ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA

Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOKUTIBU MALARIA

Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo. Lakini kabla ya kutokea kifo malaria huanza kwa kuathiri maeneo nyeti sana ya kiafya na hivyo hupelekea athari kubwa ambazo huleta kifo. Hebu tuone maeneo ambayo malaria hushambulia:-

 

Ubongo, vimjidudud vya malaria vinapoingia kwenye mfumo wa damu huanza kushambulia seli hai nyekundu za damu. Kupitia damu vijidudu hivi vinaweza kuingia kwenye ubongo na kusababisha kuziba kwa vimishipa vijidogo ndani ya upongo. Vimishipa hivi ndivyo hupeleka virutubisho na hewa kwenye ubongo. Hali hii inaweza kumfanya mgonjwa achanganyikie na kupoteza fahamu kabisa.

 

Ini na figo, vijidudu hivi vinaweza kusababisha ini na figo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi, ama tena kufa kabisa. Endapo hali hii ikitikea basi itakuwa ni athari kubwa sana katika afya ya mtu husika.

 

Mapafu, endapo malaria haitatibiwa na ikiendelea kuwepo mwilini inaweza kusababisha kujaa kwa majimaji kwenye mapafu. Hali hii inaweza kusbabisha mgonjwa kushindwa kupumua kwa ufanisi. Endapo hili litatokea itakuwa ni katika athari mbaya sana za malaria.

 

Damu, kwakuwa vijidudu hivi hushabulia seli hai nyekundu za damu, na seli hizi ndizo hubeba hewa ya oksijeni na kuisambaza mwilini. Hivyo malaria inaweza kusababisha upungufu wa hewa ya oksijeni mwlini na kusababisha ugonjwa unaotambulika kama anaemia.

 

Wakati mwingine malaria inaweza kuwa kali zaidi na kusababisha sukari kushuka, hali hii kitaalamu inajulukana kama hypoglycaemia. Na ni katika hali mbaya sana kwani mgonjwa anaweza kupoteza fahamu.

 



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1450

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

MATIBABU YA FANGASI

Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi.

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza makali ya pressure au shinikizo la damu

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kupunguza ugonjwa wa pressure au shinikizo la damu kwa waliokwisha kupata wanaweza kupunguza na kwa wake ambao hawajapata ni nzuri inawasaidia kuepuka hatari ya kupata ppresha.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya watu walio hatarini kupata fangasi

Soma Zaidi...
Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao

Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.

Soma Zaidi...
Kuona damu kwenye mkojo

Kuona damu kwenye mkojo kunaweza kusababisha wasiwasi. Ingawa katika hali nyingi kuna sababu zisizofaa, Damu kwenye mkojo (hematuria) pia inaweza kuonyesha ugonjwa mbaya.

Soma Zaidi...
Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi

Kubana kwa kifuwa ni katika hali ambazo si naweza kuhatarisha maisha. Huwenda kuwa ni miongoni mwa dalili za magonjwa mengi. Je unadhani na HIv na UKIMWI ni moja ya magonjwa hayo?

Soma Zaidi...
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia

Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...
Madhara ya minyoo

Somo hili linakwenda kukuletea madhara ya minyoo

Soma Zaidi...
Typhoid husabisha mwili kuchoka na maumivu ya kichwa pamoja na joint za miguu kuchoka

Dalili za typhid zinapasa kuangaliwa kwa umakini. Bila vipimo mtu asitumie dawa za tyohod, kwanu dalili za tyohid hufanana na daliki za maradhi mengi.

Soma Zaidi...