Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.
Fanya hivi ili kuilinda figo yako:
1. kula vyakula vyenye kuupa mwili wako afya. Vyakula hivi ni kama samaki, matunda, mbogmboga na kuepuka vyakula visivyo boresha afya kama vyenye mafuta mengi, chumvi nyingi ama vyenye sukari nyingi.
2. fanya mazoezi kwa mara kwa mara. Kufanya mazoezi sio tu kuwa kunaboresha afya ya figo bali kunaboresha afya ya viungo vingine kama moyo, misuli na mifumo mingine ya mwili. Pia mazoezi hufanya mwili kuwa imara.
3. hakikisha una uzito wa kawaida. Uzito kuzidi tofauti na kawaida kunaweza kusababisha shida nyingi za kiafya kama hatari ya kuweza kupata kisukari, pia huhatarisha afya ya moyo na figo. hakikisha uzito wako unaendana na urefu wako. Ongea na daktari kujuwa kama uzito wako umeendana na urefu wako.
4. Pata usingizi wa kutosha. Mwili unahitaji usingizi kwa ajili ya mambo mengi, usingizi husaidia mwili kutibu majeraha kwa ufanisi, kuboresha mfumo wa kinga na kufanya mwili ku starehe (relax). Mtu akikosa ukisngizi anaweza kuwa katika hatari ya kupata maradhi mbalimbali ikiwepo maradhi ya figo.
Njia nyingine za kulinda figo:
1. Wacha kuvuta sigara
2. Punguza kunywa pombe
3. Punguza misongo ya mawazo
4. Hakiisha sukari ya mwili ipo katika hali ya kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 kitabu cha Simulizi π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 Simulizi za Hadithi Audio π6 web hosting
Post zinazofanana:
Fangasi wa sehemu za Siri
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu fangasi wa sehemu za Siri
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kupooza (Stroke): Dalili za mwanzo na kinga.
βUgonjwa wa kupooza, unaojulikana kitabibu kama stroke au cerebrovascular accident (CVA), ni dharura kubwa ya kitabibu inayotokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo unapoingiliwa au kukatika. Kila sekunde ni muhimu katika kuokoa tishu za ubongo na kupunguza ulemavu wa kudumu. Makala haya yanafafanua dalili za mwanzo, sababu za hatari, na mikakati madhubuti ya kuzuia ugonjwa huu kwa maisha yenye afya bora
Soma Zaidi...WAJUE FANGASI, AINA ZAKE, DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE
Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa macho.
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Sababu za ugonjwa wa mkojo kuwa na damu
Posti hii inaelezea sababu zinazosababisha mkojo kuwa na damu.
Soma Zaidi...Sababu Zinazoweza Kusababisha Majibu ya Uongo ya HIV
βKupata matokeo ya "positive" (chanya) katika kipimo cha VVU ni jambo linaloweza kuleta hofu kubwa. Hata hivyo, mara chache sana, vipimo vya VVU vinaweza kutoa majibu yanayoitwa false positive (majibu ya uongo), ambapo mtu hana virusi lakini kipimo kinaonyesha anavyo. Makala hii inaelezea mazingira ambayo yanaweza kusababisha hali hii na nini unapaswa kufanya ikiwa utapata matokeo hayo.
Soma Zaidi...