picha

WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)

Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri.

WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)

WATU WALIO HATARINI NA MALARIA

Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri. Lakini kuna watu endapo wakipata malaria inakuwa ni mbaya zaidi kwa afya yao binafsi ama na kwa ya watu wengine. Watu hao ni:-

 

Wajawazito: wajawazito ni katika watu ambao ni hatari sana kwao wakipata malaria. kwani inaweza ikahatarisha pia afya ya mtoto aliye tumboni. wajawazito wanashauriwa kulala kwenye chandarua tena kilichokuwa na dawa. hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata malaria.

 

Watoto wadogo chini ya miaka mitano, tafiti zinaonesha kuwa wanaofariki kwa ugonjwa wa malaria wengi wao ni watoto tena walio chini ya umri wa miaka 5. kundi hili la watu ndilo ambalo bado halijakuwa madhubuti kiafya kiasi cha kuweza kupambana na athari za malaria. hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa watoto siku zote wanalala kwenye chandarua chenye dawa.

 

Wazee; kundi jingine linaloathiriwa na malaria ni hili kundi la wazee. afya za wazee hazipo imara sana ukilinganisha na afya za vijana. huenda ni kwa sababu miili yao haipo active muda wowote, huenda kwa sababu wazee wengi hawana kawaida ya kufanya mazoezi ya hapa na pale.


Watu wanaotoka ameneo yasiyo na malaria, kundi la mwisho linawahusu sana wageni ambao wametoka katika maeneo yasiyo na mbu ama yasiyo na ugonjwa huu. watu hawa miili yao haina mazoea na ugo njwa huu hivyo hakuna walinzi walio tayari kwa ajili ya kupunguza athari za malaria.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1869

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 web hosting     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 ai web app     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.

Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.

Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
DALILI ZA SELIMUDU

Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos

Soma Zaidi...
Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI

Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.

Soma Zaidi...
Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo

Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

Soma Zaidi...