Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.
Madhara ya kutumia Tiba homoni
1. Kuongezeka Uzito kwa mgonjwa
Kuongezeka kwa uzito wa mgonjwa ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia Tiba homoni, tunajua kwamba hii Aina ya Tiba uzuia homoni ambazo usababisha saratani kushindwa kuzalishwa au kusambaa kwenye mwili, madawa haya umwongezea mgonjwa uzito kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia sana Mazoezi Ili kuepuka kuongezeka kwa magonjwa mengine kwa sababu ya kuongezeka kwa uzito, kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula ambavyo haviongezi Uzito kwa haraka.
2. Kupoteza kumbukumbu.
Kwa sababu ya kuwepo kwa madawa ambayo uzuia kuzalisha kwa homoni zinazosababisha kuongezeka kwa saratani haya madawa uingilia mfumo wa ubongo ambao usaidia kutunza kumbukumbu na kusababisha mgonjwa kupoteza kumbukumbu za mara kwa mara kwa hiyo wale wanaiwauguza wagonjwa wawasaidie katika kuwakumbusha mambo mbalimbali na ya maana na wasiwalaumu pale wanapotokea kusahau baadhi ya vitu na vya muhimu kwa sababu ya hali waliyonayo.
3. Mabadiliko ya hisia
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani Wana Tabia ya kubadilika kwa hisia mara nyingine utawakuta wamefurahi sana, mara nyingi utawakuta wamekasilika sana na hata mara nyingine kuwachagua watu wa kuwatunza na kuwakataa wengine, Hal hii ikitokea kwa wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani jamaa na wote wanaomuuguza wanapaswa kuchukualia kawaida walidhani na kuona ni kawaida na wasiwe wakali kwa Tabia za mabadiliko ya wagonjwa.
4. Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani mara nyingi ukumbwa na tatizo la kukosa hamu ya ngono kwa sababu mara nyingine dawa zinazotumika kuharibu homoni za kansa hata hivyo uleta madhara katika mfumo mzima wa kujamiiana kwa hiyo mgonjwa anakosa hamu ya tendo la ndoa, kwa hiyo mwenza wake anapaswa kufahamu tatizo hili na kuelewa mwenzake kama Hana hamu ya tendo la ndoa.
5.kuwepo kwa uchovu
Kwa sababu ya ya dawa ambayo inafanya kazi mwilini na kwa sababu ya kuharibika kwa seli usababisha mwili ws binadamu kuchoka na mara nyingi mgonjwa uhishiwa nguvu kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia vyakula vyenye wingi wa vitamin, madini na Aina zote za vyakula Ili kumrudisa mgonjwa afya yake ya kawaida
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Ndugu mke Wang viungo vina mlegea miguu inamuaka moto nn tatozo
Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.
Soma Zaidi...Sababu za vidonda kwenye uume
Vidonda kwenye uume vinaweza kusababishwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) kama kaswende na herpes, maambukizi ya fangasi au bakteria, majeraha madogo, mzio (allergy), au usafi duni. Uchunguzi wa kitabibu ni muhimu ili kutambua chanzo na kupata tiba sahihi.
Soma Zaidi...Je utambuzi wa maambukizi ya ukimwi hupatikana mda gani pale mtu anapoambukizwa
Kuna ukimwi na HIV na kila kimoja kina dalili zake na muda wa kuonyesha hizo dalili.
Soma Zaidi...Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha,
Soma Zaidi...