picha

Dalili za kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.

Dalili za kifafa cha mimba.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba kifafa cha mimba utokea pale ambapo mama mjamzito Upata degedege wakati wa ujauzito na hana historia ya kuwa na Ugonjwa huo au kuwepo kwa Malaria au Magonjwa yoyote ya akili,kwa hiyo dalili zifuatazo zinaweza kuonekana kwa mjamzito zinatambulika kuwa ni kuwepo kwa kifaa cha mimba.

 

2. Kuwepo kwa protini kwenye mkojo, hii ni mojawapo ya Dalili kwa sababu panakuwepo na tatizo kwenye kibofu cha mkojo mpaka protini inaonekana kwenye mkojo, kwa hiyo matibabu yanapaswa kufanyika mapema ili kuweza kupunguza kiwango hiki cha protini kwenye mkojo.

 

3. Kiwango cha shinikizo la damu juwa kubwa kuliko kawaida, kwa kawaida kiwango cha presha kinapaswa kuanzia sitini mpaka tisini kwa presha ya chini na mia ishirini mpaka mia arobaini kwa presha ya juu, utamkuta mja mzito ana presha mia sitini kwa mia na kumi kwa hiyo hii ni Dalili mbaya na inaitaji  huduma mara moja ili kuweza kupunguza kiwango hiki.

 

4. Kuvimba kwa miguu wakati wa ujauzito.

Pia kuna tatizo jingine ambapo Mama anavimba miguu wakati wa ujauzito na pengine anatembea kwa shida, kwa sababu ya kuwepo kwa dalili hii mjamzito anapaswa kuwahi hospitali kwa sababu ya vipimo.

 

5. Maumivu makali ya kichwa.

Vile vile kuna kipindi mjamzito anahisi maumivu makali ya kichwa kwa hiyo anapaswa kuwahi hospitali mapema ili kuweza kupata huduma mara moja.

 

6 Kuwepo kwa matatizo wakati wa kuona, kwa wakati mwingine mama mjamzito anaanza kuona kwa shida, au kuona maluwe luwe kwa hiyo anapaswa kuwahi na kupata matibabu mapema.

 

7. Pengine Wajawazito wanahisi kuwepo kwa kiungulia kisicho cha kawaida, kwa hiyo wanapaswa kutoa taarifa ili kuweza kutibiwa.

 

8. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi wajawazito wanapaswa kwenda mara moja hospitali ili kuweza kupata matibabu, kwa hiyo Mama maisha ni ya kwako na mtoto wako jaribu kuepuka matibabu yasiyo sahihi yaani kutibiwa kienyeji kwenye matatizo kama haya.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3482

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa

Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoabkunaweza kuashiria kuwa kuna majeraha yametokea huwenda ni michubuko ilitokea ndio ikavujisha damu. Lakini kwa nini hali kama hii itokee. Posti hii itakwwnda mujibu swali hili.

Soma Zaidi...
CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO

Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...
maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba

Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi?

Soma Zaidi...
Signs and symptoms of pregnancy.

In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by mi

Soma Zaidi...