picha

WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)

Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri.

WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)

WATU WALIO HATARINI NA MALARIA

Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri. Lakini kuna watu endapo wakipata malaria inakuwa ni mbaya zaidi kwa afya yao binafsi ama na kwa ya watu wengine. Watu hao ni:-

 

Wajawazito: wajawazito ni katika watu ambao ni hatari sana kwao wakipata malaria. kwani inaweza ikahatarisha pia afya ya mtoto aliye tumboni. wajawazito wanashauriwa kulala kwenye chandarua tena kilichokuwa na dawa. hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata malaria.

 

Watoto wadogo chini ya miaka mitano, tafiti zinaonesha kuwa wanaofariki kwa ugonjwa wa malaria wengi wao ni watoto tena walio chini ya umri wa miaka 5. kundi hili la watu ndilo ambalo bado halijakuwa madhubuti kiafya kiasi cha kuweza kupambana na athari za malaria. hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa watoto siku zote wanalala kwenye chandarua chenye dawa.

 

Wazee; kundi jingine linaloathiriwa na malaria ni hili kundi la wazee. afya za wazee hazipo imara sana ukilinganisha na afya za vijana. huenda ni kwa sababu miili yao haipo active muda wowote, huenda kwa sababu wazee wengi hawana kawaida ya kufanya mazoezi ya hapa na pale.


Watu wanaotoka ameneo yasiyo na malaria, kundi la mwisho linawahusu sana wageni ambao wametoka katika maeneo yasiyo na mbu ama yasiyo na ugonjwa huu. watu hawa miili yao haina mazoea na ugo njwa huu hivyo hakuna walinzi walio tayari kwa ajili ya kupunguza athari za malaria.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2234

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰3 web hosting     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Sababu za mngurumo wa moyo

Mngurumo wa moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako. Sauti hizi zinaweza kusikika na kifaa kinachojulikana kama stethoscope. Mapigo ya moyo ya kawaida

Soma Zaidi...
Athari za mabadiliko ya misimu (Seasonal Affective Disorder).

Seasonal Affective Disorder (SAD)β€”aina ya sonona inayochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa na misimu. Makala haya yanachambua dalili zake, sababu za kisayansi, na jinsi ya kukabiliana nayo ili ubaki na furaha na utulivu mwaka mzima.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster

Soma Zaidi...
Namna Ugonjwa wa UKIMWI unavyoambukizwa.

UKIMWI (acquired immunodeficiency syndrome) ni hali ya kudumu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya ukimwi (VVU) Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako wa kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Inawe

Soma Zaidi...
Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?

Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu

Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.

Soma Zaidi...