picha

Dalili za kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.

Dalili za kifafa cha mimba.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba kifafa cha mimba utokea pale ambapo mama mjamzito Upata degedege wakati wa ujauzito na hana historia ya kuwa na Ugonjwa huo au kuwepo kwa Malaria au Magonjwa yoyote ya akili,kwa hiyo dalili zifuatazo zinaweza kuonekana kwa mjamzito zinatambulika kuwa ni kuwepo kwa kifaa cha mimba.

 

2. Kuwepo kwa protini kwenye mkojo, hii ni mojawapo ya Dalili kwa sababu panakuwepo na tatizo kwenye kibofu cha mkojo mpaka protini inaonekana kwenye mkojo, kwa hiyo matibabu yanapaswa kufanyika mapema ili kuweza kupunguza kiwango hiki cha protini kwenye mkojo.

 

3. Kiwango cha shinikizo la damu juwa kubwa kuliko kawaida, kwa kawaida kiwango cha presha kinapaswa kuanzia sitini mpaka tisini kwa presha ya chini na mia ishirini mpaka mia arobaini kwa presha ya juu, utamkuta mja mzito ana presha mia sitini kwa mia na kumi kwa hiyo hii ni Dalili mbaya na inaitaji  huduma mara moja ili kuweza kupunguza kiwango hiki.

 

4. Kuvimba kwa miguu wakati wa ujauzito.

Pia kuna tatizo jingine ambapo Mama anavimba miguu wakati wa ujauzito na pengine anatembea kwa shida, kwa sababu ya kuwepo kwa dalili hii mjamzito anapaswa kuwahi hospitali kwa sababu ya vipimo.

 

5. Maumivu makali ya kichwa.

Vile vile kuna kipindi mjamzito anahisi maumivu makali ya kichwa kwa hiyo anapaswa kuwahi hospitali mapema ili kuweza kupata huduma mara moja.

 

6 Kuwepo kwa matatizo wakati wa kuona, kwa wakati mwingine mama mjamzito anaanza kuona kwa shida, au kuona maluwe luwe kwa hiyo anapaswa kuwahi na kupata matibabu mapema.

 

7. Pengine Wajawazito wanahisi kuwepo kwa kiungulia kisicho cha kawaida, kwa hiyo wanapaswa kutoa taarifa ili kuweza kutibiwa.

 

8. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi wajawazito wanapaswa kwenda mara moja hospitali ili kuweza kupata matibabu, kwa hiyo Mama maisha ni ya kwako na mtoto wako jaribu kuepuka matibabu yasiyo sahihi yaani kutibiwa kienyeji kwenye matatizo kama haya.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3200

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 web hosting     👉3 ai web app     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa

Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa saratani ya matiti

Saratani ya matiti ji moja kati ya saratani zinazosumbuwa wqnawake wengi. Katika somo hili utajifunza chanzo cha kutokea saratani ya matiti

Soma Zaidi...
Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza

Soma Zaidi...