WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)
Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri.
WATU WALIO HATARINI NA MALARIA
Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri. Lakini kuna watu endapo wakipata malaria inakuwa ni mbaya zaidi kwa afya yao binafsi ama na kwa ya watu wengine. Watu hao ni:-
Wajawazito: wajawazito ni katika watu ambao ni hatari sana kwao wakipata malaria. kwani inaweza ikahatarisha pia afya ya mtoto aliye tumboni. wajawazito wanashauriwa kulala kwenye chandarua tena kilichokuwa na dawa. hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata malaria.
Watoto wadogo chini ya miaka mitano, tafiti zinaonesha kuwa wanaofariki kwa ugonjwa wa malaria wengi wao ni watoto tena walio chini ya umri wa miaka 5. kundi hili la watu ndilo ambalo bado halijakuwa madhubuti kiafya kiasi cha kuweza kupambana na athari za malaria. hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa watoto siku zote wanalala kwenye chandarua chenye dawa.
Wazee; kundi jingine linaloathiriwa na malaria ni hili kundi la wazee. afya za wazee hazipo imara sana ukilinganisha na afya za vijana. huenda ni kwa sababu miili yao haipo active muda wowote, huenda kwa sababu wazee wengi hawana kawaida ya kufanya mazoezi ya hapa na pale.
Watu wanaotoka ameneo yasiyo na malaria, kundi la mwisho linawahusu sana wageni ambao wametoka katika maeneo yasiyo na mbu ama yasiyo na ugonjwa huu. watu hawa miili yao haina mazoea na ugo njwa huu hivyo hakuna walinzi walio tayari kwa ajili ya kupunguza athari za malaria.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 ai web app 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 web hosting 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Ugonjwa wa kisukari ambao husababisha kupoteza fahamu ( coma ya kisukari)..
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kisukari unaopelekea kukosa fahamu ni tatizo linalohatarisha maisha kisukari ambalo husababisha kupoteza fahamu. Ikiwa una kisukari, sukari ya juu ya damu (hyperglycemia) au sukari iliyopungua sana (hypoglyc
Soma Zaidi...Je vidonda vya tumbo husababisha maumivu mpka upande mmoja wa mgongoni !?
Ni ngumu kujuwa vidonda vya tumbo uhakika wake bila ya kupata vipimo. Unajuwa ni kwa nini, ni kwa sababu maumivu ya tumbo ni dalili ya shida nyingi za kiafya kama ujauzito, mimba, typhod, na shida kwenye unfumo wa chakula.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutofautisha maumivu ya kichwa cha kawaida na ya malaria.
Maumivu ya kichwa ni tatizo la kawaida linaloweza kusababishwa na mambo mengi, kuanzia uchovu, njaa, hadi magonjwa kama malaria. Kwa kuwa malaria ni ugonjwa unaoweza kuwa hatari ndani ya muda mfupi, ni muhimu kujua jinsi ya kutofautisha maumivu ya kichwa ya kawaida na yale yanayoashiria maambukizi ya vimelea vya malaria. Makala haya yanakupa mwongozo wa dalili za msingi ili uweze kuchukua hatua sahihi za kiafya.
Soma Zaidi...Ujuwevmv ugonjwa Nimonia na dalili zake
Nimonia ni Hali ya kuvimba pafu inayoathiri hasa vifuko vya hewa viitwavyo Alveoli, husababishwa na Maambukizi ya virusi
Soma Zaidi...Upungufu wa damu (Anemia): Dalili na vyakula vya kuongeza damu.
Upungufu wa damu (Anemia) ni changamoto kubwa ya afya ya jamii duniani inayotokea pale mwili unapokosa seli nyekundu za damu au protini ya hemoglobin ya kutosha kusafirisha oksijeni. Makala haya ya kitaalamu yanachambua kwa kina dalili za kliniki za anemia, makundi yaliyo katika hatari kubwa, na namna ya kukabili tatizo hili kupitia lishe. Muundo maalum wa makala haya unalenga kutoa mwongozo wa vyakula vyenye madini ya chuma ya Heme na Non-Heme, nafasi ya Vitamini C katika ufyonzwaji wa virutubisho, na mbinu za kuzuia anemia kwa mujibu wa miongozo ya kisayansi ya Shirika la Afya Duniani (WHO).
Soma Zaidi...Dalili zinazoonyesha joto la kupungua mwilini (hypothermia)
joto la mwili wako linapungua, moyo wako, mfumo wa neva na viungo vingine haviwezi kufanya kazi kwa kawaida. Isipopotibiwa, Hypothermia hatimaye inaweza kusababisha moyo wako na mfumo wa upumuaji kushindwa kabisa na hata kifo.
Soma Zaidi...