picha

Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.

Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO
Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo. Basi HIV nayo ina hatua zake mpaka kuwa UKIMWI.



DALILI ZA MWANZO ZA HIV AMA UKIMW
Dalili hizi huanza kuonekana kuanzia wiki mbili mpaka nne na wakati mwingine mpaka sita toka kuingia mwilini. Mara chache sana huweza kuonekana mwanzoni mwa wiki ya kwanza. Katika kipindi hiki mtu anaweza kuona dalili zifuatazo:
1.kufimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua




Dalili hizi pia zinaweza kuhusiana na maradhi mengine, hivyo inaweza kuwa vigumu kujuwa nini chanzo zaidi. Wengi katika wanaopata HIV wametaja kuwa kuvimba kwa tezi ndio dalili pekee walioweza kuopata mwanzoni mwa kuathirika kwao. Wengine wanataja mafua kuwa ndio dalili yao ya kwanza.



Baada ya kipindi hiki kupita mgonjwa hatapata dalili yeyote ile. Hiki ni kipindi hatari sana kwani mtu hataweza kujijua kama ameathirika. Kipindi hiki kinaweza kudumi mpaka miaka 10. katika kipindi hiki virusi vinaendelea kuathiri seli za mwili. Baada ya mwili kuwa umeathirika sana na kudhoofu mtu ataanza kupata dalili za UKIMWI.



DALILI ZA UKIMWI
1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi





                   



Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 13907

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 web hosting     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Njia za kuzuia ugonjwa wa kisonono

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo utumiwa Ili kuweza kuzuia kuwepo ugonjwa wa kisonono, kwa kufuata njia hizi ugonjwa huu wa kisonono unaweza kupungua kwa kiasi au kuisha kabisa.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya masikio (Ear infections): Nini cha kufanya?

Maambukizi ya masikio hutokea pale bakteria au virusi vinaposhambulia sehemu ya sikio (kwa kawaida sikio la kati au la nje). Ni tatizo la kawaida kwa watoto, lakini linaweza kuwapata watu wazima pia. Makala hii inachambua dalili za kawaida, hatua za dharura za kuchukua nyumbani, na tahadhari kali dhidi ya matumizi mabaya ya dawa za masikio.

Soma Zaidi...
Sababu za Maumivu ya Korodani

Maumivu ya korodani ni tatizo linaloweza kusababishwa na mambo mengi, kuanzia majeraha madogo hadi hali za kiafya zinazohitaji matibabu ya haraka. Makala haya yanalenga kutoa ufahamu kuhusu visababishi hivi na kusisitiza umuhimu wa kuona daktari pale maumivu yanapokuwa makali au ya ghafla.

Soma Zaidi...
Vyakula Bora kwa Mtoto Anayekua

​Lishe sahihi ni msingi mkuu wa ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili. Makala haya yataangazia vyakula muhimu vinavyopaswa kuwemo katika mlo wa mtoto, jinsi ya kuandaa mlo kamili, na ukweli wa kisayansi kuhusu virutubisho vinavyohitajika katika kila hatua ya ukuaji.

Soma Zaidi...
Dalili za Mimba Kabla ya Kukosa Hedhi

​Siku za mwanzoni baada ya kutunga mimba, mwili wa mwanamke huanza kuonyesha mabadiliko madogo ya homoni. Post hii inaangazia ishara za awali ambazo zinaweza kujitokeza hata kabla ya siku ya hedhi inayotarajiwa, ikielezea sababu zake na jinsi ya kuzitofautisha na dalili za kawaida za kabla ya hedhi (PMS).

Soma Zaidi...