picha

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA

Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOKUTIBU MALARIA

Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo. Lakini kabla ya kutokea kifo malaria huanza kwa kuathiri maeneo nyeti sana ya kiafya na hivyo hupelekea athari kubwa ambazo huleta kifo. Hebu tuone maeneo ambayo malaria hushambulia:-

 

Ubongo, vimjidudud vya malaria vinapoingia kwenye mfumo wa damu huanza kushambulia seli hai nyekundu za damu. Kupitia damu vijidudu hivi vinaweza kuingia kwenye ubongo na kusababisha kuziba kwa vimishipa vijidogo ndani ya upongo. Vimishipa hivi ndivyo hupeleka virutubisho na hewa kwenye ubongo. Hali hii inaweza kumfanya mgonjwa achanganyikie na kupoteza fahamu kabisa.

 

Ini na figo, vijidudu hivi vinaweza kusababisha ini na figo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi, ama tena kufa kabisa. Endapo hali hii ikitikea basi itakuwa ni athari kubwa sana katika afya ya mtu husika.

 

Mapafu, endapo malaria haitatibiwa na ikiendelea kuwepo mwilini inaweza kusababisha kujaa kwa majimaji kwenye mapafu. Hali hii inaweza kusbabisha mgonjwa kushindwa kupumua kwa ufanisi. Endapo hili litatokea itakuwa ni katika athari mbaya sana za malaria.

 

Damu, kwakuwa vijidudu hivi hushabulia seli hai nyekundu za damu, na seli hizi ndizo hubeba hewa ya oksijeni na kuisambaza mwilini. Hivyo malaria inaweza kusababisha upungufu wa hewa ya oksijeni mwlini na kusababisha ugonjwa unaotambulika kama anaemia.

 

Wakati mwingine malaria inaweza kuwa kali zaidi na kusababisha sukari kushuka, hali hii kitaalamu inajulukana kama hypoglycaemia. Na ni katika hali mbaya sana kwani mgonjwa anaweza kupoteza fahamu.

 



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2668

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...
Kuungulia kwa moyo (Heartburn): Chanzo na njia za kupunguza.

Kuungulia kwa moyoβ€”hali ile ya kuhisi moto au maumivu yanayotokea nyuma ya mfupa wa katikati ya kifuaβ€”ni tatizo linalowasumbua watu wengi. Licha ya jina lake, tatizo hili halina uhusiano wowote na moyo; linahusu mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Makala haya yanakupa mwongozo wa kile kinachosababisha hali hii na hatua unazoweza kuchukua ili kupata nafuu.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Maandalizi ya kisaikolojia na kimwili kabla ya kubeba mimba.

Kupanga kupata mtoto ni uamuzi mkubwa na wa furaha katika maisha ya mtu. Hata hivyo, safari hii haihitaji tu matamanio, bali inahitaji maandalizi ya kina. Makala hii inaangazia misingi ya kujiandaa kisaikolojia na kimwili ili kuhakikisha afya ya mama na mtoto, na kuimarisha utayari wa kuwa mzazi katika kipindi chote cha ujauzito

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 13: Faida za bamia

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za bamia mwilini

Soma Zaidi...
ujuwe ugonjwa wa gout na athari zake mwilini

Post hii itakwenda kuzungumzia ugonjwa wa gout unaosababishwa na ongezeko la asidi mwilini.

Soma Zaidi...