WATU WALIO HATARINI KWA UGONJWA WA MALARIA (wazee, watoto, wajawazito, wageni n.k)
Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri.
WATU WALIO HATARINI NA MALARIA
Malaria inaweza kumpata mtu yeyote bila ya kujali mri. Lakini kuna watu endapo wakipata malaria inakuwa ni mbaya zaidi kwa afya yao binafsi ama na kwa ya watu wengine. Watu hao ni:-
Wajawazito: wajawazito ni katika watu ambao ni hatari sana kwao wakipata malaria. kwani inaweza ikahatarisha pia afya ya mtoto aliye tumboni. wajawazito wanashauriwa kulala kwenye chandarua tena kilichokuwa na dawa. hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata malaria.
Watoto wadogo chini ya miaka mitano, tafiti zinaonesha kuwa wanaofariki kwa ugonjwa wa malaria wengi wao ni watoto tena walio chini ya umri wa miaka 5. kundi hili la watu ndilo ambalo bado halijakuwa madhubuti kiafya kiasi cha kuweza kupambana na athari za malaria. hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa watoto siku zote wanalala kwenye chandarua chenye dawa.
Wazee; kundi jingine linaloathiriwa na malaria ni hili kundi la wazee. afya za wazee hazipo imara sana ukilinganisha na afya za vijana. huenda ni kwa sababu miili yao haipo active muda wowote, huenda kwa sababu wazee wengi hawana kawaida ya kufanya mazoezi ya hapa na pale.
Watu wanaotoka ameneo yasiyo na malaria, kundi la mwisho linawahusu sana wageni ambao wametoka katika maeneo yasiyo na mbu ama yasiyo na ugonjwa huu. watu hawa miili yao haina mazoea na ugo njwa huu hivyo hakuna walinzi walio tayari kwa ajili ya kupunguza athari za malaria.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Njia za kuzuia upele
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika.
Soma Zaidi...Homoni za uzazi: Kazi ya Estrogen na Progesterone.
Makala haya yanachunguza kwa kina dhima muhimu za homoni za estrogen na progesterone katika mfumo wa uzazi wa mwanamke. Tutachambua jinsi homoni hizi zinavyoshirikiana kudhibiti mzunguko wa hedhi, kurutubisha yai, na kudumisha ujauzito, pamoja na athari zake katika afya ya mifupa na mfumo wa moyo na mishipa.
Soma Zaidi...Dalili za VVU/UKIMWI Ni zipi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu maambukizi chini ya kitovu ni madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mgonjwa pale ambapo matibabu yanapokuwa hayatolewi kwa mgonjwa wa maumivu chini ya kitovu.
Soma Zaidi...DALILI ZA SELIMUDU
Posti hii inazungumzia ishara na dalili za SELIMUDU ambao kitaalamu huitwa Sickle cell Anemia.selimudu ni aina ya kurithi ya Anemia — hali ambayo hakuna chembechembe nyekundu za damu zenye afya za kutosha kubeba oksijeni ya kutos
Soma Zaidi...Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcer): Chanzo na vyakula vya kuepuka.
Vidonda vya tumbo ni vidonda wazi vinavyojitokeza kwenye utando wa ndani wa tumbo (gastric ulcers) au sehemu ya juu ya utumbo mdogo (duodenal ulcers). Hali hii hutokea wakati kinga ya utando wa tumbo dhidi ya asidi inapovunjika, na kusababisha maumivu makali, kiungulia, na kichefuchefu. Makala haya yanalenga kukupa uelewa wa chanzo cha vidonda hivi na orodha ya vyakula unavyopaswa kuviepuka ili kusaidia uponyaji wa kidonda na kupunguza maumivu.
Soma Zaidi...