NJIA ZA KUJIKINGA NA MALARIA (zijue njia za kupambana na mbu wa malaria)
KUJIKINGA NA MALARIA
Kwa kuwa mbu wanaosambaza malaria wanang’ata usiku sana ama alfajiri, hivyo tunaweza kujikinga na malaria kwa :-
Kulala kwenye chandarua, ni vyema kikatiwa dawa. pia ni vyema ukahakikisha kuwa chandarua hakina matundu yaani kiwe kizima. ha hakikisha unawatoa mbu kwenye chandarua kama wapo kisha ndipo ujiandae kulala.
Kupaka losheni ya mbu; hiki ni losheni ambazo zina harufu mbaya ambayo inawakera mbu. harufu hiki huweza kutofautiana. kuna nyingine ni kali na nyengine ni kawaida. kuna nyingine utapenda harufu zao na nyingine hutapenda. watu wengine wakipaka losheni hizi huwashwa hususani wanapopaka usoni. hakikisha haupaki mdomoni kiasi kwamba unaweza kuila losheni kwa bahati mbaya.
Kuvaa nguo ndefu zinazoziba viungo; nguo hizi zisiwe ndefu tu bali ziwe nzito kiasi kwamba zinaweza kuzuia mbu kuifikia ngozi yako. ni vyea zikafunika mikono na miguu, na maeneo mengine ambayo yanashambuliwa na mbu kama shingo.
Kutumia dawa za mbu; dawa hizi zipo za kupulizia kama pafyumu na zipo za kuchoma. unaweza kutumia za kupulizia wakati hupo ndani kwa muda wa dakika kama 30. dawa za kuchoma nazo pia ni vyema ukachoma ukiwa umetoka kisha baada ya dakika 30 kisha ingia ndani.
Fyeka vichaka, punguza nyasi na fukia madimbwi yaliyo karibu na nyumba. hakikisha hakuna makopo, vifuu ama chochote kinachoweka maji. hii itasaidia kupambana na mazalia ya mbu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 ai web app 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...Sababu za mdomo kuwa mchungu
Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.
Soma Zaidi...Fahamu ugonjwa wa Varicose vein
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa vericose veini, hili ni tatizo ambalo utokea katika mzunguko wa damu hasa kwenye miguu.
Soma Zaidi...Dalili za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi dalili za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu, ni dalili ambazo zinaweza kujitokeza Kwa mgonjwa,Kwa hiyo baada ya kuona dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospital mara moja Kwa ajili ya matibabu.
Soma Zaidi...Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitomvu kwa wanawake na wanaumr?
Makala hii inakwenda kukuletea somo linalozungumzia maumivu ya tumbo chini ya kitomvu. Ni katika maumivu amaboyo kwa wanaume mara nyingi huhusishwa an ngiri na kwa upande wa wanawake huhusishwa na chango hasa pale wanapokaribia kuingia katika siku zao. Ma
Soma Zaidi...