Mapendekezo  muhimu kwa wajawazito

Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Mapendekezo muhimu kwa wajawazito.

1.Kwanza kabisa wajawazito wanapaswa kuwa na mlo kamili na kupata chakula cha kutosha na pia akina mama wanapaswa kula vyakula vyenye wanga , protini, mafuta, mboga za majani, matunda na kunywa maji walau kwa siku glass nane na pia akina mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile kula pembe, Mawe na vitu vya aina hiyo na pia wanawake wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vikali pamoja na uvutaji wa bangi kwa sababu ni hatari kwa afya ya mtoto.

 

2. Pia akina Mama wanapaswa kuangaliwa kila mwezi kwa Upande wa Mama anapaswa kuangaliwa kama anavimba miguu, ana damu ya kutosha,ana malaria au anaumwa ugonjwa wowote kama kina shida kati ya hayo anapaswa kwenda kupata matibabu Mara moja, na kwa upande wa mtoto aliyeko tumboni anapaswa kuangaliwa jinsi alivyolala tumboni,kama anapumua , kupima kimo cha mtoto na kutabiri tarehe na siku ambayo mtoto atazaliwa kwa kufanya hivyo kila mwezi kwa asilimia tisini na tano mtoto atazaliwa salama.

 

3.Kuzuia magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

Kwa kuzuia magonjwa nyemelezi kama vile Malaria, kupungua kwa damu mwilini, kupima maambukizi ya virus vya ukimwi ni pendekezo la Muhimu sana ambalo homkinga mtoto na maradhi mbalimbali, kwa hiyo ili kupambana na magonjwa hayo kila baada ya mwezi Mama utumia vidonge vya sp, vidonge vya follic asidi kwa ajili ya kuongeza damu,kutumia dawa za minyoo pale anapoanza mahudhurio na pia Mama hupewa neti bure anapoanza mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kupambana na magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

 

4.Uangalizi wa Mama baada ya kujifungua na uangalizi mkubwa pale ambapo mimba inaonekana kubwa na vikwazo vingi, katika kipindi hiki Mama ambaye ana matatizo wakati wa kujifungua anapaswa kuja hospitalini mapema anapofikisha miezi ile inayofikiliwa kubwa huwa anapata matatizo, mama huwa kwenye uangalizi wa manes na wataalamu wa afya walio na ujuzi ili likitokea jambo lolote awe tayari kupambana nalo na kumfanya Mama akifungua salama.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views: 2235

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 web hosting     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

mpenzi wangu nimeshiriki nae tendo la ndoa akiwa siku zake za hatar kwa siku 3 lakin hajashika mimba tatizo linaweza kuwa ni nini?

Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili.

Soma Zaidi...
Uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga manii nje.

Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.

Soma Zaidi...
Ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango.

Posti hii inahusu zaidi ukweli kuhusu njia za uzazi wa mpango, sio kwa imani potofu ambazo Watu utumia kuelezea uzazi wa mpango.

Soma Zaidi...
Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto mchanga kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, ni tatizo ambalo utokea kwa baadhi ya wajawazito kupata mtoto mwenye Uzito mkubwa, wengine uona kama ni sifa ila Kuna madhara yanaweza kujitokeza kwa Mama hasa wakati wa kujif

Soma Zaidi...
Huduma kwa wanaotoa damu yenye mabonge

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Njia za kiasili zilizotumika zamani kqtika kupima ujauzito

Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito

Soma Zaidi...