Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo.
Mambo muhimu ya kuongea na Mama mjamzito.
1. Maelezo kwa ujumla kuhusu Mama.
Maelezo kwa ujumla kuhusu mama kama vile kuna la mama, mme wake, sehemu anapoishi, miaka yake, kazi yake, kazi ya mwanaume, umri wa mwanaume ,jina mwenyekiti wa kijiji na number ya simu hayo yote uulizwa na mwanamke ili kuweza kujua wazi hali yake ingawa kama kitu chochote kimetokea iwe rahisi kumpata au kuna wanawake wengine ambao huwa wanaacha makusudi kwenye mahudhurio kwa kutumia maelezo kwa ujumla ni rahisi kumpata Mama huyo na kuweza kumpatia huduma za muhimu kwa hiyo ni kuhakikisha kujua hali halisi ya Mama.
2.Kujua juu ya mimba za Mama.
Kwa mama mjamzito akija kwenye mahudhurio ni lazima kujua hali ya mimba zake kwa ujumla kwa mfano mimba aliyonayo ni ya ngapi, amezaa watoto wangapi, je walio hai ni wangapi, ambao wamekufa ni wa ngapi au ni mimba ngapi zimetoka kwa kufanya hivyo tunaweza kuja matatizo aliyo nayo Mama katika kujifungua, kwa mfano kama mimba zimetoka tunaweza kujua chanzo cha kutoka kwa mimba na kupata tiba au kama watoto wanafariki kwa mda fulani tunaweza kujua sababu kwa hiyo kwa watoa huduma wanapaswa kuuliza mama kuhusu mimba zake zikoje na kama kuna tatizo liweze kutatuliwa.
3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua miezi ya mimba yake na kujua tarehe ya kujifungua.
Mama akija kwenye mahudhurio anapaswa kujua wazi siku ya kujifungua ambapo mhudumu wa afya ambaye ana ujuzi anaweza kumwesabia Mama kuanzia siku ya kwanza ya mwezi wa mwisho wa kuona siku za ke za mwezi na Mama akishaambiwa siku ya matarajio ya kujifungua anaanza kujiandaa taratibu na akisikia mabadiliko anaweza kwenda hospitali au kituo cha afya, na pia Mama anapaswa kujua wazi mda wa mimba yake ambapo kazi hiyo usaidiwa na mhudumu wa afya kuhakikisha kuwa Mama anajua wazi mda wa mimba yake.
4. Mzio au aleji yoyote kwa dawa na chakula.
Mama anapaswa kuongea na mhudumu wa afya kuhusu mzio wowote wa dawa na vyakula kwa sababu kila mahudhurio mama anapaswa kupewa dawa za minyoo, dawa za kumzuia mtoto hasipatwe na Malaria kwa kitaalamu dawa hizo huitwa sp na pia Mama anapaswa kupewa dawa za kuongeza damu ili akija kujifungua awe na damu ya kutosha , kwa kupewa dawa hizo Mama anapaswa kuwa wazi kama kuna dawa yoyote inayoletea mzio au aleji na kuweza kuibadilisha kwa hiyo tuwe makini kwa kujua mizio ya kila Mama.
5. Kumuuliza Mama kama anatumia vileo na Mambo mengine kama hayo.
Kitu kingine ni kumuuliza kuhusu matumizi ya pombe kali, madawa ya kulevya, na vitu vingine ambavyo utumiwa na wanawake wajawazito ambavyo kwa kitaalamu huitwa PICA vitu hivyo ni kama pembe, kula udongo,kula mkaa na vitu kwa ujumla ambavyo si vyakula vitu hivyo huwa havina faida yoyote kwenye mwili na pia Mama wajawazito wanapaswa kuelewa wazi madhara ya madawa ya kulevya, pombe na sigara kwa watoto na kuachana navyo wakati wa ujauzito.
6. Pia Mama anapaswa kuhimizwa kuhusu chanjo na milo anayoitumia kila siku.
Kwa kawaida tunajua kuwa wajawazito wanapaswa kupata chanjo mbalimbali kama vile Tetunus na vitamini A hizi chanjo umkinga mototo kutokana na magonjwa na pia vitamini A uepusha upofu wa mtoto kwa hiyo Mama anapaswa kupata chanjo ambazo ni za lazima na pia Mama mjamzito anapaswa kula na kushiba vizuri anapaswa kula milo mitano kwa siku kama ifuatavyo, kifungua kinywa cha asubuhi, saa nne au tano anapaswa kupata chochote, chakula cha mchana, saa kumi apate chochote na jioni mlo wa usiku.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.
Soma Zaidi...Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.
Soma Zaidi...Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za ugumba kwa Mwanaume, ni sababu ambazo umfanye mwanaume ashindwe kumpatia mwanamke mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.
Soma Zaidi...Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Tendo la ndoa wakati wa siku za hedhi ni halia mbayo jamii nying zinakataza. Katika vitabu vya dini pia haviruhusu, hata ki saikolojia utaona kuwa sio jambo jema. Hata hivyo hapa ninakuletea madhara yake kiafya
Soma Zaidi...Dalili za mimba pekee haziwezi kuthibitisha uwepo wa mimba. Bila vipimo kwa. Muda sahihi huwezi kuwa. Na uhakika. Je na wewe unasumbuliwa na dalili za mimba na ukapona hakuna mimba? Makala hii ni kwa ajili yako. Swali
Soma Zaidi...