Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo.
Mambo muhimu ya kuongea na Mama mjamzito.
1. Maelezo kwa ujumla kuhusu Mama.
Maelezo kwa ujumla kuhusu mama kama vile kuna la mama, mme wake, sehemu anapoishi, miaka yake, kazi yake, kazi ya mwanaume, umri wa mwanaume ,jina mwenyekiti wa kijiji na number ya simu hayo yote uulizwa na mwanamke ili kuweza kujua wazi hali yake ingawa kama kitu chochote kimetokea iwe rahisi kumpata au kuna wanawake wengine ambao huwa wanaacha makusudi kwenye mahudhurio kwa kutumia maelezo kwa ujumla ni rahisi kumpata Mama huyo na kuweza kumpatia huduma za muhimu kwa hiyo ni kuhakikisha kujua hali halisi ya Mama.
2.Kujua juu ya mimba za Mama.
Kwa mama mjamzito akija kwenye mahudhurio ni lazima kujua hali ya mimba zake kwa ujumla kwa mfano mimba aliyonayo ni ya ngapi, amezaa watoto wangapi, je walio hai ni wangapi, ambao wamekufa ni wa ngapi au ni mimba ngapi zimetoka kwa kufanya hivyo tunaweza kuja matatizo aliyo nayo Mama katika kujifungua, kwa mfano kama mimba zimetoka tunaweza kujua chanzo cha kutoka kwa mimba na kupata tiba au kama watoto wanafariki kwa mda fulani tunaweza kujua sababu kwa hiyo kwa watoa huduma wanapaswa kuuliza mama kuhusu mimba zake zikoje na kama kuna tatizo liweze kutatuliwa.
3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua miezi ya mimba yake na kujua tarehe ya kujifungua.
Mama akija kwenye mahudhurio anapaswa kujua wazi siku ya kujifungua ambapo mhudumu wa afya ambaye ana ujuzi anaweza kumwesabia Mama kuanzia siku ya kwanza ya mwezi wa mwisho wa kuona siku za ke za mwezi na Mama akishaambiwa siku ya matarajio ya kujifungua anaanza kujiandaa taratibu na akisikia mabadiliko anaweza kwenda hospitali au kituo cha afya, na pia Mama anapaswa kujua wazi mda wa mimba yake ambapo kazi hiyo usaidiwa na mhudumu wa afya kuhakikisha kuwa Mama anajua wazi mda wa mimba yake.
4. Mzio au aleji yoyote kwa dawa na chakula.
Mama anapaswa kuongea na mhudumu wa afya kuhusu mzio wowote wa dawa na vyakula kwa sababu kila mahudhurio mama anapaswa kupewa dawa za minyoo, dawa za kumzuia mtoto hasipatwe na Malaria kwa kitaalamu dawa hizo huitwa sp na pia Mama anapaswa kupewa dawa za kuongeza damu ili akija kujifungua awe na damu ya kutosha , kwa kupewa dawa hizo Mama anapaswa kuwa wazi kama kuna dawa yoyote inayoletea mzio au aleji na kuweza kuibadilisha kwa hiyo tuwe makini kwa kujua mizio ya kila Mama.
5. Kumuuliza Mama kama anatumia vileo na Mambo mengine kama hayo.
Kitu kingine ni kumuuliza kuhusu matumizi ya pombe kali, madawa ya kulevya, na vitu vingine ambavyo utumiwa na wanawake wajawazito ambavyo kwa kitaalamu huitwa PICA vitu hivyo ni kama pembe, kula udongo,kula mkaa na vitu kwa ujumla ambavyo si vyakula vitu hivyo huwa havina faida yoyote kwenye mwili na pia Mama wajawazito wanapaswa kuelewa wazi madhara ya madawa ya kulevya, pombe na sigara kwa watoto na kuachana navyo wakati wa ujauzito.
6. Pia Mama anapaswa kuhimizwa kuhusu chanjo na milo anayoitumia kila siku.
Kwa kawaida tunajua kuwa wajawazito wanapaswa kupata chanjo mbalimbali kama vile Tetunus na vitamini A hizi chanjo umkinga mototo kutokana na magonjwa na pia vitamini A uepusha upofu wa mtoto kwa hiyo Mama anapaswa kupata chanjo ambazo ni za lazima na pia Mama mjamzito anapaswa kula na kushiba vizuri anapaswa kula milo mitano kwa siku kama ifuatavyo, kifungua kinywa cha asubuhi, saa nne au tano anapaswa kupata chochote, chakula cha mchana, saa kumi apate chochote na jioni mlo wa usiku.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume
Soma Zaidi...Tendo la ndoa wakati wa siku za hedhi ni halia mbayo jamii nying zinakataza. Katika vitabu vya dini pia haviruhusu, hata ki saikolojia utaona kuwa sio jambo jema. Hata hivyo hapa ninakuletea madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Soma Zaidi...Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye ngozi wakati wa ujauzito, ni mabadiliko yanayotokea kwenye ngozi ya Mama wakati wa ujauzito.
Soma Zaidi...