HOMA YA MANJANO (yellow fever)Homa ya manjano ni maradhi yanayosababishwa na virusi na husambazwa na mbu.
HOMA YA MANJANO (yellow fever)
Homa ya manjano ni maradhi yanayosababishwa na virusi na husambazwa na mbu. Homa hii ipo sana nchi za Afrika na Amerika ya Kusini. Kwa hali ya kawaida homa ya manjano huweza kusababisha homa, maumivu ya kichwa, kichefuchefu na kutapika. Pia homa ya manjano inaweza kuwa mbaya zaidi na kupelekea matatizo kwenye ini, figo na moyo pamoja na kutoka kwa damu yali inayotambulika kitaalamu kama hemorrhaging.
Inakadiriwa kuwa asilimia 50 ya wanaopata homa ya manjano wanafariki kwa maradhi maradhi haya. Tafiti zinaonyesha kuwa mpaka sasa hakuna tiba maalumu ya homa ya manjano, ila ipo chanjo kwa ajili ya kujikinga na virusi wanaosababisha homa hii.
Tafiti zinaonesha kuwa baada ya kungโatwa na mbu na kukuachia virusi hawa wa haoma ya manjano, virusi hivi huchukuwa siku tatu mpaka sita kumomaa. Kipindi hiki kitaalamu hufahamika kama incubation period. Katika kipindi hiki katu hutohisi dalili yeyote. Kisha hatua inayofuatainatambulika kama accute phrase kisha hatua ya meisho ni toxic phrase.
DALILI ZA HOMA YA MANJANO
A.Dalili za homa nya manjano katika hatua ya pili (Acute phrase)
1.Homa
2.Maumivu ya kichwa
3.Maumivu ya misuli hasa ya kwenye mgongo na magoti
4.Kutokufurahia mwanga wa jua
5.Vichefuchefu na kutapika
6.Kukosa hamu ya kula
7.Kuhisi kizunguzungu
8.Macho kuwa mekundu, uso na ulimu pia kuwa na rangi nyekundu
B. Dalili za homa ya manjano katika hatua ya pili (toxic phrase)
1.Macho na ngozi kuwa na rangi ya njano
2.Maumivu yasiyo ya kawaida pamoja na kutapika damu
3.Kuongezeka kukojoakojoa
4.Kutoka na damu kwenye mdomo, pua na macho
5.Kupungua kwa mapigo ya moyo (bradycardia)
6.Ini na figo kushindwa kufanya kazi
7.Ubongo kushinwa kufanya kazi, vyema na kusababisha matatizo kama kifafa (seizure), kupoteza fahami (coma) pamoja na kuchanganyikiwa (delirium)
SABABU ZA HOMA NA MANJANO (YELLOW FEVER)
Kama tulivyokwisha kuona kuwa homa ya manjano husababishwa na virusi wanaoenezwa na mbua aina ya Aedes aegypti. Mbu hawa hukaa karibu na maeneo ambayo watu huwa wanaishi na huzaliana kwenye maji yaliyo safi. Virusi vya homa ya manjano vinaweza pia kuwaathiri manyani.
KUJIKINGA NA HOMA YA MANJANO
Ijapokuwa asilimia 20 mapa 50 ya wanaopata homa ya manjano hufariki, lakini itambulike kuwa mgonjwa anauwezo wa kupona kabisa endapo atawahi kupatiw matibabu. Zifuatazo ni baadhi ya njia tu za kujikinga na homa ya manjano
1.pata chanjo ya homa ya manjano
2.Jikinge na kungโatwa na mbu kwa:
?Kulala kwenye chandarua kizima na chenye dawa
?Kupaka losheni ya kuzuia mbu
?Kuondoa majimaji yaliyotuwama na kukata nyasi
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Haya ni masharti ya mwenye vidonda vya tumbo. Mgojwa wa vidonda vya hatumbo hatakiwi kufanya yafuatayo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea pale ambapo Ugonjwa wa ngiri unaposhindwa kutibiwa mapema.
Soma Zaidi...Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu inayotumiwa kwa ajili ya kusikia, Kuna wakati mwingine hushambulia na bakteria na virusi
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalilili za kukosa oksijeni ambalo kitaalamu hujulikana Kama apnea.kukosa oksijeni ni tatizo ambapo kupumua kwako hukoma na kuanza unapolala.
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za Pua iliyovunjika, pia inaitwa fracture ya pua, ni kuvunjika au kupasuka kwa mfupa katika pua yako
Soma Zaidi...Homa ni moka ya dalili inayohusiana na maradhi mengi sana. Unaweza kuwa na homa ikawa pia si maradhi kumbe ni stress tu. Je unasumbuliwa na homa za mara kwamara, Makala hii ni kwa ajili yako
Soma Zaidi...kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako
Soma Zaidi...post hii inaelezea kuhusiana na dalili au ishara na madhara ya Kiungulia ni maumivu ya moto kwenye kifua chako, nyuma ya mfupa wako wa kifua. Maumivu huwa mabaya zaidi wakati wa kulala au kuinama
Soma Zaidi...Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza zaidi khusu dalili za ukimwi ama HIV kwa wanaume
Soma Zaidi...