Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO
Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo. Basi HIV nayo ina hatua zake mpaka kuwa UKIMWI.
DALILI ZA MWANZO ZA HIV AMA UKIMW
Dalili hizi huanza kuonekana kuanzia wiki mbili mpaka nne na wakati mwingine mpaka sita toka kuingia mwilini. Mara chache sana huweza kuonekana mwanzoni mwa wiki ya kwanza. Katika kipindi hiki mtu anaweza kuona dalili zifuatazo:
1.kufimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua
Dalili hizi pia zinaweza kuhusiana na maradhi mengine, hivyo inaweza kuwa vigumu kujuwa nini chanzo zaidi. Wengi katika wanaopata HIV wametaja kuwa kuvimba kwa tezi ndio dalili pekee walioweza kuopata mwanzoni mwa kuathirika kwao. Wengine wanataja mafua kuwa ndio dalili yao ya kwanza.
Baada ya kipindi hiki kupita mgonjwa hatapata dalili yeyote ile. Hiki ni kipindi hatari sana kwani mtu hataweza kujijua kama ameathirika. Kipindi hiki kinaweza kudumi mpaka miaka 10. katika kipindi hiki virusi vinaendelea kuathiri seli za mwili. Baada ya mwili kuwa umeathirika sana na kudhoofu mtu ataanza kupata dalili za UKIMWI.
DALILI ZA UKIMWI
1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Bongolite - Game zone - Play free game ๐2 Dua za Mitume na Manabii ๐3 web hosting ๐4 ai web app ๐5 Simulizi za Hadithi Audio ๐6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Tofauti ya dalili za mafua ya kawaida na COVID-19.
โKatika ulimwengu wa sasa, kuelewa tofauti kati ya mafua ya kawaida (common cold) na COVID-19 ni muhimu kwa ajili ya usalama wako na wa jamii inayokuzunguka. Ingawa magonjwa yote mawili husababishwa na virusi na kushambulia mfumo wa upumuaji, yana tofauti muhimu katika jinsi yanavyoanza, muda wake, na dalili zake mahususi. Makala haya yanakupa mwongozo wa kulinganisha dalili ili uweze kuchukua hatua sahihi za kiafya.
Soma Zaidi...Kuungulia kwa moyo (Heartburn): Chanzo na njia za kupunguza.
Kuungulia kwa moyoโhali ile ya kuhisi moto au maumivu yanayotokea nyuma ya mfupa wa katikati ya kifuaโni tatizo linalowasumbua watu wengi. Licha ya jina lake, tatizo hili halina uhusiano wowote na moyo; linahusu mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Makala haya yanakupa mwongozo wa kile kinachosababisha hali hii na hatua unazoweza kuchukua ili kupata nafuu.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa vericose veini
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa vericose veini
Soma Zaidi...Dalilili za mimba Kuharibika
Kuharibika kwa mimba ni upotevu wa hiari wa ujauzito kabla ya wiki ya 20. Takriban asilimia 10 hadi 20 ya mimba zinazojulikana huisha kwa kuharibika kwa mimba. Lakini idadi halisi labda ni kubwa zaidi kwa sababu mimba nyingi hutokea mapema sana katika u
Soma Zaidi...Dalili kuu 7 za malaria na dawa ya kutibu malaria
Makala hii itazungumzia dalili za Malaria, athari za kuchelewa kutibu malaria, na matibabu ya malaria
Soma Zaidi...