Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil

Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kutumia aina zote tano za vyakula kama vile vyakula vya wanga kwa kiasi kikubwa ili kuongeza nguvu kwa Mama, vyakula vya protini kwa wingi ili kujenga mwili, vyakula vya mafuta kwa kiwango kidogo, pia Mama anapaswa kutumia mboga mboga za majani na kunywa maji kwa wingi, anapaswa kunywa glasi nane au lita moja na nusu kila siku na pia Mama anapaswa kula vyakula vya wanyama kama vile maini na nyama kwa kufanya hivyo anaweza kumfanya mtoto akue vizuri.

 

2. Pia Mama anapaswa kula vyakula vyenye wingi wa vitamini C kama vile matunda mbalimbali yanayoweza kulinda mwili na kuzuia dhidi ya magonjwa ili kuongeza kiasi cha kuongeza kiasi cha damu mwilini na kuongeza madini ya chuma. Kwa hiyo tunajua kabisa mama mjamzito anapaswa kuwa na damu ya kutosha kwa hiyo mboga za majani ni lazima.

 

3. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana kutumia kahawa, soda na chai wakati wa kula chakula kwa sababu uingiliana na madini ya chuma yaliyomo mwilini na baadae mama anaweza kupata upungufu wa damu  na pia Mama mjamzito anapaswa kuachana na kunywa pombe kali  na yenyewe uingilia na madini ya chuma na kusababisha kuwepo kwa upungufu wa damu.

 

4. Pia Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa mbalimbali za hospitali ambazo uongeza damu kuzuia Malaria na kuzuia minyoo, dawa hizo ni kama  iron na folic acid, iron inapaswa kuwa na 200g ya ferrous sulphate, na 0.4 milligram of follic asidi. Na pia wajawazito wanapaswa kutumia calcium kuanzia 1.5 mpaka Mbili milligram, pia wanapaswa kutumia Mebendazole na sp, wanawake wajawazito wakifanya hivyo wataweza kuwa na damu ya kutosha na kuzuia mtoto dhidi ya Malaria na minyoo.

 

5. Pia wanawake wanapaswa kuachana na mila potofu ambazo ziko kwenye baadhi ya makabila kama vile kutotumia baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani, mayai na vyakula vinginevyo na pia wanawake wanapaswa kuachana na mila mbaya za kutotumia dawa za hospitali na baadae utumia dawa za nyumbani ili kuongeza uchungu, hizi dawa usababisha mtoto kukatika tumboni na baadae matatizo mbalimbali yanaweza kutokea kama vile kifo cha mama na mtoto.

 

6. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vyovyote wakati wa Mimba kama vile uvutaji wa sigara, matumizi ya madawa ya kulevya, kutumia pombe kali hali huu usababisha Mama kujifungua mtoto njiti au mara nyingine mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, kujifungua mtoto mfu na pengine kujifungua mtoto mwenye ulemavu, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa vileo vyovyote hasa vikali kwa Mama mjamzito ni hatari na usababisha kupata watoto wengi wenye matatizo mbalimbali.

 

7. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini, vyakula hivi ni kama vile matumizi ya pemba, udongo, mkaa na vitu mbalimbali kama hivyo iwapo Mama akijisikia kutumia vyakula vya hivyo anapaswa kwenda kuonana na mhudumu wa afya inawezekana ikawa ni kuwepo kwa minyoo au upungufu wa madini mwilini. Kwa hiyo jamii ijue kuwa vyakula vya hivi havina umuhimu wowote mwilini.

 

8. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa Mama mjamzito anapaswa kula mara nyingi iwapo kama chakula kipo na chakula hicho kinapaswa kuwa na toka au vya muhimu kama tulivyoona hapo awali, kwa hiyo jamii yenye imani potovu na kuwawekea wajawazito mda wa kula ambao ni mdogo wanakosea kwa sababu Mama asipopata chakula cha kutosha anaweza kujifungua mtoto mwenye kilo chini ya mbili na nusu kwa hiyo chakula ni muhimu kwa wajawazito .

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2339

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?

Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?

Soma Zaidi...
Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa maziwa wakati wa ujauzito.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa maziwa kwa akina Mama wakati wa ujauzito ni kawaida kwa sababu ya kuzaliwa kwa homoni ambayo usaidia kutoa maziwa.

Soma Zaidi...
Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.

Soma Zaidi...
Je kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?

Nimesoma makala yenu, sasa nina swaliJe kitunguu saumu kina madhara kwa Mgonjwa wa figo?

Soma Zaidi...
Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje

Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?

Soma Zaidi...