Navigation Menu



Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.

Madhara ya kutumia Tiba homoni

1. Kuongezeka Uzito kwa mgonjwa

Kuongezeka kwa uzito wa mgonjwa ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia Tiba homoni, tunajua kwamba hii Aina ya Tiba uzuia homoni ambazo usababisha saratani kushindwa kuzalishwa au kusambaa kwenye mwili, madawa haya umwongezea mgonjwa uzito kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia sana Mazoezi Ili kuepuka kuongezeka kwa magonjwa mengine kwa sababu ya kuongezeka kwa uzito, kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula ambavyo haviongezi Uzito kwa haraka.

 

2. Kupoteza kumbukumbu.

Kwa sababu ya kuwepo kwa madawa ambayo uzuia kuzalisha kwa homoni zinazosababisha kuongezeka kwa saratani haya madawa uingilia mfumo wa ubongo ambao usaidia kutunza kumbukumbu na kusababisha mgonjwa kupoteza kumbukumbu za mara kwa mara kwa hiyo wale wanaiwauguza wagonjwa wawasaidie katika kuwakumbusha mambo mbalimbali na ya maana na wasiwalaumu pale wanapotokea kusahau baadhi ya vitu na vya muhimu kwa sababu ya hali waliyonayo.

 

3. Mabadiliko ya hisia

Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani Wana Tabia ya kubadilika kwa hisia mara nyingine utawakuta wamefurahi sana, mara nyingi utawakuta wamekasilika sana na hata mara nyingine kuwachagua watu wa kuwatunza na kuwakataa wengine, Hal hii ikitokea kwa wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani jamaa na wote wanaomuuguza wanapaswa kuchukualia kawaida walidhani  na kuona ni kawaida na wasiwe wakali kwa Tabia za mabadiliko ya wagonjwa.

 

4. Kukosa hamu ya tendo la ndoa.

Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani mara nyingi ukumbwa na tatizo la kukosa hamu ya ngono kwa sababu mara nyingine dawa zinazotumika kuharibu homoni za kansa hata hivyo uleta madhara katika mfumo mzima wa kujamiiana kwa hiyo mgonjwa anakosa hamu ya tendo la ndoa, kwa hiyo mwenza wake anapaswa kufahamu tatizo hili na kuelewa mwenzake kama Hana hamu ya tendo la ndoa.

 

5.kuwepo kwa uchovu 

Kwa sababu ya ya dawa ambayo inafanya kazi mwilini na kwa sababu ya kuharibika kwa seli usababisha mwili ws binadamu kuchoka na mara nyingi mgonjwa uhishiwa nguvu kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia vyakula vyenye wingi wa vitamin, madini na  Aina zote za vyakula Ili kumrudisa mgonjwa afya yake ya kawaida

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 919


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.
Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya jino
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za maumivu ya jino Soma Zaidi...

Mambo yanayosababisha kuharisha
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisichokuwa na damu Soma Zaidi...

Dalili za malaria
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu kwa kitaalamu anaitwa Anopheles.na anasambazwa na mbu jike pale anapotafuta chakula hasa wakati akiwa na mimba. Mbu hawa hupenda kuishi kwenye mnyasi, madibwi haswa kwenye maji yaliyo simama. Soma Zaidi...

Dalili za tetekuwanga
Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu Soma Zaidi...

Visababishi vya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari. Soma Zaidi...

mfano mtu ametoka kusex, jana alafu Leo akikojoa mkojo una muhuma na Wa mwisho unatoka damu, itakuwa ugonjwa gani eti,
Soma Zaidi...

Sababu za Maumivu ya shingo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu. Soma Zaidi...

Ishara na dalili za saratani ya mdomo.
Posti hii inaonyesha dalili na mabo ya hatari kwenye ugonjwa wa saratani ya mdomon.Saratani ya mdomo inarejelea Kansa inayotokea katika sehemu zozote zinazounda mdomo. Saratani ya mdomo inaweza kutokea kwa: Midomo, Fizi, Lugha, Nd Soma Zaidi...

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...