image

mambo ambayo utaulizwa mama mjamzito ukifika kituo cha afya unatakiwa utoe majibu sahihi.

Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo.

Mambo muhimu ya kuongea na Mama mjamzito.

1. Maelezo kwa ujumla kuhusu Mama.

Maelezo kwa ujumla kuhusu mama kama vile kuna la mama, mme wake, sehemu anapoishi, miaka yake, kazi yake, kazi ya mwanaume, umri wa mwanaume ,jina mwenyekiti wa kijiji na number ya simu hayo yote uulizwa na mwanamke ili kuweza kujua wazi hali yake ingawa kama kitu chochote kimetokea iwe rahisi kumpata au kuna wanawake wengine ambao huwa wanaacha makusudi kwenye mahudhurio kwa kutumia maelezo kwa ujumla ni rahisi kumpata Mama huyo na kuweza kumpatia huduma za muhimu kwa hiyo ni kuhakikisha kujua hali halisi ya Mama.

 

2.Kujua juu ya mimba za Mama.

Kwa mama mjamzito akija kwenye mahudhurio ni lazima kujua hali ya mimba zake kwa ujumla kwa mfano mimba aliyonayo ni ya ngapi, amezaa watoto wangapi, je walio hai ni wangapi, ambao wamekufa ni wa ngapi au ni mimba ngapi zimetoka kwa kufanya hivyo tunaweza kuja matatizo aliyo nayo Mama katika kujifungua, kwa mfano kama mimba zimetoka tunaweza kujua chanzo cha kutoka kwa mimba na kupata tiba au kama watoto wanafariki kwa mda fulani tunaweza kujua sababu kwa hiyo kwa watoa huduma wanapaswa kuuliza mama kuhusu mimba zake zikoje na kama kuna tatizo liweze kutatuliwa.

 

3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua miezi ya mimba yake na kujua tarehe ya kujifungua.

Mama akija kwenye mahudhurio anapaswa kujua wazi  siku ya kujifungua ambapo mhudumu wa afya ambaye ana ujuzi anaweza kumwesabia  Mama kuanzia siku ya kwanza ya  mwezi wa mwisho wa kuona siku za ke za mwezi na Mama akishaambiwa siku ya matarajio ya kujifungua anaanza kujiandaa taratibu na akisikia mabadiliko anaweza kwenda hospitali au kituo cha afya, na pia Mama anapaswa kujua wazi mda wa mimba yake ambapo kazi hiyo usaidiwa na mhudumu wa afya kuhakikisha kuwa Mama anajua wazi mda wa mimba yake.

 

4. Mzio au aleji yoyote kwa dawa na chakula.

Mama anapaswa kuongea na mhudumu wa afya kuhusu mzio wowote wa dawa na vyakula kwa sababu kila mahudhurio mama anapaswa kupewa dawa za minyoo,  dawa za kumzuia mtoto hasipatwe na Malaria kwa kitaalamu dawa hizo huitwa sp na pia Mama anapaswa kupewa dawa za kuongeza damu ili akija kujifungua awe na damu ya kutosha , kwa kupewa dawa hizo Mama anapaswa kuwa wazi kama kuna dawa yoyote inayoletea mzio au aleji na kuweza kuibadilisha kwa hiyo tuwe makini kwa kujua mizio ya kila Mama.

 

5. Kumuuliza Mama kama anatumia vileo na Mambo mengine kama hayo.

Kitu kingine ni kumuuliza  kuhusu matumizi ya pombe kali, madawa ya kulevya, na vitu vingine ambavyo utumiwa na wanawake wajawazito ambavyo kwa kitaalamu huitwa PICA vitu hivyo ni kama pembe, kula udongo,kula mkaa na vitu kwa ujumla ambavyo si vyakula vitu hivyo huwa havina faida yoyote kwenye mwili na pia Mama wajawazito wanapaswa kuelewa wazi madhara ya madawa ya kulevya, pombe na sigara kwa watoto na kuachana navyo wakati wa ujauzito.

 

6. Pia Mama anapaswa kuhimizwa kuhusu chanjo na milo anayoitumia kila siku.

Kwa kawaida tunajua kuwa wajawazito wanapaswa kupata chanjo mbalimbali kama vile Tetunus na vitamini A hizi chanjo umkinga mototo kutokana na magonjwa na pia vitamini A uepusha upofu wa mtoto kwa hiyo Mama anapaswa kupata chanjo ambazo ni za lazima na pia Mama mjamzito anapaswa kula na kushiba vizuri anapaswa kula milo mitano kwa siku kama ifuatavyo, kifungua kinywa cha asubuhi, saa nne au tano anapaswa kupata chochote, chakula cha mchana, saa kumi apate chochote na jioni mlo wa usiku. 



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/10/Monday - 11:25:03 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1074


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Nimegundua ni mjamzito na kibaya zaid namtoto mchanga nimefanyiwa opaleshen naomba ushauli wako mkuu
Inatakiwa angalau nafasivkati ya mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Soma Zaidi...

Mambo muhimu kuhusu mbegu za kiume
Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa s Soma Zaidi...

Dalili za mimba changa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba changa Soma Zaidi...

Dalili za ujauzito: Nini kinatokea kwanza
Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia. Soma Zaidi...

Tiba mbadala ya fangasi wa uumeni
Somo hili linakwenda kukuletea tiba mbadala ya fangasi wa uumeni Soma Zaidi...

Upungufu wa homoni ya cortisol
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni hii ya cortisol,hii ni homoni ambayo utokana na tezi glang(adrenal gland) kufanya kazi kupitiliza hali ambayo mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo wa mda mrefu, yaani wale watu ambao mda mwingi huwa wenye Soma Zaidi...

Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

Kuwepo kwa maziwa wakati wa ujauzito.
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa maziwa kwa akina Mama wakati wa ujauzito ni kawaida kwa sababu ya kuzaliwa kwa homoni ambayo usaidia kutoa maziwa. Soma Zaidi...

Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi
Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa. Soma Zaidi...

Nini sababu ya kuwashwa kwa njia ya mkojo kwa wanaume
Habari ya muda huu Dokata. Soma Zaidi...

Imani potofu kuhusu uzazi wa mpango
Post hii inahusu zaidi imani potofu kuhusu uzazi wa mpango, ni imani walizonazo Watu kuhusu matumizi ya uzazi wa mpango. Soma Zaidi...

Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.
Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka. Soma Zaidi...