Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil

Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kutumia aina zote tano za vyakula kama vile vyakula vya wanga kwa kiasi kikubwa ili kuongeza nguvu kwa Mama, vyakula vya protini kwa wingi ili kujenga mwili, vyakula vya mafuta kwa kiwango kidogo, pia Mama anapaswa kutumia mboga mboga za majani na kunywa maji kwa wingi, anapaswa kunywa glasi nane au lita moja na nusu kila siku na pia Mama anapaswa kula vyakula vya wanyama kama vile maini na nyama kwa kufanya hivyo anaweza kumfanya mtoto akue vizuri.

 

2. Pia Mama anapaswa kula vyakula vyenye wingi wa vitamini C kama vile matunda mbalimbali yanayoweza kulinda mwili na kuzuia dhidi ya magonjwa ili kuongeza kiasi cha kuongeza kiasi cha damu mwilini na kuongeza madini ya chuma. Kwa hiyo tunajua kabisa mama mjamzito anapaswa kuwa na damu ya kutosha kwa hiyo mboga za majani ni lazima.

 

3. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana kutumia kahawa, soda na chai wakati wa kula chakula kwa sababu uingiliana na madini ya chuma yaliyomo mwilini na baadae mama anaweza kupata upungufu wa damu  na pia Mama mjamzito anapaswa kuachana na kunywa pombe kali  na yenyewe uingilia na madini ya chuma na kusababisha kuwepo kwa upungufu wa damu.

 

4. Pia Mama wajawazito wanapaswa kutumia dawa mbalimbali za hospitali ambazo uongeza damu kuzuia Malaria na kuzuia minyoo, dawa hizo ni kama  iron na folic acid, iron inapaswa kuwa na 200g ya ferrous sulphate, na 0.4 milligram of follic asidi. Na pia wajawazito wanapaswa kutumia calcium kuanzia 1.5 mpaka Mbili milligram, pia wanapaswa kutumia Mebendazole na sp, wanawake wajawazito wakifanya hivyo wataweza kuwa na damu ya kutosha na kuzuia mtoto dhidi ya Malaria na minyoo.

 

5. Pia wanawake wanapaswa kuachana na mila potofu ambazo ziko kwenye baadhi ya makabila kama vile kutotumia baadhi ya vyakula kama vile mboga za majani, mayai na vyakula vinginevyo na pia wanawake wanapaswa kuachana na mila mbaya za kutotumia dawa za hospitali na baadae utumia dawa za nyumbani ili kuongeza uchungu, hizi dawa usababisha mtoto kukatika tumboni na baadae matatizo mbalimbali yanaweza kutokea kama vile kifo cha mama na mtoto.

 

6. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vileo vyovyote wakati wa Mimba kama vile uvutaji wa sigara, matumizi ya madawa ya kulevya, kutumia pombe kali hali huu usababisha Mama kujifungua mtoto njiti au mara nyingine mtoto kuzaliwa kabla ya wakati, kujifungua mtoto mfu na pengine kujifungua mtoto mwenye ulemavu, kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua kuwa vileo vyovyote hasa vikali kwa Mama mjamzito ni hatari na usababisha kupata watoto wengi wenye matatizo mbalimbali.

 

7. Pia Mama wajawazito wanapaswa kuachana na vyakula ambavyo havina faida yoyote mwilini, vyakula hivi ni kama vile matumizi ya pemba, udongo, mkaa na vitu mbalimbali kama hivyo iwapo Mama akijisikia kutumia vyakula vya hivyo anapaswa kwenda kuonana na mhudumu wa afya inawezekana ikawa ni kuwepo kwa minyoo au upungufu wa madini mwilini. Kwa hiyo jamii ijue kuwa vyakula vya hivi havina umuhimu wowote mwilini.

 

8. Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa Mama mjamzito anapaswa kula mara nyingi iwapo kama chakula kipo na chakula hicho kinapaswa kuwa na toka au vya muhimu kama tulivyoona hapo awali, kwa hiyo jamii yenye imani potovu na kuwawekea wajawazito mda wa kula ambao ni mdogo wanakosea kwa sababu Mama asipopata chakula cha kutosha anaweza kujifungua mtoto mwenye kilo chini ya mbili na nusu kwa hiyo chakula ni muhimu kwa wajawazito .

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2498

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Uzazi wa mpango

Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur

Soma Zaidi...
Zijue sababu za kutobeba mimba

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kupasuka kwa mfuko wa uzazi,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama ambaye anakuwa amepasuka mfuko wa kizazi.

Soma Zaidi...
Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUKOSA HAMU YA TENDO LANDOA

Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto.

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kondo la nyuma (placenta)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kupasuka kwa kondo la nyuma (plasenta) (abruptio placentae) ni tatizo lisilo la kawaida lakini kubwa la ujauzito.Kondo la nyuma (Placenta) ni muundo ambao hukua ndani ya uterasi wakati wa ujauzito ili kumlisha mtoto ana

Soma Zaidi...
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Soma Zaidi...