image

Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil

Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kutumia aina zote tano za vyakula kama vile vyakula vya wanga kwa kiasi kikubwa ili kuongeza nguvu kwa Mama, vyakula vya protini kwa wingi ili kujenga mwili, vyakula vya mafuta kwa kiwango kidogo, pia Mama anapaswa kutumia mboga mboga za majani na kunywa maji kwa wingi, anapaswa kunywa glasi nane au lita moja na nusu kila siku na pia Mama anapaswa kula vyakula vya wanyama kama vile maini na nyama kwa kufanya hivyo anaweza kumfanya mtoto akue vizuri.

 

2. Pia Mama anapaswa kula vyakula vyenye wingi wa vitamini C kama vile matunda mbalimbali yanayoweza kulinda mwili na kuzuia dhidi ya magonjwa ili kuongeza kiasi cha kuongeza kiasi cha damu mwilini na kuongeza madini ya chuma. Kwa hiyo tunajua kabisa mama mjamzito anapaswa kuwa na damu ya kutosha kwa hiyo mboga za majani ni lazima.

 

3. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana kutumia kahawa, soda na chai wakati wa kula chakula kwa sababu uingiliana na madini ya chuma yaliyomo mwilini na baadae mama anaweza kupata upungufu wa damu  na pia Mama mjamzito anapaswa kuachana na kunywa pombe kali  na yenyewe uingilia na madini ya chuma na kusababisha kuwepo kwa upungufu wa damu.

 

4. Pia Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa mbalimbali za hospitali ambazo uongeza damu kuzuia Malaria na kuzuia minyoo, dawa hizo ni kama  iron na folic acid, iron inapaswa kuwa na 200g ya ferrous sulphate, na 0.4 milligram of follic asidi. Na pia wajawazito wanapaswa kutumia calcium kuanzia 1.5 mpaka Mbili milligram, pia wanapaswa kutumia Mebendazole na sp, wanawake wajawazito wakifanya hivyo wataweza kuwa na damu ya kutosha na kuzuia mtoto dhidi ya Malaria na minyoo.

 

5. Pia wanawake wanapaswa kuachana na mila potofu ambazo ziko kwenye baadhi ya makabila kama vile kutotumia baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani, mayai na vyakula vinginevyo na pia wanawake wanapaswa kuachana na mila mbaya za kutotumia dawa za hospitali na baadae utumia dawa za nyumbani ili kuongeza uchungu, hizi dawa usababisha mtoto kukatika tumboni na baadae matatizo mbalimbali yanaweza kutokea kama vile kifo cha mama na mtoto.

 

6. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vyovyote wakati wa Mimba kama vile uvutaji wa sigara, matumizi ya madawa ya kulevya, kutumia pombe kali hali huu usababisha Mama kujifungua mtoto njiti au mara nyingine mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, kujifungua mtoto mfu na pengine kujifungua mtoto mwenye ulemavu, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa vileo vyovyote hasa vikali kwa Mama mjamzito ni hatari na usababisha kupata watoto wengi wenye matatizo mbalimbali.

 

7. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini, vyakula hivi ni kama vile matumizi ya pemba, udongo, mkaa na vitu mbalimbali kama hivyo iwapo Mama akijisikia kutumia vyakula vya hivyo anapaswa kwenda kuonana na mhudumu wa afya inawezekana ikawa ni kuwepo kwa minyoo au upungufu wa madini mwilini. Kwa hiyo jamii ijue kuwa vyakula vya hivi havina umuhimu wowote mwilini.

 

8. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa Mama mjamzito anapaswa kula mara nyingi iwapo kama chakula kipo na chakula hicho kinapaswa kuwa na toka au vya muhimu kama tulivyoona hapo awali, kwa hiyo jamii yenye imani potovu na kuwawekea wajawazito mda wa kula ambao ni mdogo wanakosea kwa sababu Mama asipopata chakula cha kutosha anaweza kujifungua mtoto mwenye kilo chini ya mbili na nusu kwa hiyo chakula ni muhimu kwa wajawazito .





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1777


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Umuhimu wa uzazi wa mpango
Uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na WA awake na wasichana Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji na kuepuka mimba zisizotarajiwa. Soma Zaidi...

Zijuwe Dalili za minyoo na dalili kuu 9 za minyoo
Utajifunza dalili za minyoo, sababu za minyoo na namna ya kujiepusha na minyoo. Dalili kuu 5 za minyoo mwilini Soma Zaidi...

Huduma kwa mtoto mwenye matatizo ya upumuaji
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa mtoto mwenye shida ya kupumua, mtoto kama ana shida ya kupumua tunaangalia dalili kwanza na baadaye tunaweza kutoa huduma kulingana na Dalili. Soma Zaidi...

utaratibu wa lishe kwa Mjamzito, Vyakula anavyopasa kula mjamzito
Ni vyakula gani anapasa kula mjamzito, na utaratibu mzima wa lishe kwa wajawazito Soma Zaidi...

Uzazi wa mpango
Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur Soma Zaidi...

Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi
Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi. Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya hedhi
Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine,  Soma Zaidi...

Mwanaune anapataje fangasi kwenye uume
Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake Soma Zaidi...

Samahani naomba kuhuliza je unaweza kutokwa na maji maji ambayoa ayana rangi Wala harufu Ni dalili gani kwa mimba ya mwezi mmoja
ukiwa na ujauzito unaweza kuona mabadiliko mengi katika mwili wako yakiwemo kutokwa na majimaji. je majimaji haya yana dalili gani kwenye ujauzito? Soma Zaidi...

Sababu za Mayai kushindwa kuzalishwa kwa mwanamke
Posti hii inahusu zaidi sababu za kushindwa kuzalishwa mayai kwa mwanamke, ni tatizo ambalo utokea kwa mwanamke ambapo mwanamke anashindwa kuzalisha mayai. Soma Zaidi...

Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa. Soma Zaidi...

DALILI ZA TEZI DUME
Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk Soma Zaidi...