Homa ya manjano, dalili za homa ya manjano na namna ya kujikinga na homa ya manjano

HOMA YA MANJANO (yellow fever)Homa ya manjano ni maradhi yanayosababishwa na virusi na husambazwa na mbu.

Homa ya manjano, dalili za homa ya manjano na namna ya kujikinga na homa ya manjano

HOMA YA MANJANO (yellow fever)
Homa ya manjano ni maradhi yanayosababishwa na virusi na husambazwa na mbu. Homa hii ipo sana nchi za Afrika na Amerika ya Kusini. Kwa hali ya kawaida homa ya manjano huweza kusababisha homa, maumivu ya kichwa, kichefuchefu na kutapika. Pia homa ya manjano inaweza kuwa mbaya zaidi na kupelekea matatizo kwenye ini, figo na moyo pamoja na kutoka kwa damu yali inayotambulika kitaalamu kama hemorrhaging.



Inakadiriwa kuwa asilimia 50 ya wanaopata homa ya manjano wanafariki kwa maradhi maradhi haya. Tafiti zinaonyesha kuwa mpaka sasa hakuna tiba maalumu ya homa ya manjano, ila ipo chanjo kwa ajili ya kujikinga na virusi wanaosababisha homa hii.



Tafiti zinaonesha kuwa baada ya kung’atwa na mbu na kukuachia virusi hawa wa haoma ya manjano, virusi hivi huchukuwa siku tatu mpaka sita kumomaa. Kipindi hiki kitaalamu hufahamika kama incubation period. Katika kipindi hiki katu hutohisi dalili yeyote. Kisha hatua inayofuatainatambulika kama accute phrase kisha hatua ya meisho ni toxic phrase.



DALILI ZA HOMA YA MANJANO
A.Dalili za homa nya manjano katika hatua ya pili (Acute phrase)
1.Homa
2.Maumivu ya kichwa
3.Maumivu ya misuli hasa ya kwenye mgongo na magoti
4.Kutokufurahia mwanga wa jua
5.Vichefuchefu na kutapika
6.Kukosa hamu ya kula
7.Kuhisi kizunguzungu
8.Macho kuwa mekundu, uso na ulimu pia kuwa na rangi nyekundu



B. Dalili za homa ya manjano katika hatua ya pili (toxic phrase)
1.Macho na ngozi kuwa na rangi ya njano
2.Maumivu yasiyo ya kawaida pamoja na kutapika damu
3.Kuongezeka kukojoakojoa
4.Kutoka na damu kwenye mdomo, pua na macho
5.Kupungua kwa mapigo ya moyo (bradycardia)
6.Ini na figo kushindwa kufanya kazi
7.Ubongo kushinwa kufanya kazi, vyema na kusababisha matatizo kama kifafa (seizure), kupoteza fahami (coma) pamoja na kuchanganyikiwa (delirium)



SABABU ZA HOMA NA MANJANO (YELLOW FEVER)
Kama tulivyokwisha kuona kuwa homa ya manjano husababishwa na virusi wanaoenezwa na mbua aina ya Aedes aegypti. Mbu hawa hukaa karibu na maeneo ambayo watu huwa wanaishi na huzaliana kwenye maji yaliyo safi. Virusi vya homa ya manjano vinaweza pia kuwaathiri manyani.



KUJIKINGA NA HOMA YA MANJANO
Ijapokuwa asilimia 20 mapa 50 ya wanaopata homa ya manjano hufariki, lakini itambulike kuwa mgonjwa anauwezo wa kupona kabisa endapo atawahi kupatiw matibabu. Zifuatazo ni baadhi ya njia tu za kujikinga na homa ya manjano



1.pata chanjo ya homa ya manjano
2.Jikinge na kung’atwa na mbu kwa:
?Kulala kwenye chandarua kizima na chenye dawa
?Kupaka losheni ya kuzuia mbu
?Kuondoa majimaji yaliyotuwama na kukata nyasi







                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2507

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Visababishi vya ugonjwa wa Varicose vein

Posti hii inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya ugonjwa wa vericose veini, ni visababishi mbalimbali ambavyo utokea kwenye mtindo wa maisha kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo vya minyoo

Soma Zaidi...
Tatizo la mapafu kuwa na usaha.

Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha .

Soma Zaidi...
Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
je..! naweza kuambukizwa fangasi kwa kujamiiana na mtu mwenye fangasi?

Je ukifanya mapenz na mtu mweny aina hi ya fangasi na akawa anayo maambukizi ya ukimwi.

Soma Zaidi...
Yajue matatizo yanayosababisha Ugonjwa wa akili.

Madhara ya ugonjwa wa akili yanaweza kuwa ya muda au ya kudumu. Unaweza pia kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa afya ya akili kwa wakati mmoja. Kwa mfano, unaweza kuwa na ulegevu na ugonjwa wa matumizi ya madawa ya kulevya.

Soma Zaidi...
Yajue maambukizi kwenye epididimisi kwa kitaalamu huitwa (Epididymitis)

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.

Soma Zaidi...
Dalili zinazoonyesha joto la kupungua mwilini (hypothermia)

joto la mwili wako linapungua, moyo wako, mfumo wa neva na viungo vingine haviwezi kufanya kazi kwa kawaida. Isipopotibiwa, Hypothermia hatimaye inaweza kusababisha moyo wako na mfumo wa upumuaji kushindwa kabisa na hata kifo.

Soma Zaidi...
DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...