picha

Fahamu kuhusu michubuko kwa watoto wakati wa kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi michubuko ambayo mara nyingi utokea kwa watoto wakati wa kuzaliwa,na mara nyingi uweza kupona baada ya masaa ishilini na manne au ndani ya masaa ishilini na manne.

Michubuko kwa watoto wakati wa kuzaliwa.

1. Kwanza kabisa tunafahamu mtoto anapozaliwa upitia sehemu mbalimbali na hatua mbalimbali Ili kuweza kutoka nje ya tumbo la uzazi la mama ,Kuna wakati mwingine kichwa cha mtoto na kiuno cha mama ambapo mtoto anapaswa kupitia huwa havilingani hali ambayo usababisha mtoto kutumia nguvu Ili kutoka nje na hivyo kusababisha michubuko kwenye kichwa cha mtoto kwa hiyo wataalamu wa afya ni vizuri kabisa kugundua  hali hizi Ili kuweza kuepuka na hali ya michubuko wakati wa mtoto kuzaliwa.

 

2. Tunaposema kuhusu michubuko sio kama Ile ya Kawaida  ya kuchubuka kwa ngozi, michubuko mingine uingia ndani ya layer za ndani hali ambayo usababisha mtoto kuvuja kwa ndani na dalili mojawapo ni mtoto kuwa na macho mekundu au kuvimba uso na wakati mwingine mtoto anakuwa analia kila unapomgusa kichwani au kumshika kwa sababu ya kutojisikia vizuri mtoto anaweza kushindwa kunyonya na pengine kukosa Raha na kulia mara kwa mara , kwa hiyo ni vizuri kabisa kwa wataalamu wa afya kugundua tatizo mapema na kufanyia utafiti Ili kuweza kuepuka madhara mengine zaidi.

 

3. Vile vile Kuna michubuko ambayo ujitokeza nje yaani mtoto anakuwa amevimba kichwani pindi anapozaliwa,hali hii utokea hasa kwa akina mama wanaojifungua kwa mara ya kwanza ,kwa sababu utumia nguvu kubwa wakati wa kusukuma na pia utumia masaa mengi wakati wa kujifungua kuliko akina mama ambao wamejifungua Zaid ya mara Moja kwa hiyo, watoto wakizaliwa hivyo kwa kawaida upona ndani ya masaa ishilini na manne na pia usafi ni lazima, kwa hiyo akina mama hawapaswi kiwa na wasiwasi endapo mtoto akiwa amepata mikwaruzo kwenye kichwa ambayo uonekana kama uvimbe.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2187

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dalili za fizi kuvuja damu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda.

Soma Zaidi...
Kazi ya chanjo ya kifua kikuu

Posti hii inahusu kazi ya chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu huitwa BCG. Ni chanjo ambayo uzuia kifua kikuu na ukoma.

Soma Zaidi...
Ukiwa unalima sana unaweza kukonda

Unadhanivkufanya kazi kunaweza kukusababishia maradhi ama mwili kudhoofu, ama kukonda. Umeshawahivkujiuliza wanao nenepa huwa hawafanyi kazi?

Soma Zaidi...
Hatari ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Matokeo ya maumivu makali.

Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maumivu makali , kuna wakati mwingine mgonjwa anapata maumivu makali ya viungo na dawa mbalimbali uweza kutolewa kwa mgonjwa huyo lakini matokeo yake huwa ni kuendelea kwa maumivu kwa hiyo yafuatayo ni matokeo ya maumivu

Soma Zaidi...
Njia za kujilinda dhidi ya mapunye

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujilinda dhidi ya mapunye

Soma Zaidi...