Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.
Fanya hivi ili kuilinda figo yako:
1. kula vyakula vyenye kuupa mwili wako afya. Vyakula hivi ni kama samaki, matunda, mbogmboga na kuepuka vyakula visivyo boresha afya kama vyenye mafuta mengi, chumvi nyingi ama vyenye sukari nyingi.
2. fanya mazoezi kwa mara kwa mara. Kufanya mazoezi sio tu kuwa kunaboresha afya ya figo bali kunaboresha afya ya viungo vingine kama moyo, misuli na mifumo mingine ya mwili. Pia mazoezi hufanya mwili kuwa imara.
3. hakikisha una uzito wa kawaida. Uzito kuzidi tofauti na kawaida kunaweza kusababisha shida nyingi za kiafya kama hatari ya kuweza kupata kisukari, pia huhatarisha afya ya moyo na figo. hakikisha uzito wako unaendana na urefu wako. Ongea na daktari kujuwa kama uzito wako umeendana na urefu wako.
4. Pata usingizi wa kutosha. Mwili unahitaji usingizi kwa ajili ya mambo mengi, usingizi husaidia mwili kutibu majeraha kwa ufanisi, kuboresha mfumo wa kinga na kufanya mwili ku starehe (relax). Mtu akikosa ukisngizi anaweza kuwa katika hatari ya kupata maradhi mbalimbali ikiwepo maradhi ya figo.
Njia nyingine za kulinda figo:
1. Wacha kuvuta sigara
2. Punguza kunywa pombe
3. Punguza misongo ya mawazo
4. Hakiisha sukari ya mwili ipo katika hali ya kawaida.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza namna mbalimbali za kujikinga na VVU/UKIMWI
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi kwenye figo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.
Soma Zaidi...Dalili za Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Yaani minasumbuliwa na mgongo kuuma pia kuchoka mgongo na homa zisizo isha
Maumivu ya mgongo yanaweza kuwa ni dalili inayoonyesha tatizo fulani la kiafya ikiwemo magonjwa au majeraha.
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya ini
Posti hii inahusu zaidi dalili za saratani ya ini, ni baadhi ya Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na kuona kwamba mtu fulani ana saratani ya ini.
Soma Zaidi...