Fahamu kuhusu fangasi za ukeni
Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.
Fangasi za ukeni
1. Dalili ya kwanza ya kuwepo kwa fangasi za ukeni ni kukojoa mara kwa mara, kwa kawaida tunajua wazi ili mtu akojoe ni lazima awe amekunywa kimiminika chochote,ila kuna kipindi mtu anakojoa mara kwa mara bila kunywa chochote cha zaidi.
2. Mkojo kuwa na harufu mbaya.
Kwa kawaida mkojo huwa na harufu yake ya kawaida ila kuna kipindi mkojo unakuwa na harufu mbaya sana, kwa hiyo ni vizuri kuangalia tatizo mapema.
3. Maumivu ya misuli ya tumbo hasa chini ya kitovu.kuna wakati mwingine tumbo linauma hasa kitovuni ingawa inaweza kuwa ni Dalili ya magonjwa mbalimbali lakini ni vizuri kufanya uangalizi.
4. Maumivu ya kiuno.
Kwa sababu ya kusambaa kwa fangasi mara nyingi kunakuwepo na maumivu ya kiuno kwa hiyo ni vizuri kuangalia mapema ili kuweza kufahamu tatizo ni nini.
5. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu za siri.
Hii ni Dalili kubwa sana ambayo inatokea kwa walio wengi kwa sababu kuna kipindi mtu anawashwa sana kwenye sehemu za siri hasa hasa baada tu ya kukojoa.
6. Maumivu wakati wa kujamiiana.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na maumivu makali wakati wa kujamiiana, kwa sababu ya kuwepo kwa vidonda au majeraha yaliyosababishwa na fangasi kwa hiyo ni lazima maumivu kuwepo wakati wa tendo.
7. Kuwepo kwa vidonda ukenu.
Kwa sababu ya kuwepo kwa fangasi hasa wa mda mrefu usababisha vidonda ukeni na kusababisha mgonjwa awe anajikuna mara kwa mara.
8. Kuwepo kwa moto baada ya kujamiiana.
Kwa sababu ya kuwepo kwa fangasi usababisha kuwepo kwa moto baada ya kujamiiana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Aina za uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.
Soma Zaidi...Endapo nina dalili za mimba na nikipima sina mimba, je, tatizo ni nini?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Madhara ya fangasi ukeni.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi ukeni, madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa fangasi mapema.
Soma Zaidi...Nimegundua ni mjamzito na kibaya zaid namtoto mchanga nimefanyiwa opaleshen naomba ushauli wako mkuu
Inatakiwa angalau nafasivkati ya mtoto na mtoto wapishane miaka miwili.
Soma Zaidi...Huduma kwa wanaotoa damu yenye mabonge
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wanaotoa hedhi yenye mabonge, ni tatizo ambalo uwakumba wasichana hata wanawake wakati wa hedhi.
Soma Zaidi...Samahani nauliza mjamzito akiwa na presha140/90 Kuna madhara?
Presha ya kupanda hypertension huweza kuzumbuwa watu kwa jinsia zote, na umri wote. Wajawazito pia wamekuwa wakisumbuliwa na presha hii mara kwa mara.
Soma Zaidi...