picha

Fahamu ugonjwa wa kifafa cha mimba.

Post hii inahusu zaidi Ugonjwa wa kifafa cha mimba ambapo kwa kitaalamu huitwa eclampsia, utokea pale ambapo Mama anapokuwa na degedege wakati wa mimba na baada ya kujiunga.

Ugonjwa wa kifafa cha mimba.

1. Kama tulivyoona hapo juu kwamba Ugonjwa huu usababishwa na kuwe kwa kifafa wakati wa ujauzito na mtu anakuwa hana historia yoyote ya kifafa au Magonjwa ya akili au Malaria, ila utokea tu hasa wakati wa ujauzito na wakati baada ya kujifungua, kwa hiyo tatizo hili halijapata ufumbuzi zaidi kwamba kisababishi ni nini.

 

2.Pamoja na kukosa kisababishi Tatizo hili uwapata hasa hasa wanawake wenye shinikizo la damu wakati wa ujauzito na kuwepo kwa kiasi kikubwa cha protini kwenye mkojo, kwa hiyo hali hii ikitokea kwa wajawazito ni lazima kutibu mapema ili kuepuka kuwepo kwa tatizo la kifafa wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua kwa hiyo wauguzi na ndugu wa karibu ni jukumu la kuwa sana karibu na wanawake walio katika hatari ya kupata tatizo hili na kuwasaidia wale walio kwisha pata Ugonjwa huu.

 

3. Kwa hiyo ili kuweza kuepuka tatizo hili wanawake wote wanapaswa kuhudhuria kliniki mapema pale wanapogundua kwamba ni wajawazito kwa sababu kwa kufanya hivyo wakiwa kliniki wanapata mafunzo mbalimbali kuhusu Dalili za hatari wakati wa ujauzito na pia kupima presha kila udhulio ili kuhakikisha kama hali ya Mama iko sawa ikitokea Mama akakutwa na presha au protini kwenye mkojo matibabu uanza mapema na tatizo haliwezi kuwa kubwa kama yule ambaye hakutambua mapema.

 

4. Vile vile kuna mila na desturi ambazo ufanyika kwenye jamii kwa kutumia matibabu yasiyo sahihi kwa kuwatumia waganga wa kienyeji pale Mama akipata kifafa hali ambayo Usababisha hali za wamama kuwa mbaya na kusababisha vifo wakati wa ujauzito,kwa hiyo ni vizuri elimu ikatolewa kwa jamii ili kuweza kuepuka vifo visivyo vya lazima kwa watoto na akina Mama, kwa hiyo akina Mama wawe Macho ili kuokoa maisha yao na watoto wao .

 

5.Endapo Mama wajawazito wakihisi dalili ambazo si za kawaida wanapaswa kuwahi mapema hospitali na kuwahi mapema kliniki mara tu wanapohisi wana mimba ili kuweza kupata huduma muhimu na za kweli.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2945

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 web hosting     👉4 ai web app     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Haya maji meupe hutokea wakat mimba ishatungwa au ukifanya tendo la ndoa lazima utokee?

Majimaji yanayitoka kwenye uke yanafungamana na taarifa nyingi kuhusu afya vya mwanamke. Ujauzito, maradhi, mabadiliko ya homoni na zaidi.

Soma Zaidi...
KUWAHI KUMALIZA TENDO LA NDOA MAPEMA: kumwaga mbegu mapema

Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika.

Soma Zaidi...
VYAKULA VYA KUONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA NA NGUVU ZA KIUME

Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.

Soma Zaidi...
Mimba kutoka kabla ya umri wake

Posti hii inahusu zaidi kuhusu kwa mimba kutoka kabla ya mda wake,ni kitendo ambacho mimba utoka kabla ya wiki ishilini na na nane.

Soma Zaidi...
Sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto mchanga kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, ni tatizo ambalo utokea kwa baadhi ya wajawazito kupata mtoto mwenye Uzito mkubwa, wengine uona kama ni sifa ila Kuna madhara yanaweza kujitokeza kwa Mama hasa wakati wa kujif

Soma Zaidi...