picha

Dalili za kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.

Dalili za kifafa cha mimba.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kwamba kifafa cha mimba utokea pale ambapo mama mjamzito Upata degedege wakati wa ujauzito na hana historia ya kuwa na Ugonjwa huo au kuwepo kwa Malaria au Magonjwa yoyote ya akili,kwa hiyo dalili zifuatazo zinaweza kuonekana kwa mjamzito zinatambulika kuwa ni kuwepo kwa kifaa cha mimba.

 

2. Kuwepo kwa protini kwenye mkojo, hii ni mojawapo ya Dalili kwa sababu panakuwepo na tatizo kwenye kibofu cha mkojo mpaka protini inaonekana kwenye mkojo, kwa hiyo matibabu yanapaswa kufanyika mapema ili kuweza kupunguza kiwango hiki cha protini kwenye mkojo.

 

3. Kiwango cha shinikizo la damu juwa kubwa kuliko kawaida, kwa kawaida kiwango cha presha kinapaswa kuanzia sitini mpaka tisini kwa presha ya chini na mia ishirini mpaka mia arobaini kwa presha ya juu, utamkuta mja mzito ana presha mia sitini kwa mia na kumi kwa hiyo hii ni Dalili mbaya na inaitaji  huduma mara moja ili kuweza kupunguza kiwango hiki.

 

4. Kuvimba kwa miguu wakati wa ujauzito.

Pia kuna tatizo jingine ambapo Mama anavimba miguu wakati wa ujauzito na pengine anatembea kwa shida, kwa sababu ya kuwepo kwa dalili hii mjamzito anapaswa kuwahi hospitali kwa sababu ya vipimo.

 

5. Maumivu makali ya kichwa.

Vile vile kuna kipindi mjamzito anahisi maumivu makali ya kichwa kwa hiyo anapaswa kuwahi hospitali mapema ili kuweza kupata huduma mara moja.

 

6 Kuwepo kwa matatizo wakati wa kuona, kwa wakati mwingine mama mjamzito anaanza kuona kwa shida, au kuona maluwe luwe kwa hiyo anapaswa kuwahi na kupata matibabu mapema.

 

7. Pengine Wajawazito wanahisi kuwepo kwa kiungulia kisicho cha kawaida, kwa hiyo wanapaswa kutoa taarifa ili kuweza kutibiwa.

 

8. Kwa hiyo baada ya kuona dalili kama hizi wajawazito wanapaswa kwenda mara moja hospitali ili kuweza kupata matibabu, kwa hiyo Mama maisha ni ya kwako na mtoto wako jaribu kuepuka matibabu yasiyo sahihi yaani kutibiwa kienyeji kwenye matatizo kama haya.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3623

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 ai web app     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Soma Zaidi...
Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu mapacha wanaofanana

Post hii inahusu zaidi watoto mapacha wanaofanana,ni watoto wanaozaliwa wakiwa wanaofanana kwa sura na hata group la damu huwa ni Moja.

Soma Zaidi...
Utaratibu kwa wajawazito na wanaonyonshesha wakiwa na virusi vya ukimwi na ukimwi

Je kuna madhara kwa mwenye virusi vya ukimwi kunyonyesha ama kubeba mimba, na nini afyanye kama ameshabeba mimba ama kama ananyonyesha

Soma Zaidi...
Kiwango cha juu cha Androgen

Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.

Soma Zaidi...
Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.

Soma Zaidi...