Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO
Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo. Basi HIV nayo ina hatua zake mpaka kuwa UKIMWI.
DALILI ZA MWANZO ZA HIV AMA UKIMW
Dalili hizi huanza kuonekana kuanzia wiki mbili mpaka nne na wakati mwingine mpaka sita toka kuingia mwilini. Mara chache sana huweza kuonekana mwanzoni mwa wiki ya kwanza. Katika kipindi hiki mtu anaweza kuona dalili zifuatazo:
1.kufimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua
Dalili hizi pia zinaweza kuhusiana na maradhi mengine, hivyo inaweza kuwa vigumu kujuwa nini chanzo zaidi. Wengi katika wanaopata HIV wametaja kuwa kuvimba kwa tezi ndio dalili pekee walioweza kuopata mwanzoni mwa kuathirika kwao. Wengine wanataja mafua kuwa ndio dalili yao ya kwanza.
Baada ya kipindi hiki kupita mgonjwa hatapata dalili yeyote ile. Hiki ni kipindi hatari sana kwani mtu hataweza kujijua kama ameathirika. Kipindi hiki kinaweza kudumi mpaka miaka 10. katika kipindi hiki virusi vinaendelea kuathiri seli za mwili. Baada ya mwili kuwa umeathirika sana na kudhoofu mtu ataanza kupata dalili za UKIMWI.
DALILI ZA UKIMWI
1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 Dua za Mitume na Manabii π3 kitabu cha Simulizi π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 Kitabu cha Afya π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Walio katika hatari ya kupata magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye liski ya kupata magonjwa ya ngono, ni watu wanaofanya mambo yanayosababisha kupata magonjwa ya ngono.
Soma Zaidi...Matumizi ya chumvi nyingi: Hatari kwa afya ya moyo.
Katika ulimwengu wa kisasa, mtindo wa maisha na vyakula vilivyosindikwa vimesababisha ongezeko kubwa la ulaji wa chumvi kupita kiasi. Makala hii inachunguza uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa sodiamu na magonjwa ya moyo. Tutajadili jinsi chumvi inavyoathiri shinikizo la damu, utaratibu wa uharibifu wa mishipa ya damu, na hatua za kivitendo unazoweza kuchukua ili kupunguza matumizi yake kwa maisha bora na marefu.
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na damu puani: Nini cha kufanya?
Kutokwa na damu puani ni hali inayoweza kumtisha mtu yeyote, hasa kwa sababu ya kuona damu ikitiririka ghafla. Ingawa mara nyingi inaonekana kuwa tatizo kubwa, ukweli ni kwamba sehemu kubwa ya visa hivi ni vidogo na vinaweza kutatuliwa kwa hatua rahisi za nyumbani. Makala haya yanakupa mwongozo wa jinsi ya kudhibiti hali hii kwa usahihi na wakati gani unapaswa kutafuta msaada wa kitabibu.
Soma Zaidi...Ishara za Mpenzi Asiye Mwaminifu
βKuhisi mashaka katika mahusiano ni jambo linaloweza kuleta fadhaa kubwa. Post hii inachunguza ishara mbalimbali za tabia zinazoweza kuashiria kutokuwa mwaminifu, huku ikisisitiza umuhimu wa mawasiliano na ushahidi kabla ya kuhukumu.
Soma Zaidi...Dalilili za kukosa oksijeni
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalilili za kukosa oksijeni ambalo kitaalamu hujulikana Kama apnea.kukosa oksijeni ni tatizo ambapo kupumua kwako hukoma na kuanza unapolala.
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi ya via vya uzazi (PID) na tiba yake.
Maambukizi ya viungo vya uzazi, kitaalamu kama Pelvic Inflammatory Disease (PID), ni hali ya kuvimba kwa viungo vya uzazi vya ndani ya mwanamke, ikiwemo mji wa mimba, mirija ya uzazi, na ovari. Makala hii inaelezea dalili za ugonjwa huu, sababu zake, na umuhimu wa kupata tiba sahihi na ya haraka ili kulinda uwezo wako wa kuzaa.
Soma Zaidi...