picha

Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo

HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu.

Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo

HOMA YA DENGUE
Homa ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu. Huweza kutokea katia maeneo ynye uoto wa kitropiki kama maeneo ya Afrika na Asia. Dengue kitaalamu pia hufahamika kama hdengue emorrhagic fever. Homa hii huweza kusababisha kushuka kwa presha ya damu, homa kali sana kutokwa na damu na hata kufariki.

Ugonjwa wa dengue huweza kuathiri mamilioni ya watu dunia nzima bado wataalamu wapo katika kutafuta chanjo ya ugonjwa huu. Kama ilivyo magonjwa mengine ya virusi dengue pia haina dawa maalumu, lakini mgonjwa atatibiwa kulingana na dalili anazoonyesha na hatimaye atapona. Wagonjwa wengi hupata nafuu dani ya wiki moja.

DALILI ZA UGONJWA WA HOMA YA DENGUE
1.homa kali sana inayofika nyizi 41 za sentigredi
2.Maumivu ya kicha
3.Maumivu ya misuli, viungio na mifupa
4.Maumivu nyuma ya macho

Pia unaweza ukaona dalili nyingine kama:-
1.kuenea kwa ukurutu mwilini
2.Kuchefuchefu na kutapika
3.Kutokwa na damu kwenye finzi na pua

ATHARI ZA KUCHELEWA KUTIBUWA KWA HOMA YA DENGUE
1.kutoka damu kwa wingi kwenye pua na mdomo
2.Maumivu makali sana ya tumbo
3.Kutapika kusikokoma
4.Kutokwa na damu chini ya ngozi
5.Matatizo kwenye ini, mapafu na moyo
6.Kifo

SABABU ZA HOMA YA DENGUE
Kama tulivyoona hapo juu kuwa homa ya dengue husababishwa na virusi ambao wanasambazwa na mbu. Pindi mbu kwenye virusi hawa akimng’ata mtu kumuachia virusi vya dengue.

NJIA ZA KUPAMBA NA NA HOMA YA DENGUE
Mpaka sasa hakuna chanjo ya homa ya dengue. Hivyo njia madhubuti na ya kipekee ni kujiepusha na kungwata na mbu aina ya Aedes aegypti. Kwa kutokomeza mazalia yote ya mbu karibu na maeneo unayoishi. Mbu hawa wanang’ata wakati wa mchana tofauti na mbu wanaoleta malaria ambao hung’ata wakati wa usiku.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2304

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ujue ugonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata UTI

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa

Soma Zaidi...
Sababu za vidonda kwenye uume

Vidonda kwenye uume vinaweza kusababishwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) kama kaswende na herpes, maambukizi ya fangasi au bakteria, majeraha madogo, mzio (allergy), au usafi duni. Uchunguzi wa kitabibu ni muhimu ili kutambua chanzo na kupata tiba sahihi.

Soma Zaidi...
Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtot

Soma Zaidi...