri Uponyaji wa Jeraha
1. Ukubwa au Kiwango cha jeraha: Jeraha dogo la juu juu hupona haraka kuliko jeraha kubwa na
majeraha ya kina zaidi.
2. Hali ya lishe: Lishe duni huchelewesha uponyaji wa jeraha na kwa watu wenye majeraha wanatakiwa kupata lishe Bora zaidi ambayo inaweza kuponesha kidonda kwa haraka.
3. Utoaji wa kiasi cha kutosha cha protini, vitamini C na kalori huharakisha uponyaji kwa Sababu huupatia mwili nguvu hivyo kupelekea sehemu penye jeraha kuwahi kupona lakini akisa protein vitamini C lazima kidonda kuchelewa kupona.
4. Mahali kidonda kilipo: Majeraha kwenye miguu na mikono au kutosafishwa kidogo hupona polepole kuliko majeraha usoni au kichwani.
5. Umri wa mgonjwa: Uponyaji ni wa haraka zaidi kwa watoto na vijana kuliko wazee na watu wazima kwa sababu tishu,Ngozi na hata mifupa ya Mtoto mdogo (viungo) Huma haijakomaa na huwahi kupona kuliko viungo vya mtu mzima.
6. Kitu kilichoingia kwenye jeraha Kama vile msubari, mwiba n.k Uponyaji hautafanyika hadi miili ya kigeni iondolewe kwenye hilo jeraha. Miili hii ya kigeni inaweza kuwa katika mfumo wa tishu zilizoharibiwa, vipande vilivyoingizwa vya mbao, na metali za mirija ya mifereji ya maji.
7. Kuvuja damu na kutokwa na damu: Hizi huongeza muda wa uponyaji kwa vile hutoa nzuri njia ya utamaduni kwa ukuaji wa viumbe vidogo.
8.Uwepo wa magonjwa mengine: Magonjwa kama vile kisukari (diabetes mellitus) huongeza muda wa kupona, majeraha yanayotokana na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu.
8. Dawa fulani: Dawa zinazoweza kubadilisha kiwango cha uponyaji ni pamoja na dawa za kuzuia uchochezi, kama vile dawa za kukandamiza kinga na saratani.
Mwisho; Ni vyema ukipata jeraha uende kituo Cha afya ili kupata matibabu Kama vile kidonda kusafishwa, kutolewa uchafu ulioingia Ndani ya kidonda, kutolea usaha na majimaji machafu yanayoleta Uvimbe kwenye kidonda, pia matibabu hayo yatakusaidia na dactari atakupa maelekezo zaidi ya kukusaidia jeraha lako kupona.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya vidonda vya tumbo, ni hatari inayotokea kwa mtu ambaye haujatibiwa vidonda vya tumbo.
Soma Zaidi...Kukaza kwa misuli lunaweza kutokea muda wowote ila mara nyingi hutokea pindi mtu anapofanya mazoezi, amnapoogelea ama anapofanya kazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina kuu za vidonda,kuna aina kuu tatu za vidonda ambapo kila aina utumiwa kwa njia yake kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hiii ni ratiba ambayo chanjo hii utolewa na ushauri mbalimbali utolewa ili kuweza kufanikisha kazi ya chanjo hii
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k
Soma Zaidi...Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya madini mwilini
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...