picha

Fahamu kuhusu michubuko kwa watoto wakati wa kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi michubuko ambayo mara nyingi utokea kwa watoto wakati wa kuzaliwa,na mara nyingi uweza kupona baada ya masaa ishilini na manne au ndani ya masaa ishilini na manne.

Michubuko kwa watoto wakati wa kuzaliwa.

1. Kwanza kabisa tunafahamu mtoto anapozaliwa upitia sehemu mbalimbali na hatua mbalimbali Ili kuweza kutoka nje ya tumbo la uzazi la mama ,Kuna wakati mwingine kichwa cha mtoto na kiuno cha mama ambapo mtoto anapaswa kupitia huwa havilingani hali ambayo usababisha mtoto kutumia nguvu Ili kutoka nje na hivyo kusababisha michubuko kwenye kichwa cha mtoto kwa hiyo wataalamu wa afya ni vizuri kabisa kugundua  hali hizi Ili kuweza kuepuka na hali ya michubuko wakati wa mtoto kuzaliwa.

 

2. Tunaposema kuhusu michubuko sio kama Ile ya Kawaida  ya kuchubuka kwa ngozi, michubuko mingine uingia ndani ya layer za ndani hali ambayo usababisha mtoto kuvuja kwa ndani na dalili mojawapo ni mtoto kuwa na macho mekundu au kuvimba uso na wakati mwingine mtoto anakuwa analia kila unapomgusa kichwani au kumshika kwa sababu ya kutojisikia vizuri mtoto anaweza kushindwa kunyonya na pengine kukosa Raha na kulia mara kwa mara , kwa hiyo ni vizuri kabisa kwa wataalamu wa afya kugundua tatizo mapema na kufanyia utafiti Ili kuweza kuepuka madhara mengine zaidi.

 

3. Vile vile Kuna michubuko ambayo ujitokeza nje yaani mtoto anakuwa amevimba kichwani pindi anapozaliwa,hali hii utokea hasa kwa akina mama wanaojifungua kwa mara ya kwanza ,kwa sababu utumia nguvu kubwa wakati wa kusukuma na pia utumia masaa mengi wakati wa kujifungua kuliko akina mama ambao wamejifungua Zaid ya mara Moja kwa hiyo, watoto wakizaliwa hivyo kwa kawaida upona ndani ya masaa ishilini na manne na pia usafi ni lazima, kwa hiyo akina mama hawapaswi kiwa na wasiwasi endapo mtoto akiwa amepata mikwaruzo kwenye kichwa ambayo uonekana kama uvimbe.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2286

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 ai web app     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.

Soma Zaidi...
Vyakula vya madini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya madini mwilini

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mwenye uchafu kwenye sikio.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.

Soma Zaidi...
Jinsi moyo unavyosukuma damu

Post hii inahusu zaidi jinsi moyo unavyosukuma damu, moyo ni ogani ambayo usukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

Soma Zaidi...
Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa Damu kwenye moyo.

 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Soma Zaidi...