picha

NJIA ZA KUJIKINGA NA MALARIA (zijue njia za kupambana na mbu wa malaria)

NJIA ZA KUJIKINGA NA MALARIA (zijue njia za kupambana na mbu wa malaria)

KUJIKINGA NA MALARIA

 

Kwa kuwa mbu wanaosambaza malaria wanang’ata usiku sana ama alfajiri, hivyo tunaweza kujikinga na malaria kwa :-
Kulala kwenye chandarua, ni vyema kikatiwa dawa. pia ni vyema ukahakikisha kuwa chandarua hakina matundu yaani kiwe kizima. ha hakikisha unawatoa mbu kwenye chandarua kama wapo kisha ndipo ujiandae kulala.

 

Kupaka losheni ya mbu; hiki ni losheni ambazo zina harufu mbaya ambayo inawakera mbu. harufu hiki huweza kutofautiana. kuna nyingine ni kali na nyengine ni kawaida. kuna nyingine utapenda harufu zao na nyingine hutapenda. watu wengine wakipaka losheni hizi huwashwa hususani wanapopaka usoni. hakikisha haupaki mdomoni kiasi kwamba unaweza kuila losheni kwa bahati mbaya.

 

Kuvaa nguo ndefu zinazoziba viungo; nguo hizi zisiwe ndefu tu bali ziwe nzito kiasi kwamba zinaweza kuzuia mbu kuifikia ngozi yako. ni vyea zikafunika mikono na miguu, na maeneo mengine ambayo yanashambuliwa na mbu kama shingo.

 

Kutumia dawa za mbu; dawa hizi zipo za kupulizia kama pafyumu na zipo za kuchoma. unaweza kutumia za kupulizia wakati hupo ndani kwa muda wa dakika kama 30. dawa za kuchoma nazo pia ni vyema ukachoma ukiwa umetoka kisha baada ya dakika 30 kisha ingia ndani.

 

Fyeka vichaka, punguza nyasi na fukia madimbwi yaliyo karibu na nyumba. hakikisha hakuna makopo, vifuu ama chochote kinachoweka maji. hii itasaidia kupambana na mazalia ya mbu.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4150

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Dalili za saratani ya kwenye Njia ya haja kubwa.

Saratani ya kwenye Njia ya haja kubwa ni aina isiyo ya kawaida ambayo kitaalamu hujulikana Kama saratani ya mkundu.Mfereji wa mkundu ni mirija fupi iliyo mwisho wa puru yako ambayo kinyesi hutoka mwilini mwako. Saratani ya kwenye Njia ya  ha

Soma Zaidi...
Kumsaidia sliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo

Posti hii inahusu namna ya kumsaidia mgonjwa aliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo.

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuungua Mdomo (mouth burning syndrome)

Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuwaka moto mara kwa mara mdomoni bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea ya mdomo wako wot

Soma Zaidi...
Kukosa choo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kukosa choo

Soma Zaidi...
Fahamu mapacha wanavyounganishwa.

Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa vijusi viwili vitakua kutoka kwa kiinitete hiki, wataendelea kushikamana mar

Soma Zaidi...