Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi.
Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi. basi tambua kuwa ni mbu jike tu ndiye huweza kuambukiza malaria. basi hapa nitakueleza namna ambavyo malaria huweza kutokea.
kwanza kabisa lazima kuwepo kwa vimelea vya malaria aidha kwa mtu ama kwenye mwili wa mbu jike aina ya anophelesi. vimelea hivi vya malaria vinaanza kuzaliana kwenye mwili wa mbu jike. baada ya siku 10 mpaka 18 vimelea hivi vinakomaa na kuwa kimelea kipya kinachojulikana kama sporozoite. Kisha hivi vimelea vingi vinahamia kwenye tezi za mate za mbu na hatimaye kuingia kwenye mate ya mbu.
Mdomo wa mbu una mirija mikuu miwiliu. Mmoja ni wa kunyonyea damu na mwingine ni wa kutolea mate. Wakati anapong'ata mtu mate yake huingia kwenye mwili wa mtu. Mate haya yakiwa yana vimelea vya malaria (sporozoite) vijidudu hivi huingia kwenye mwili wa mtu. Na hapa hatua nyingine ya vimelea hivi inaanza.
Vimelea hivi (sporozoite) vinapoingia kwenye mwili wa mtu moja kwa moja vinaelekea kwenye ini. na huko huanza kukuwa na kuwa schizonts baadaye hupasuka na kutoa merozoites hivi ni vimelea vipya vilivyokomaa. vimelea hivi kama havitapatiwa dawa ya kuondolewa vitaendelea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli nyekundu za damu.
Baada ya merozoite kupatikana huelekea kwenye mfumo wa damu na kuanza kushambulia seli hai nyekundu za damu na kuanza kuzaliana humo kwa mara nyingine na kuleta vimelea vipya vitambulikavyo kama schizont na baadaye kupasuka na kutoa vimlea waitwao merozoites.
Na hapa sasa vimelea hawa wapya wanaanza kushambulia seli hai nyekundi na kuzaliana humo kisha seli hupasuka na kuleta vimelea wengi zaidi. Na kuanzia hapa ndipo mgonjwa sasa ataanza kuona dalili za malaria kama homa, maumivu ya kichwa, tumbo, misuli na viungo, kichefuchefu, kutapika na kuharisha.
Kama vimelea hivi havitatibiwa athari zaidi itatokea na kuanza kushambulia maeneo mengine ya mwili kama ini, figo, mapafu na moyo. hapa mgonjwa ataweza kuchanganyikiwa, matatizo ya ini na figo, kupumua kwa shida ama kuhohoa. Kama mgonjwa hatatibiwa athari zaidi inaweza kutokea kama kupoteza fahamu na hatimaye kifo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m
Soma Zaidi...Maumivu ya kifua huja kwa aina nyingi, kuanzia kuchomwa na kisu hadi kuuma kidogo. Baadhi ya Maumivu ya kifua yanafafanuliwa kama kuponda kuungua. Katika baadhi ya matukio, maumivu husafiri juu ya shingo, hadi kwenye taya.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi makundi ambayo yapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa ngiri, ni hatari kwa sababu tunajua kuwa ngiri utokea kwa sababu ya kuta au tishu zinazoshikilia viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwepo kwa uwazi na kufanya viun
Soma Zaidi...Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu
Soma Zaidi...Mngurumo wa moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako. Sauti hizi zinaweza kusikika na kifaa kinachojulikana kama stethoscope. Mapigo ya moyo ya kawaida
Soma Zaidi...Ugojwa wa pumu ni hatari na unaweza kutokea ghafla. Lakini je unaweza kusababisha kifo, makalahii itakwend akujibu swali hili
Soma Zaidi...Kama unahisi maumivu ya tumbo huwenda umejiuliza swali hili ukiwa kama mwanamke "Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?". Post hii inakwenda kujibu swali hili
Soma Zaidi...