Mapendekezo muhimu kwa wajawazito


image


Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ulemavu wa aina yoyote ile.


Mapendekezo muhimu kwa wajawazito.

1.Kwanza kabisa wajawazito wanapaswa kuwa na mlo kamili na kupata chakula cha kutosha na pia akina mama wanapaswa kula vyakula vyenye wanga , protini, mafuta, mboga za majani, matunda na kunywa maji walau kwa siku glass nane na pia akina mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini kama vile kula pembe, Mawe na vitu vya aina hiyo na pia wanawake wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vikali pamoja na uvutaji wa bangi kwa sababu ni hatari kwa afya ya mtoto.

 

2. Pia akina Mama wanapaswa kuangaliwa kila mwezi kwa Upande wa Mama anapaswa kuangaliwa kama anavimba miguu, ana damu ya kutosha,ana malaria au anaumwa ugonjwa wowote kama kina shida kati ya hayo anapaswa kwenda kupata matibabu Mara moja, na kwa upande wa mtoto aliyeko tumboni anapaswa kuangaliwa jinsi alivyolala tumboni,kama anapumua , kupima kimo cha mtoto na kutabiri tarehe na siku ambayo mtoto atazaliwa kwa kufanya hivyo kila mwezi kwa asilimia tisini na tano mtoto atazaliwa salama.

 

3.Kuzuia magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

Kwa kuzuia magonjwa nyemelezi kama vile Malaria, kupungua kwa damu mwilini, kupima maambukizi ya virus vya ukimwi ni pendekezo la Muhimu sana ambalo homkinga mtoto na maradhi mbalimbali, kwa hiyo ili kupambana na magonjwa hayo kila baada ya mwezi Mama utumia vidonge vya sp, vidonge vya follic asidi kwa ajili ya kuongeza damu,kutumia dawa za minyoo pale anapoanza mahudhurio na pia Mama hupewa neti bure anapoanza mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kupambana na magonjwa nyemelezi kwa Mama na mtoto.

 

4.Uangalizi wa Mama baada ya kujifungua na uangalizi mkubwa pale ambapo mimba inaonekana kubwa na vikwazo vingi, katika kipindi hiki Mama ambaye ana matatizo wakati wa kujifungua anapaswa kuja hospitalini mapema anapofikisha miezi ile inayofikiliwa kubwa huwa anapata matatizo, mama huwa kwenye uangalizi wa manes na wataalamu wa afya walio na ujuzi ili likitokea jambo lolote awe tayari kupambana nalo na kumfanya Mama akifungua salama.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Huduma ya kwanza kwa mgonjwa aliyepata ajali ya kichwa
Ajali ya kichwa na ajali inayotolewa kwenye sehemu mbalimbali za kichwa, ambavyo husababishwa madhara kwa aliyepata ajali hiyo Soma Zaidi...

image Malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele.
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kumsafisha mgonjwa nywele zake, ni sababu ambazo upelekea kumsafisha mgonjwa nywele kama tutakavyoona hapo chini. Soma Zaidi...

image Umuhimu wa uzazi wa mpango
Uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na WA awake na wasichana Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji na kuepuka mimba zisizotarajiwa. Soma Zaidi...

image Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)
maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri wanaume na wanawake na hutokea katika makundi yote ya umri, ingawa imeenea zaidi kati ya wanawake vijana. si vigumu kutibu mara tu unapojua kuwa unayo. Hata hivyo, ikiwa haitatibiwa, inaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi ya afya Soma Zaidi...

image Dalili na madhara ya Kiungulia
post hii inaelezea kuhusiana na dalili au ishara na madhara ya Kiungulia ni maumivu ya moto kwenye kifua chako, nyuma ya mfupa wako wa kifua. Maumivu huwa mabaya zaidi wakati wa kulala au kuinama Soma Zaidi...

image Kushambukiwa kwa moyo na kupumua
Post hii inahusu zaidi kuhusu kushambuliwa kwa moyo na kupumua, kushambuliwa kwa moyo na kupumua kwa kitaala huitwa (cardiopulmonary Arrest) ni kitendo Cha kusimama ghafla kwa moyo na kupumua. Soma Zaidi...

image tatizo la kushindwa kujaza misuli ya mwilini na kusinyaa kwa misuli mwilini
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kusinyaa kwa Misuli. Ni maradhi yanayopelekea uzalishwaji hafifu wa misuli, hivyo kupelekea misuli kukosa protini, kushunwa kukuwa na kusinyaa. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa surua kwa watoto.
Surua ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na homa na upele mwekundu, unaotokea utotoni. Wakati mtu aliye na virusi akikohoa au kupiga chafya, matone yaliyoambukizwa huenea angani na kutua kwenye sehemu zilizo karibu. Mtoto anaweza kupata virusi kwa kuvuta matone haya au kwa kugusa na kisha kugusa uso, mdomo, macho au masikio yao. Surua ni ugonjwa unaoambukiza sana unaosababishwa na virusi vya surua Soma Zaidi...

image Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kushuka
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kushuka Soma Zaidi...

image Habari,mfano umekunywa dawa za chupa hizi halafu baadae unagundua chupa ilikuwa na UFA nn kofanyike
Kunywa soda ama dawa kwenyechupa zakioo ambayo ina ufa ama mipasuko ni hatari. Ni kwa sababu huwezijuwa huwenda kipande kikaingia mdomoni na umangimeza. Sasa nini ufanye endapo umeshakula? Soma Zaidi...