Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil
Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.
1. Mama mjamzito anapaswa kutumia aina zote tano za vyakula kama vile vyakula vya wanga kwa kiasi kikubwa ili kuongeza nguvu kwa Mama, vyakula vya protini kwa wingi ili kujenga mwili, vyakula vya mafuta kwa kiwango kidogo, pia Mama anapaswa kutumia mboga mboga za majani na kunywa maji kwa wingi, anapaswa kunywa glasi nane au lita moja na nusu kila siku na pia Mama anapaswa kula vyakula vya wanyama kama vile maini na nyama kwa kufanya hivyo anaweza kumfanya mtoto akue vizuri.
2. Pia Mama anapaswa kula vyakula vyenye wingi wa vitamini C kama vile matunda mbalimbali yanayoweza kulinda mwili na kuzuia dhidi ya magonjwa ili kuongeza kiasi cha kuongeza kiasi cha damu mwilini na kuongeza madini ya chuma. Kwa hiyo tunajua kabisa mama mjamzito anapaswa kuwa na damu ya kutosha kwa hiyo mboga za majani ni lazima.
3. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana kutumia kahawa, soda na chai wakati wa kula chakula kwa sababu uingiliana na madini ya chuma yaliyomo mwilini na baadae mama anaweza kupata upungufu wa damu na pia Mama mjamzito anapaswa kuachana na kunywa pombe kali na yenyewe uingilia na madini ya chuma na kusababisha kuwepo kwa upungufu wa damu.
4. Pia Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa mbalimbali za hospitali ambazo uongeza damu kuzuia Malaria na kuzuia minyoo, dawa hizo ni kama iron na folic acid, iron inapaswa kuwa na 200g ya ferrous sulphate, na 0.4 milligram of follic asidi. Na pia wajawazito wanapaswa kutumia calcium kuanzia 1.5 mpaka Mbili milligram, pia wanapaswa kutumia Mebendazole na sp, wanawake wajawazito wakifanya hivyo wataweza kuwa na damu ya kutosha na kuzuia mtoto dhidi ya Malaria na minyoo.
5. Pia wanawake wanapaswa kuachana na mila potofu ambazo ziko kwenye baadhi ya makabila kama vile kutotumia baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani, mayai na vyakula vinginevyo na pia wanawake wanapaswa kuachana na mila mbaya za kutotumia dawa za hospitali na baadae utumia dawa za nyumbani ili kuongeza uchungu, hizi dawa usababisha mtoto kukatika tumboni na baadae matatizo mbalimbali yanaweza kutokea kama vile kifo cha mama na mtoto.
6. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vyovyote wakati wa Mimba kama vile uvutaji wa sigara, matumizi ya madawa ya kulevya, kutumia pombe kali hali huu usababisha Mama kujifungua mtoto njiti au mara nyingine mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, kujifungua mtoto mfu na pengine kujifungua mtoto mwenye ulemavu, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa vileo vyovyote hasa vikali kwa Mama mjamzito ni hatari na usababisha kupata watoto wengi wenye matatizo mbalimbali.
7. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini, vyakula hivi ni kama vile matumizi ya pemba, udongo, mkaa na vitu mbalimbali kama hivyo iwapo Mama akijisikia kutumia vyakula vya hivyo anapaswa kwenda kuonana na mhudumu wa afya inawezekana ikawa ni kuwepo kwa minyoo au upungufu wa madini mwilini. Kwa hiyo jamii ijue kuwa vyakula vya hivi havina umuhimu wowote mwilini.
8. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa Mama mjamzito anapaswa kula mara nyingi iwapo kama chakula kipo na chakula hicho kinapaswa kuwa na toka au vya muhimu kama tulivyoona hapo awali, kwa hiyo jamii yenye imani potovu na kuwawekea wajawazito mda wa kula ambao ni mdogo wanakosea kwa sababu Mama asipopata chakula cha kutosha anaweza kujifungua mtoto mwenye kilo chini ya mbili na nusu kwa hiyo chakula ni muhimu kwa wajawazito .
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Soma Zaidi...Kipimo cha mimba cha mkojo hakiwezi kyonyesha mimva changa sana. Hivyo kama ni mimba baada ya wikibpima tena itaweza kuonekana. Dalili hizobulizotaja pekee haziashirii mimba tu huwenda ni homoni zimebadilika kidogo, ama una uti.
Soma Zaidi...In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by mi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.
Soma Zaidi...Inaweza kutokea ukapima mimbaikawa ipo, na baada ya wiki kadhaa unapima tena haipo. Hali hii unadhani inaweza kusababishwa na nini?
Soma Zaidi...Kipimo chamimba cha mkojo, huonyesha nestory miwili kuwa una mimba, na mmoja kuwa huna mimba. Sasa je ukitokea mmoja umekoleana mwingine hafifu? Endelea na pasti Γ’ΕΒΓ―ΒΈΒ hadi mwisho
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kuziba kwa mrija wa kizazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapian tube, ni sababu ambazo ufanya mirija ya follapian tube kuziba.
Soma Zaidi...Je, unafahamu dalili za mwanzo za ujauzito? Kutoka kwa kichefuchefu hadi uchovu, ujue nini cha kutarajia.
Soma Zaidi...