NJIA ZA KUJIKINGA NA MALARIA (zijue njia za kupambana na mbu wa malaria)
KUJIKINGA NA MALARIA
Kwa kuwa mbu wanaosambaza malaria wanang’ata usiku sana ama alfajiri, hivyo tunaweza kujikinga na malaria kwa :-
Kulala kwenye chandarua, ni vyema kikatiwa dawa. pia ni vyema ukahakikisha kuwa chandarua hakina matundu yaani kiwe kizima. ha hakikisha unawatoa mbu kwenye chandarua kama wapo kisha ndipo ujiandae kulala.
Kupaka losheni ya mbu; hiki ni losheni ambazo zina harufu mbaya ambayo inawakera mbu. harufu hiki huweza kutofautiana. kuna nyingine ni kali na nyengine ni kawaida. kuna nyingine utapenda harufu zao na nyingine hutapenda. watu wengine wakipaka losheni hizi huwashwa hususani wanapopaka usoni. hakikisha haupaki mdomoni kiasi kwamba unaweza kuila losheni kwa bahati mbaya.
Kuvaa nguo ndefu zinazoziba viungo; nguo hizi zisiwe ndefu tu bali ziwe nzito kiasi kwamba zinaweza kuzuia mbu kuifikia ngozi yako. ni vyea zikafunika mikono na miguu, na maeneo mengine ambayo yanashambuliwa na mbu kama shingo.
Kutumia dawa za mbu; dawa hizi zipo za kupulizia kama pafyumu na zipo za kuchoma. unaweza kutumia za kupulizia wakati hupo ndani kwa muda wa dakika kama 30. dawa za kuchoma nazo pia ni vyema ukachoma ukiwa umetoka kisha baada ya dakika 30 kisha ingia ndani.
Fyeka vichaka, punguza nyasi na fukia madimbwi yaliyo karibu na nyumba. hakikisha hakuna makopo, vifuu ama chochote kinachoweka maji. hii itasaidia kupambana na mazalia ya mbu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 ai web app 👉3 web hosting 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Dalili za Saratani ya figo.
Saratani ya Figo ni Saratani ambayo huanzia kwenye figo. Figo zako ni viungo viwili vyenye umbo la maharagwe, kila kimoja kikiwa na ukubwa wa ngumi yako. Ziko nyuma ya viungo vyako vya tumbo, na figo moja kila upande wa mgongo wako.
Soma Zaidi...UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles.
Soma Zaidi...Maumivu ya kifua: Je, yanaweza kuwa ishara ya ugonjwa wa moyo?
Maumivu ya kifua ni dalili inayopaswa kuchukuliwa kwa uzito mkubwa kila wakati. Ingawa si kila maumivu ya kifua yanamaanisha ugonjwa wa moyo—kwani yanaweza kusababishwa na matatizo ya mmeng'enyo wa chakula, misuli, au mapafu—ni vigumu sana kwa mtu wa kawaida kutofautisha kati ya maumivu ya kawaida na yale yanayoashiria dharura ya moyo. Makala haya yanalenga kukupa elimu kuhusu dalili hatari, sababu nyingine za maumivu, na wakati sahihi wa kutafuta msaada wa kitabibu wa haraka.
Soma Zaidi...Matumizi ya chumvi nyingi: Hatari kwa afya ya moyo.
Katika ulimwengu wa kisasa, mtindo wa maisha na vyakula vilivyosindikwa vimesababisha ongezeko kubwa la ulaji wa chumvi kupita kiasi. Makala hii inachunguza uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa sodiamu na magonjwa ya moyo. Tutajadili jinsi chumvi inavyoathiri shinikizo la damu, utaratibu wa uharibifu wa mishipa ya damu, na hatua za kivitendo unazoweza kuchukua ili kupunguza matumizi yake kwa maisha bora na marefu.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuondokana na mawazo hasi na kujenga tabasamu.
Je, unatatizika na mawazo hasi yanayokwamisha maendeleo yako? Jifunze mbinu za kitaalamu za kubadilisha mtazamo, kuondoa msongo wa mawazo, na kujenga tabasamu la kudumu kwa ajili ya maisha yenye furaha na tija.
Soma Zaidi...Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo
HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu.
Soma Zaidi...