Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.
Madhara ya kutumia Tiba homoni
1. Kuongezeka Uzito kwa mgonjwa
Kuongezeka kwa uzito wa mgonjwa ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia Tiba homoni, tunajua kwamba hii Aina ya Tiba uzuia homoni ambazo usababisha saratani kushindwa kuzalishwa au kusambaa kwenye mwili, madawa haya umwongezea mgonjwa uzito kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia sana Mazoezi Ili kuepuka kuongezeka kwa magonjwa mengine kwa sababu ya kuongezeka kwa uzito, kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula ambavyo haviongezi Uzito kwa haraka.
2. Kupoteza kumbukumbu.
Kwa sababu ya kuwepo kwa madawa ambayo uzuia kuzalisha kwa homoni zinazosababisha kuongezeka kwa saratani haya madawa uingilia mfumo wa ubongo ambao usaidia kutunza kumbukumbu na kusababisha mgonjwa kupoteza kumbukumbu za mara kwa mara kwa hiyo wale wanaiwauguza wagonjwa wawasaidie katika kuwakumbusha mambo mbalimbali na ya maana na wasiwalaumu pale wanapotokea kusahau baadhi ya vitu na vya muhimu kwa sababu ya hali waliyonayo.
3. Mabadiliko ya hisia
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani Wana Tabia ya kubadilika kwa hisia mara nyingine utawakuta wamefurahi sana, mara nyingi utawakuta wamekasilika sana na hata mara nyingine kuwachagua watu wa kuwatunza na kuwakataa wengine, Hal hii ikitokea kwa wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani jamaa na wote wanaomuuguza wanapaswa kuchukualia kawaida walidhani na kuona ni kawaida na wasiwe wakali kwa Tabia za mabadiliko ya wagonjwa.
4. Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
Wagonjwa wanaotumia homoni kama dawa ya kutibu saratani mara nyingi ukumbwa na tatizo la kukosa hamu ya ngono kwa sababu mara nyingine dawa zinazotumika kuharibu homoni za kansa hata hivyo uleta madhara katika mfumo mzima wa kujamiiana kwa hiyo mgonjwa anakosa hamu ya tendo la ndoa, kwa hiyo mwenza wake anapaswa kufahamu tatizo hili na kuelewa mwenzake kama Hana hamu ya tendo la ndoa.
5.kuwepo kwa uchovu
Kwa sababu ya ya dawa ambayo inafanya kazi mwilini na kwa sababu ya kuharibika kwa seli usababisha mwili ws binadamu kuchoka na mara nyingi mgonjwa uhishiwa nguvu kwa hiyo mgonjwa anapaswa kutumia vyakula vyenye wingi wa vitamin, madini na Aina zote za vyakula Ili kumrudisa mgonjwa afya yake ya kawaida
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 ai web app 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Ujuwe ugonjwa wa ebola, dalili zake na jinsi unavyoweza kusambazwa.
Posti hii inahusu sana kuhusu ugonjwa wa ebora. Ugonjwa huu usababishwa na virusi.Virusi hivyo husababisha kutokwa na damu nyingi mwilini kutokana na kupasuka kwa mishipa ya damu
Soma Zaidi...Presha ya kushuka/hypotension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka/ hypotension
Soma Zaidi...Yaani minasumbuliwa na mgongo kuuma pia kuchoka mgongo na homa zisizo isha
Maumivu ya mgongo yanaweza kuwa ni dalili inayoonyesha tatizo fulani la kiafya ikiwemo magonjwa au majeraha.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa kifaduro kwa watoto chini ya miaka mitano
post hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifaduro ambao hujulikana Kama Pertussis pia inajulikana kama kifaduro ni maambukizi ya bakteria ambayo huingia kwenye pua yako na koo.
Soma Zaidi...Dalili za jeraha kali kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili za jeraha kali kwenye ubongo, ni majeraha ambayo utokea kwenye ubongo pale ambapo mtu anapata ajali au amepigwa na kitu chochote kigumu kichwni, zifuatazo ni dalili za jeraha kali kwenye ubongo
Soma Zaidi...