Matatozo katika choo kidogo, maradhi ya figo na dalili zake pia namna ya kujikinga na madhradhi ya figo

MATATIZO YA CHOO KIDOGO NA FIGOFigo ni kiungo muhimu sana katika uchujaji wa mkojo, na afya ya mfumo wa utoaji taka mwili.

Matatozo katika choo kidogo, maradhi ya figo na dalili zake pia namna ya kujikinga na madhradhi ya figo

MATATIZO YA CHOO KIDOGO NA FIGO
Figo ni kiungo muhimu sana katika uchujaji wa mkojo, na afya ya mfumo wa utoaji taka mwili. Figo inakazi ya kuchija damu na kuondoa uchafu usiohitajika. Uchafu hii hukusanyika na kutoka nje kwa kupitia moko. Ndani ya mkojo kumekusanyika uchafu wa kemikali, ikiwemo sumu za vyakula na makemikali mabaya kutoka mwilini.



Endapo mfumo huu wa mkojo ukitetereka unaweza kuaathiri afya ya mtu kwa ujumla. Miongoni mwa matatizo katika mfumo wa mkojo ni kuwepo kwa vijijiwe vidogo. Hivi vinaweza kusababisha maumivu makali na kukosa choo kidogo.



Makala hii inakwenda kukupa ufahamu juu ya tatizo la choo kidogo na kutokea kwa vijijiwe kwenye figo. Pia tutaona sababu za kutokea kwa tatizo hili na vipi tutaweza kujiepusha. Songa nayo makala hii ya afya kwa ni ni muhimu sana kufahamu afya yako na afya ya walio karibu nawe.



VIJIWE VYA KWENYE FIGO NI NINI?
Hivi ni vitu vidogo vigumu kama vijijiwe vilivyotengenezwa ka kemikali zinazopatikana kwenye mkojo kama aina za chumvi na tindikali zilizomo kwenye mkojo. Vijijiwe hivi vinaweza kutokea kwenye figo, kibovu ama mirija ya kusafirisha mkojo. Vijiwe hivi hutengenezwa pale mkojo unapojikusanya kwa muda mrefu hivyo hali hii hutoa nafasi kwa kemikali kujikusanya na kutengeneza vijiwe.



Vijiwe hivi huweza kutoka kwa kupitia njia ya mkojo, kwa maumivu makali sana. Pia endapo hali itakuwa ni mbaya zaidi mgonjwa atafanyiwa upasuaji ili kuweza kuondoa vijiwe hivi. Katika kipindi kama hichi mjonjwa anaweza kutumia dawa za kupunguza maumivu. Athari ya vijiwe hivi inaweza kupelekea maumivu wakati wa kukojoa.



DALILI ZAKE
Vijiwe hivi mwanzoni havina dalili yeyote lakini endapo vitakuwa vimeshajikusanya vinaweza kuonyesha dalili zifuatazo:-
1.maumivu wakati wa kukujoa
2.Maumivu upande mmoja, kwenye mgongo na chini ya mbavu
Kukojoa mkojo wa rangi ya pinki, nyekundu ama wenye harufu mbaya
3.Kukojoa mara kwa mara
4.Kupata mkojo kidogo unapokwenda kukojoa
5.Homa
6.Kupata kichefuchefu ama kutapika.



SABABU ZA TATIZO HILI NA CHOO KIDOGO NA FIGO
1.vyakula, ulaji wa baadhi ya vyakula kwa wingi unawza kuwa sababu ya kutengenezwa kwa majingira ya kufanyika kwa viji wa vyakula vyenye chumvi hasa calcium unaweza kusababisha vijiwe hivi. Ulaji wa vyakula vya protini kupitiliza pia unaweza kuleta athaji hasi hata kutokea vijiwe hivi.



2.Athari za mashambulizi ya bakteria katika mfumo wa mkojo; mashambulizi kama ya UTI (Urinary track Infection) yanaweza kusababisha vijijiwe hivi. Endapo ugonjwa wa UTI utakaa kwa muda mrefu bila ya kutibiwa na kupona unakuwa UTI sugu, hii inaweza ksababisha kutokea kwa vijiwe kwenye mfumo wa mkojo.



3.nmna ya mtu anavyoishi yaani staili za maisha (life style). mtindo ambao mtu anaishi unaweza kuwa ni hatari kwa afya yako. Kwa mfano kuwa na tabia ya kutokunywa maji mengi, wakati huo huo ukawa unafanya kazi ambazo zinapoteza maji mwilini kwa wingi, kwa mfano kazi ambazo zinaleta jasho sana kisha ukawa haunywi maji ya kutosha. Hii inaweza kusababisha vijijiwe hivi.



4.kurithi baadhi ya matatizo ya kiafya., unaweza kurithi hali ambazo zinaweza kusababisha kwa urahisi kutokea kwa vijiwe hivi. Unaweza kurithi matatizo flani ya kiafya ambayo husababisha figo kuchuja aina maalumu ya asidi za amino itambulikayo kama cystinuria.



MAMBO YAAYOWEZA KUSAIDIA KUTOKEA KWA MATATIZO KATIKA NJIA YA MKOJO NA KUTOKEA KWA VIJIWE VYA KWENYE FIGO
1.familia (kurithi)
2.Kupungua kwa maji mwilini
3.Vyakula
4.Kuzidi kwa uzito
5.Upasuaji



JE UTAZUIAJE MATATIZO KATIKA NJIA YA MKOJO NA VIJIWE VYA KWENYE FIGO?



Wataalamu wa afya wanatueleza baadhi ya njia za kuweza kukabiliana na kujikinga na matatizo ya haja ndogo yaani mkojo. Njia hizi ukizifuata zitakusaidia usiweze kupatwa na vijiwe katika figo:-
1.kunywa maji mengi ya kutosha
2.Punguza kula vyakula vya chumvi kupituliza
3.Punguza ulaji wa baadhi ya vyakula kwa wingi kupitiliza kama bamia, unywaji wa chai kupitiliza, spinachi, viazi vitamu, maharage ya soya, karanga, na chokoleti



JE MADHARA HAYA YA FIGO, NJIA YA MKOJO NA VIJIWE VYE KWENYE FIGO HUWEZA KUTIBIKA?
Ndio matatizo haya yanatibika bila ya tatizo lolote. Mgonjwa atapewa dawa kulingana nna tatizo lake. Kwa hakika atapona kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu.







                   



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1089

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

YAJUE MARADHI YA KISUKARI

Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa dondakoo

Dondakoo ni ugonjwa mbaya unaosababishwa na sumu inayotengenezwa na bakteria. Husababisha mipako nene nyuma ya pua au koo ambayo inafanya kuwa ngumu kupumua au kumeza. Inaweza kuwa mauti.

Soma Zaidi...
Dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi dalili za jeraha kali kwenye ubongo, ni majeraha ambayo utokea kwenye ubongo pale ambapo mtu anapata ajali au amepigwa na kitu chochote kigumu kichwni, zifuatazo ni dalili za jeraha kali kwenye ubongo

Soma Zaidi...
Ishara na dalili za saratani ya mdomo.

Posti hii inaonyesha dalili na mabo ya hatari kwenye ugonjwa wa saratani ya mdomon.Saratani ya mdomo inarejelea Kansa inayotokea katika sehemu zozote zinazounda mdomo. Saratani ya mdomo inaweza kutokea kwa: Midomo, Fizi, Lugha, Nd

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.

Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
Presha ya kushuka na matibabu yake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka na matibabu yake

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya damu au uboho.

posti hii inahusu dalili za aratani ya damu au ubobo ambayo kwa jina lingine hujulikana Kama Acute lymphocytic Leukemia (ALL) ni aina ya Saratani ya damu na uboho tishu zenye sponji ndani ya mifupa ambapo seli za damu hutengenezwa.

Soma Zaidi...
Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga

Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,

Soma Zaidi...
Ndugu mke Wang viungo vina mlegea miguu inamuaka moto nn tatozo

Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu

Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.

Soma Zaidi...