Kumsaidia sliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo
Posti hii inahusu namna ya kumsaidia mgonjwa aliyepungukiwa na damu kwa sababu ya minyoo.
Namna ya kumsaidia aliyepungukiwa na damu kwas sababu ya kuwepo kwa minyoo.
1. Kwanza tibu tatizo la upungufu wa damu kwa kutumia vyakula vyenye madini ya chuma na vyakula vyenye protini, kwa kutumia vyakula hivi damu inaweza kuongezeka kwa haraka zaidi kuliko kawaida,maana hata kama shida ni minyoo Anemia ndiyo inapaswa kutibiwa haraka kwa sababu damu ikipungua sana inaweza kuleta shida.
2. Kama Kuna dalili zozote za Anemia na zinaonekana wazi, inabidi kuangalia wingi wa damu na kuona kiasi kilichomo kama kiasi Cha wingi wa damu ni zaidi ya 5g/l vyakula na dawa mbalimbali vinaweza kutumika Ili kuongeza damu na mboga mboga za majani zinaweza kutumika Ili kuongeza damu, kama kiwango Cha damu ni Chini ya 5g/l mgonjwa inabidi aongezewa damu mara Moja. Tujue kuwa damu ni muhimu kwa binadamu kwa hiyo ni muhimu kuongeza mara Moja ikiisha.
3. Baada ya kuongeza damu mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuondoa minyoo kama vile mebendazole na albendazole hizi dawa zinapaswa kutumiwa kwa maagizo ya wataalamu wa afya na sio kutumia dawa tu, na tujue mtu akiwa anatumia dawa za minyoo hapaswa kunywa pombe maana ni hatari kwa kuchanganya dawa za minyoo na pombe.
4.Baada ya kumpatia mgonjwa dawa uangalizi unapaswa kuwepo Ili kuhakikisha kuwa mgonjwa anapona kabisa na pia mgonjwa anapaswa kupima wingi wa damu Ili kuangalia kama kiwango Cha damu mwilini kipo kwenye hali ya kawaida kabla hajaruhisiwa kutoka hospitalini, na pia mgonjwa anapaswa kutumia dawa za kuongeza damu na kutumia vyakula vyenye wingi wa protein na vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma.
5. Elimu inabidi utolewa kwa mgonjwa na wote waliomzunguka kuhusu namna ya kujikinga na ugonjwa wa upungufu wa damu hasa kuhusu namna ya kupambana na minyoo kwenye mazingira na kuchimba choo, kunywa maji masafi,kuepuka kucheza kwenye maji yaliyotuhama hasa kwa watoto wadogo na kutumia dawa za minyoo kwa mda Ili kama Kuna Aina yoyote ya minyoo itaondoka na kiwango Cha damu kitakuwa kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Njia za kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi njia mbali mbali ambazo uweza kitumiwa na wataalamu ili kuweza kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.
Soma Zaidi...Jinsi ya kujikinga na mafua (common cold)
Posti hii inazungumzia dalili na namna ya kujikinga tusipate mafua .mafua kwa jina lingine hujulikana Kama baridi ya kawaida (common cold).baridi ya kawaida husababishwa na virusi kwenye pua na hutoa makamasi.
Soma Zaidi...Dalili za fangasi wa kucha.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili,sababu za Hatari,na namna ya kujizuia na fangasi wa kucha.
Soma Zaidi...Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri
Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa.
Soma Zaidi...Visababishi vya ugonjwa wa Varicose vein
Posti hii inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya ugonjwa wa vericose veini, ni visababishi mbalimbali ambavyo utokea kwenye mtindo wa maisha kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu
Soma Zaidi...