Dalili na Ishara za mawe kwenye figo

Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako.

DALILI ZA MAWE KWENYE FIGO

 Jiwe kwenye figo huenda lisisababishe dalili hadi lisogee ndani ya figo yako au lipite kwenye  mrija unaounganisha figo na kibofu.  Wakati huo huo, unaweza kupata ishara na dalili zifuatazo:

 

1. Maumivu makali upande na nyuma na chini ya mbavu

2. Maumivu ambayo huenea kwenye tumbo la chini.

3. Maumivu wakati wa kukojoa

4. Mkojo wa pink, nyekundu au kahawia

5. Mkojo wenye  harufu mbaya.

6. Kichefuchefu na kutapika.

7. Haja ya kudumu ya kukojoa.

8. Kukojoa mara nyingi zaidi kuliko kawaida.

9. Homa na baridi ikiwa kuna maambukizi.

10. Kukojoa kiasi kidogo cha mkojo.

 

MAMBO YA HATARI YANAYOSABABISHA MAWE KWENYE FIGO

 Mambo yanayoongeza hatari ya kupata mawe kwenye figo ni pamoja na:

1. Historia ya familia au ya kibinafsi.  Ikiwa mtu katika familia yako ana mawe kwenye figo, kuna uwezekano mkubwa wa kupata mawe pia.  Na ikiwa tayari una mawe kwenye figo moja au zaidi, uko kwenye hatari kubwa ya kuendeleza nyingine.

 

2. Upungufu wa maji mwilini.  Kutokunywa maji ya kutosha kila siku kunaweza kuongeza hatari ya kupata mawe kwenye figo.  Watu wanaoishi katika hali ya hewa ya joto na wale wanaotoka jasho nyingi wanaweza kuwa katika hatari zaidi kuliko wengine.

 

3. Mlo (chakula). Kula lishe iliyo na protini nyingi, sodiamu na sukari kunaweza kuongeza hatari yako ya kupata aina fulani za mawe kwenye figo kutokana na aina ya vyakula ambavyo vinatumiwa.

 

4. Kuwa mnene.  Kiwango cha juu cha uzito wa mwili, ukubwa wa kiuno kikubwa na kuongezeka kwa uzito vimehusishwa na hatari ya kuongezeka kwa mawe kwenye figo.

 

5. Magonjwa ya njia ya utumbo na upasuaji.  ugonjwa wa uvimbe wa matumbo au Kuhara mara kwa mara unaweza kusababisha mabadiliko katika usagaji chakula na kuathiri ufyonzwaji wako wa maji, na hivyo kuongeza viwango vya vitu vinavyotengeneza mawe kwenye mkojo wako.

 

6. Hali zingine za kiafya.  Magonjwa na hali ambazo zinaweza kuongeza hatari yako ya kupata mawe kwenye figo. dawa fulani na baadhi ya maambukizi ya mfumo wa mkojo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2425

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni.

Soma Zaidi...
Njia za kupambana na fangasi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na fangasi

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...
NINI CHANZO CHA UGONJWA WA MALARIA? NI YUPI MBU ANAYESAMBAZA MALARIA

Malaria husababishwa na vimelea (parasite) ambavyo husambazwa ama kubebwa na mbu aina ya anopheles.

Soma Zaidi...
Fahamu Dalili za Ugonjwa wa Bawasiri

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Bawasiri. Bawasiri ni mishipa iliyovimba kwenye njia yako ya haja kubwa na sehemu ya chini ya puru. Bawasiri inaweza kutokana na kukaza mwendo wakati wa kwenda haja ndogo au kutokana na shinikizo la kuongeze

Soma Zaidi...
Fahamu sababu za ugonjwa unanipeleka Kuvimba kwa mishipa ya Damu

posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa ya damu katika mwili wako wote. Kuvimba kwa Mishipa ya Damu hujulikana Kama Behcet amboyo husababisha dalili nyingi ambazo hapo awali zinaweza kuonekana kuwa hazihusiani. Dalili na ish

Soma Zaidi...
Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za michubuko

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa UTI

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
Fangasi aina ya Candida

Huu ni ugonjwa wa fangasi wanaosababishwa na mashambulizi ya fangani aia ya yeast waitwao candida.

Soma Zaidi...