MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

NAMNA AMBAVYO MALARIA HUTOKEA

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi. basi tambua kuwa ni mbu jike tu ndiye huweza kuambukiza malaria.  basi hapa nitakueleza namna ambavyo malaria huweza kutokea.

 

kwanza kabisa lazima kuwepo kwa vimelea vya malaria aidha kwa mtu ama kwenye mwili wa mbu jike aina ya anophelesi. vimelea hivi vya malaria vinaanza kuzaliana kwenye mwili wa mbu jike. baada ya siku 10 mpaka 18 vimelea hivi vinakomaa na kuwa kimelea kipya kinachojulikana kama sporozoite. Kisha hivi vimelea vingi vinahamia kwenye tezi za mate za mbu na hatimaye kuingia kwenye mate ya mbu.

 

Mdomo wa mbu una mirija mikuu miwiliu. Mmoja ni wa kunyonyea damu na mwingine ni wa kutolea mate. Wakati anapong'ata mtu mate yake huingia kwenye mwili wa mtu. Mate haya yakiwa yana vimelea vya malaria (sporozoite) vijidudu hivi huingia kwenye mwili wa mtu. Na hapa hatua nyingine ya vimelea hivi inaanza.

 

Vimelea hivi (sporozoite) vinapoingia kwenye mwili wa mtu moja kwa moja vinaelekea kwenye ini. na huko huanza kukuwa na kuwa schizonts baadaye hupasuka na kutoa merozoites hivi ni vimelea vipya vilivyokomaa. vimelea hivi kama havitapatiwa dawa ya kuondolewa vitaendelea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli nyekundu za damu.

 

Baada ya merozoite kupatikana huelekea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli hai nyekundu za damu na kuanza kuzaliana humo kwa mara nyingine na kuleta vimelea vipya vitambulikavyo kama schizont na baadaye kupasuka na kutoa vimlea waitwao merozoites.

 

Na hapa sasa vimelea hawa wapya wanaanza kushambulia seli hai nyekundi na kuzaliana humo kisha seli hupasuka na kuleta vimelea wengi zaidi. Na kuanzia hapa ndipo mgonjwa sasa ataanza kuona dalili za malaria kama homa, maumivu ya kichwa, tumbo, misuli na viungo, kichefuchefu, kutapika na kuharisha.

 

Kama vimelea hivi havitatibiwa athari zaidi itatokea na kuanza kushambulia maeneo mengine ya mwili kama ini, figo, mapafu na moyo. hapa mgonjwa ataweza kuchanganyikiwa, matatizo ya ini na figo, kupumua kwa shida ama kuhohoa. Kama mgonjwa hatatibiwa athari zaidi inaweza kutokea kama kupoteza fahamu na hatimaye kifo.

 


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1006

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo.
Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo.

Posti hii inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo, tunajua kubwa mama kama ana ugonjwa huu anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kinywa
Dalili za uvimbe kwenye kinywa

Post hii inahusu dalili za uvimbe kwenye kinywa ambapo kitaalamu hujulikana Kama oral candidiasis Uvimbe kwenye kinywa husababisha vidonda vyeupe, kwa kawaida kwenye ulimi au mashavu ya ndani. Wakati mwingine uvimbe kwenye kinywa huweza ku

Soma Zaidi...
Tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu (gangrene)
Tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu (gangrene)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu ambao hujulikana Kama gangrene inahusu kifo cha tishu za mwili kutokana na ukosefu wa mtiririko wa damu au maambukizi ya bakteria. Ugonjwa wa gangre

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye uume
Maambukizi kwenye uume

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye uume, maambukizi hata utokea kwenye kichwa Cha uume kwa kitaalamu huitwa Balanitis, zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?
NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?

Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye?

Soma Zaidi...
 Ugonjwa wa kisukari
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...
Saratani (cancer)
Saratani (cancer)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya cancer/saratani

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye figo
Dalili za maambukizi kwenye figo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.

Soma Zaidi...
Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo
Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Tatizo la Kikohozi Cha muda mrefu
Tatizo la Kikohozi Cha muda mrefu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kikohozi cha muda mrefu ni zaidi ya kero. Kikohozi cha muda mrefu kinaweza kuharibu usingizi wako na kukuacha unahisi uchovu. Matukio makali ya kikohozi cha muda mrefu yanaweza kusababisha kutapika, kizunguz

Soma Zaidi...