Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.
Madhara ya kutumia Tiba homoni
1. Kuongezeka Uzito kwa mgonjwa
Kuongezeka kwa uzito wa mgonjwa ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia Tiba homoni, tunajua kwamba hii Aina ya Tiba uzuia homoni ambazo usababisha saratani kushindwa kuzalishwa au kusambaa kwenye mwili, madawa haya umwongezea mgonjwa uzito kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia sana Mazoezi Ili kuepuka kuongezeka kwa magonjwa mengine kwa sababu ya kuongezeka kwa uzito, kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula ambavyo haviongezi Uzito kwa haraka.
2. Kupoteza kumbukumbu.
Kwa sababu ya kuwepo kwa madawa ambayo uzuia kuzalisha kwa homoni zinazosababisha kuongezeka kwa saratani haya madawa uingilia mfumo wa ubongo ambao usaidia kutunza kumbukumbu na kusababisha mgonjwa kupoteza kumbukumbu za mara kwa mara kwa hiyo wale wanaiwauguza wagonjwa wawasaidie katika kuwakumbusha mambo mbalimbali na ya maana na wasiwalaumu pale wanapotokea kusahau baadhi ya vitu na vya muhimu kwa sababu ya hali waliyonayo.
3. Mabadiliko ya hisia
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani Wana Tabia ya kubadilika kwa hisia mara nyingine utawakuta wamefurahi sana, mara nyingi utawakuta wamekasilika sana na hata mara nyingine kuwachagua watu wa kuwatunza na kuwakataa wengine, Hal hii ikitokea kwa wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani jamaa na wote wanaomuuguza wanapaswa kuchukualia kawaida walidhani na kuona ni kawaida na wasiwe wakali kwa Tabia za mabadiliko ya wagonjwa.
4. Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani mara nyingi ukumbwa na tatizo la kukosa hamu ya ngono kwa sababu mara nyingine dawa zinazotumika kuharibu homoni za kansa hata hivyo uleta madhara katika mfumo mzima wa kujamiiana kwa hiyo mgonjwa anakosa hamu ya tendo la ndoa, kwa hiyo mwenza wake anapaswa kufahamu tatizo hili na kuelewa mwenzake kama Hana hamu ya tendo la ndoa.
5.kuwepo kwa uchovu
Kwa sababu ya ya dawa ambayo inafanya kazi mwilini na kwa sababu ya kuharibika kwa seli usababisha mwili ws binadamu kuchoka na mara nyingi mgonjwa uhishiwa nguvu kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia vyakula vyenye wingi wa vitamin, madini na Aina zote za vyakula Ili kumrudisa mgonjwa afya yake ya kawaida
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 web hosting 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za saratani ya ini
Posti hii inahusu zaidi dalili za saratani ya ini, ni baadhi ya Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na kuona kwamba mtu fulani ana saratani ya ini.
Soma Zaidi...Madhara ya kutotibu ugonjwa wa makende kushindwa kushuka
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya makende kushindwa t, hiki ni tatizo na huleta madhara
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia afya ya ubongo
Je, umewahi kuhisi ukungu wa akili (brain fog) au kusahau mambo madogo madogo? Ubongo ndio injini ya mwili wako, na unahitaji mafuta sahihi ili kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Makala hii inajadili vyakula vitano muhimu vilivyothibitishwa kisayansi kuboresha kumbukumbu, kuongeza umakini, na kulinda ubongo wako dhidi ya kuzeeka
Soma Zaidi...Dalili za upotevu wa kusikia
posti hii inazungumzia kuhusiana na Upotevu wa kusikia unaotokea hatua kwa hatua kadri umri unavyozeeka (presbycusis) ni jambo la kawaida. T Kwa wale walio na umri wa zaidi ya miaka 75, idadi ya watu walio na upotezaji wa kusikia inakaribia 1 kati y
Soma Zaidi...Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.
Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.
Soma Zaidi...Nini husababisha Fangasi sehemu za Siri
Katika somo hili tutaeleza sababu kuu zinazopelekea kupata fangasi sehemu za siri, mazingira yanayochochea kuongezeka kwa fangasi, pamoja na vitu vinavyochangia maambukizi na kurudia-rudia kwa tatizo.
Soma Zaidi...