picha

Dalili za kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.

Dalili za kifafa cha mimba.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba kifafa cha mimba utokea pale ambapo mama mjamzito Upata degedege wakati wa ujauzito na hana historia ya kuwa na Ugonjwa huo au kuwepo kwa Malaria au Magonjwa yoyote ya akili,kwa hiyo dalili zifuatazo zinaweza kuonekana kwa mjamzito zinatambulika kuwa ni kuwepo kwa kifaa cha mimba.

 

2. Kuwepo kwa protini kwenye mkojo, hii ni mojawapo ya Dalili kwa sababu panakuwepo na tatizo kwenye kibofu cha mkojo mpaka protini inaonekana kwenye mkojo, kwa hiyo matibabu yanapaswa kufanyika mapema ili kuweza kupunguza kiwango hiki cha protini kwenye mkojo.

 

3. Kiwango cha shinikizo la damu juwa kubwa kuliko kawaida, kwa kawaida kiwango cha presha kinapaswa kuanzia sitini mpaka tisini kwa presha ya chini na mia ishirini mpaka mia arobaini kwa presha ya juu, utamkuta mja mzito ana presha mia sitini kwa mia na kumi kwa hiyo hii ni Dalili mbaya na inaitaji  huduma mara moja ili kuweza kupunguza kiwango hiki.

 

4. Kuvimba kwa miguu wakati wa ujauzito.

Pia kuna tatizo jingine ambapo Mama anavimba miguu wakati wa ujauzito na pengine anatembea kwa shida, kwa sababu ya kuwepo kwa dalili hii mjamzito anapaswa kuwahi hospitali kwa sababu ya vipimo.

 

5. Maumivu makali ya kichwa.

Vile vile kuna kipindi mjamzito anahisi maumivu makali ya kichwa kwa hiyo anapaswa kuwahi hospitali mapema ili kuweza kupata huduma mara moja.

 

6 Kuwepo kwa matatizo wakati wa kuona, kwa wakati mwingine mama mjamzito anaanza kuona kwa shida, au kuona maluwe luwe kwa hiyo anapaswa kuwahi na kupata matibabu mapema.

 

7. Pengine Wajawazito wanahisi kuwepo kwa kiungulia kisicho cha kawaida, kwa hiyo wanapaswa kutoa taarifa ili kuweza kutibiwa.

 

8. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi wajawazito wanapaswa kwenda mara moja hospitali ili kuweza kupata matibabu, kwa hiyo Mama maisha ni ya kwako na mtoto wako jaribu kuepuka matibabu yasiyo sahihi yaani kutibiwa kienyeji kwenye matatizo kama haya.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3331

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito, ni mojawapo ya njia ambazo utumiwa na wahudumu wa afya ili kuweza kuzuia upungufu wa damu kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Madhara ya kiafya ya kupiga punyeto

Post hii inakwenda kukutania madhara ya kuoiga punyeto kwa afya yako.

Soma Zaidi...
Signs and symptoms of pregnancy.

In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by mi

Soma Zaidi...
Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.

Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n

Soma Zaidi...