picha

Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Mapendekezo muhimu kwa wajawazito.

1.Kwanza kabisa wajawazito wanapaswa kuwa na mlo kamili na kupata chakula cha kutosha na pia akina mama wanapaswa kula vyakula vyenye wanga , protini, mafuta, mboga za majani, matunda na kunywa maji walau kwa siku glass nane na pia akina mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile kula pembe, Mawe na vitu vya aina hiyo na pia wanawake wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vikali pamoja na uvutaji wa bangi kwa sababu ni hatari kwa afya ya mtoto.

 

2. Pia akina Mama wanapaswa kuangaliwa kila mwezi kwa Upande wa Mama anapaswa kuangaliwa kama anavimba miguu, ana damu ya kutosha,ana malaria au anaumwa ugonjwa wowote kama kina shida kati ya hayo anapaswa kwenda kupata matibabu Mara moja, na kwa upande wa mtoto aliyeko tumboni anapaswa kuangaliwa jinsi alivyolala tumboni,kama anapumua , kupima kimo cha mtoto na kutabiri tarehe na siku ambayo mtoto atazaliwa kwa kufanya hivyo kila mwezi kwa asilimia tisini na tano mtoto atazaliwa salama.

 

3.Kuzuia magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

Kwa kuzuia magonjwa nyemelezi kama vile Malaria, kupungua kwa damu mwilini, kupima maambukizi ya virus vya ukimwi ni pendekezo la Muhimu sana ambalo homkinga mtoto na maradhi mbalimbali, kwa hiyo ili kupambana na magonjwa hayo kila baada ya mwezi Mama utumia vidonge vya sp, vidonge vya follic asidi kwa ajili ya kuongeza damu,kutumia dawa za minyoo pale anapoanza mahudhurio na pia Mama hupewa neti bure anapoanza mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kupambana na magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

 

4.Uangalizi wa Mama baada ya kujifungua na uangalizi mkubwa pale ambapo mimba inaonekana kubwa na vikwazo vingi, katika kipindi hiki Mama ambaye ana matatizo wakati wa kujifungua anapaswa kuja hospitalini mapema anapofikisha miezi ile inayofikiliwa kubwa huwa anapata matatizo, mama huwa kwenye uangalizi wa manes na wataalamu wa afya walio na ujuzi ili likitokea jambo lolote awe tayari kupambana nalo na kumfanya Mama akifungua salama.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2172

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupata mtoto wa kiume

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.

Soma Zaidi...
Kiwango cha juu cha Androgen

Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya kuharibika kwa mimba ya miezi kuanzia 0-3

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuharibika kwa mimba kuanzia miezi zero mpaka miezi mitatu, kwa sababu hii ni miezi ya kwanza kabisa Kuna sababu au vyanzo vya kuharibika kwa mimba katika kipindi hiki.

Soma Zaidi...