MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu.
MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO
Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu. Ni katika viungo vichache ambavyo vikikatwa vinaweza kujirudisha, yaani kukuwa. Ini ni katika viungo vinavyo shambuliwa na vimelea vya maradhi mbalimbali pamoja na sumu za vyakula. Ini mwilini husaidia katika mmengenyo wa chakula, na kuondoa sumu za vyakula mwilini. Endapo ini litadhurika kwa namna yeyote ile afya ya mtu katu haitakuwa salama, na athari zake endapo zitachelewa kupatiwa matibabu hupelekea kifo.
Katika makala hii tutakwenda kuyaona baadhi ya maradhi ya ini, dalili zake na njia za kukabiliana nayo. Kuwa nasi kwenye makala hii, na wasambazie wengine uwapendao, kulinda afya zao. Makala kama hizi na nyinginezo utazipata kwenye tovuti yetu www.bongoclass.com
Maradhi yanayoshambulia figo yapo mengi sana, na yapo ambayo hurithiwa na mengine hayarithiwi. Na yapo ambayo huambukizwa na mengine hayaambuizi. Ifuatayo ni orodha ya maradhi ya ini:-
SABABU ZA KUTOKEA KWA MARADHI YA INI:
Ili tuone sababu hizo kwanaz atuone aina za maradhi ya ini. Na himo kwenye aina hizo ndipo utakapojua ni sababu ipi imesababisha maradhi hayao:-
A. Maradhi ya ini yanayosababishwa na maambukizi
Maradhi ya ini yanayosababishwa na maambukizi yanajulikana kama homa ya heatitis. Homa hii husababishwa na virusi wanaotambulika kama hepatisis viruses. Miongoni mwa virusi hao ni:-
1.hepatitis A
2.Hepatitis B
3.Hepatitis C
B. Maradhi ya ini yanayosababishwa na mashambulizi ya mfumo wa kinga mwilini, kushambulia seli za ini. Kitaalamu hutambulika kama immune system Abnomality au Autoimune. Maradhi ya ini yanayosababishwa kwa njia hii ni:-
1.Autoimmune hepatitis
2.Primary biliary cirhosis
3.Primary sclerosing cholangitis
C. Maradhi ya ini yanayosababishwa kwa kurithi
Unaweza kurithi maradhi ya ini kutoka kwa wazazi wako ,ima mmoja wapo ama kwa wote. Maradhi ya ini yanayosababishwa na kurithi ni:-
1.Homochromatosis
2.Hyperoxaluria na oxalosis
3.Wilsonβs diseases
D. Maradhi ya ini yanayosababishwa na saratani (cancer)
1.saratani ya ini
2.Saratani ya nyongo
3.Kuvimba vya ini
DALILI ZA MARADHI YA INI
Katika maradhi yote tulioyataja hapo juu, ynashirikiana kwa pamoja katika dalili zifuatazo:
1.macho na ngozi kuwa na rangi ya njano.
2.Maumivu yasiyo ya kawaida yanayoendana na kuvimba mwili
3.Kuvumba kwenye miguu na vifundo vya miguu (ankles)
4.Kuuma kwa ngozi
5.Mkojo kuwa na rangi nyeusi ama giza
6.Kupata choo chenye rangi kupauka, ama kuwa na damu
7.Uchovu mkali sana na usio wa kawaida
8.Kichefuchefu na kutapika
9.Kukosa hamu ya kula
10.Ngozi kuchubuka kwa urahisi.
MAMBO YANAYOHATARISHA AFYA YA INI NA KULETA MARADHI YA INI
1.unywaji wa pombe kupitiliza
2.Kujidunga sindano kwa kushirikiana
3.Uwekaji wa tatuu
4.Kuongezewa damu
5.Muingiliano wa majimajin ya mwili na damu
6.Kupanya ngono zembe
7.Kisukari
8.Kuzidi kwa uzito
VIPI UTAWEZA KUZUIA MARADHI YA INI
1.Punguza unywaji wa pombe
2.Jiepushe na tabia hatarishi kama kujidunga masindano, kushirikiana vitu vya ncha kali, ngono zembe n.k
3.Pata chanjo ya baadhi ya maradhi ya ini kama hepatitis
4.Ilinde ngozi yako
5.Hakikisha huna uzito wa kuzidi
6.Fanya mazoezi
7.Unapopuliza dawa za wadudu vaa kitambaa puani (mask)
Umeionaje Makala hii.. ?
Dondakoo ni ugonjwa mbaya unaosababishwa na sumu inayotengenezwa na bakteria. Husababisha mipako nene nyuma ya pua au koo ambayo inafanya kuwa ngumu kupumua au kumeza. Inaweza kuwa mauti.
Soma Zaidi...Ugonjwa sugu wa figo, pia huitwa kushindwa kwa figo sugu, huelezea upotevu wa taratibu wa utendakazi wa figo. Figo zako huchuja taka na Majimaji kupita kiasi kutoka kwa damu yako, ambayo hutolewa kwenye mkojo wako. Ugonjwa sugu wa figo unapofikia hatua
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazopelekea kukosa choo ,yaani kinyesi kuwa kigumu au kukosa kabisa choo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, hizi ni njia ambazo zinapaswa kufuatwa ili kutokomeza kabisa maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Mnamo mwaka 2016 World Health Organization (WHO) iliitisha kikao cha dharura mnamo mwezi tarehe 1 mwezi wa pili mpaka tarehe 13 mwezi wa nne.
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana Kuvimbiwa kwa watoto ni tatizo la kawaida.Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi kuna sifa ya kupata haja kubwa mara kwa mara au kinyesi kigumu, kikavu. Sababu mbalimbali zinaweza kusababisha kuvimbiwa kwa watoto.Sababu za kawa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya koo, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu ya koo la hewa, na na huwa na dalili zake kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa usafi katika maisha ya mwanadamu au mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...