Navigation Menu



image

Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo

DALILI ZA UKIMWI NA HIV KWENYE ULIMU NA MDOMO

 

HIV hivi ni virusi vilivyopata umaarufu sana kwa kufahamika kuwa ndio virusi pekee vinavyoweza kusababisha upungufu wa kinga mwilini yaani UKIMWI. Virusi hivi anaweza kuvipata binadamu yeyote yule. Zipo njia nyingi ambazo unaweza kupata virusi hivi kama kushiriki ngono zembe, kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kijifungua, kushiriki vitu vyenye ncha kali, kupewa damu yenye virusi, na njia nyingine kibao. Dalili za HIV na UKIMWI zinatofautiana kulingana na hatua ya mgonjwa. Lanini kuna wakati Ulimi na Mdomo kuweza kuonyesha dalili hizi wazi wazi.

 

Dalili za HIV na UKIMWI kupitia mdomoni zinaweza kuwa ni dalili za mwanzoni sana za UKIMWI kwa baadhi ya watu. Ukweli ni kuwa dalili hizi zinaweza kumpata yeyote lakini kuna watu wapo hatarini zaidi kama watoto wachanga, wazee na watu wenye upungufu wa kinga yaani UKIMWI. Dalili hizi tutaziona moja hadi nyingine hapo chini.

 

Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi1.Kukauka kwa mdomo na kuoza kwa meno.Virusi vya HIV vinaweza kupelekea mdomo kukauka na kukosa mate ya kutosha. Hivyo miongoni mwa kazi za mate ni kulinda meno na mdomo. Hivyo kupelekea meno kuoza. Ni vyema mgonjwa kama anatatizo hili kuonana na daktari aweze kumpa ushauri. Unaweza kutumia dawa maalumu kwa ajili ya kuchochea mate ama kutafuna bigji ambazo hazina sukari.

 

2.Kupata fangasi wa kwenye mdomo wajulikanao kama candidiasis (thrush).Fangasi hawa wanaweza kusababisha madoa mekundu kwenye ulimi, ama mdoa meupe kwenye mdomo. Pia wanaweza kusababisha kupasuka kwa kona za mdomo na kutengeneza weupe kwenye kona za mdomo. Pia mdomoni kunaweza kuta buda la nyama lisilokuwa na maumivu. Fangasi hawa wanaweza kuhamia kwenye koo na kusababisha maumivu. Fangasi hawa ni rahisi sana kuondoka baada ya matibabu ila kwa baadhi ya sababu wanaweza kuwa sugu.

 

3.Vidonda kwenye mdomo na ulimiHivi ni vijidonda vijidogo ambavyo vipo duara. Vinaweza kutokea kwenye ulimi na kwenye mashavu kwa ndani. Pia vinaweza kutokea nyuma ya koo. Vidonda hivi vinakuwa na rangi nyekunu pembeni na rangi ya kijivu katikati. Misongo ya mawzo na baadhi ya vyakula vinaweza kuwa ni sababu.

 

4.Vidonda vya homa.Kama umeshawahi kushuhudia vidonda ambavyo vinatokana na homa. Vidonda hivi kwa watu wenye UKIMWI vina tabia ya kujirudia mara kwa mara. Dawa za ART huweza kusaidia hali hii kutotokea.

 

5.Maradhi ya ufinzi ama periodontitis or gingivitisHaya ni maradhi ya ufizi ambapo ufinzi unakosa nguvu na kushindwa kuzuia meno vyema. Hal hii inaweza kupelekea kung’oka kwa meno. Hali hii inaweza tokea mapema sana miezi 18 baada ya kupata HIV. Ukavu kwenye mdomo, kuvuta sigara kunaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi.

 

6.Kuota kwa kambakamba ama vinywele vinywele kwenye ulimi na pembeni ya ulimi.Kitaalamu hivi hujulikana kama Hairy Leukoplakia. Vikambakamba ama vinyweleo nyweleo hivi havina maumivu lakini pia haviwezi kutoka hata kwa kupiga mswaki. Hii inaweza kuwa ni katika dalili za mwanzo zaidi za UKIMWI. Vyenyewe vipo na rangi nyeupe

 

7.Madoa ya rangi ya dhambarau iliyowiva ama nyekundu kwenye mafinzi, sehemu ya juu ya mdomo na nyuma ya ulimi. Kitaalamu hufahamika kama Kaposi’s Sarcoma (KS Hii inaweza kuwa ni dalili ya kwanza kwa mtu ambaye hajapima HIV. Na kwa ambaye ameshaanza kutumia dawa dalili hizi ni si rahisi kujionyesha.

 

8.Kuota chunjua kwenye mdomo,na ulimi. Hizi husababishwa na virusi vinavyojulikana kama Human Papillomavirus, HPV. Kikawaida chunjua inaweza kuota popote pale kwenye mwili hasa hasa hutokea mara nyingi kwenye mikono. Watu wenye HIV chunjia hizi huweza kuvamia ulimi na kuhama maeneo mengine kwenye mdomo. Pia baadhi ya virusi wanao;eta hali hii wanaweza kusababisha saratani.

 

Mwisho nikufahamishe tu kuwa mdomo ni katika sehemu za kwanza kuonyesha dalili za HIV na UKIMWI. Ni vyema kwenda kupima endapo utagundua una moja ya dalili hizo hapo juu






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3593


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dawa za kutibu kiungulia
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...

Matibabu ya fangasi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matibabu ya fangasi Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa Saratani.
Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa macho.
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu
Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa. Soma Zaidi...

Tatizo la tezi koo
Posti hii inahusu zaidi tatizo la tezi koo, ni tatizo ambalo uwapata watu mbalimbali ambapo Usababisha koo kuvimba na mgonjwa huwa na maumivu mbalimbali na pengine mgonjwa upata kikohozi kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye koo. Soma Zaidi...

Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito
Post inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito au ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.ugonjwa huu uleta madhara kwa wajawazito kama tutakavyoona Soma Zaidi...

je Kama utaonekana kupatwa na homa,kichwa,tumbo, kiharisha kwa siku moja( ya kwanza) na vyote kupona siku nyingine (ya pili kupona) pasipo kutumia dawa inaweza kuwa Ni dalili ya ugonjwa wa zinaa ?
Homa ni moka ya dalili inayohusiana na maradhi mengi sana. Unaweza kuwa na homa ikawa pia si maradhi kumbe ni stress tu. Je unasumbuliwa na homa za mara kwamara, Makala hii ni kwa ajili yako Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya jino
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za maumivu ya jino Soma Zaidi...

Kuona damu kwenye mkojo
Kuona damu kwenye mkojo kunaweza kusababisha wasiwasi. Ingawa katika hali nyingi kuna sababu zisizofaa, Damu kwenye mkojo (hematuria) pia inaweza kuonyesha ugonjwa mbaya. Soma Zaidi...

maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?
Dr huwa nasikia maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo? Soma Zaidi...

Njia za kupambana na fangasi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na fangasi Soma Zaidi...