image

Mafunzo ya database MySQL somo la 3

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.

Matumizi ya MySQL katika database.

Naamini umeshajifunzakuwa MySQL ni software ambayo hutumika katika kudhibiti database yako. Pia ulishaweza kuandaa kifaa chako katika somo la kwanza. Katika somo hili nitakwenda kukujuza sehemu muhimu za MySQL na namna ya kutengeneza database yako.

 

Kama ulishawahi kutumia database ya microsoft office inayojulukana kama microsoft access, basi itakuwa rahisi kwako kutambuwa nini kinachotokea. Kama ndio mara yako ya kwanza kutengeneza database somo hili ni kwa ajili yako.

 

Je unajuwa kuwa:

Chati zetu zote za facebook, wasap na instagram zimehifadhiwa kwenye database? Itambulie kuwa karibia  mbog zote hutumia database. Hivyo somo hili ni moja katikamasomomuhmu sana ya wewe kujuwa nini kinachoendelea katika mitandao, na vipi taarifa zako zinahifadhiwa.

 

FUNGUWA MySQL

Pitia tena somo la kwanza namna ya kufunguwa MySQL kwenye simu ama kompyuta kisha uendelee na somo hili.kama umeshafika ile hatuwa ya kuona neno database basi tutaanzia hapo.

 

JINSI YA KUTENGENEZA DATABASE:

Kama umeshaifunguwa MySQL utaona kuna menu hapo juu. Hiyo menu utaona ina items hizi

  1. Databases
  2. SQL
  3. Status
  4. User acounts
  5. Export
  6. Import
  7. Setting
  8. Replication
  9. Variables
  10. Charsets
  11. Engines
  12. Plugins

 

Hizo ndio sehemu kuu za MySQL ambazo zitakwenda kutumika. Katika somo hili la leo tutajifunza menu ya kwanza na ya pili tu tu ambazo ni Databases na SQL. Hii ndio sehemu ambayo utaanza kutengeneza database kabla ya kujifunza kutumia SQL.

 

Create database

Tuanze somo letu sasa na kutengeneza DATABASE. Kama ulivyoifunza ni kuwa database ni mkusanyiko wa taarifa zilizopangiliwa na zinafikiwa kwa njia za ki electronic. Sasa kwa mfano una blog yako na unataka kutengeneza database kwa ajili ya blog. Kita cha kwanza mi kutafuta jina la hiyo database yako. Utaiita vipi?

 

Tuchukulie mfano jina la database yetu ni mafunzo. Sasa hatuwa inayofata ni kutengeneza database inayoitwa mafunzo. Katika menu yako bofya neno database. Utaona kuna sehemu kumeandikwa create database. Kisha chini kuna kabox ndani kana neno database name. Hapo ndani weka jina la database yako, mfano utaweka mafunzo. Kisha bofya neno create.

 

Baada ya hapo utaona kwenye orodha ya database kuna database inayoitwa mafunzo. Katika ukurasa huo pia kwa juu utaona kuna neno structure, pia kuna neno lingine limeandikwa no table found. Chini yake kuna neno limeandikwa CREATE TABLE IF NOT EXISTS. Hizi zote tutakuja ziona somo lijalo.

 

Mpaka kufikia hapo umeweza kutengeneza database yako kwa kutumia menu ya database. Sasa hatuwa inayofata ni kufuta database. Ila kabla ya kufuta database tunakwenda kutengeneza database nyingine kwa kutumia menu ya SQL.

 

Ili kfanya hivi tunatakiwa tujuwe kwanza kuwa SQL ni menu ambayo itakuletea uwanja wa kuingiza code za SQL language. Kwa kutumia sql unaweza kutengeneza database kwa kuandika create database kisha unaweka jina la database yako kwa mfano post kisha utamalza na alama hii ; hivyo itakuwa hivi create database post;. Ukiweka maneno haya maana yake unaiambia MySQL kuwa itengeneze database ambayo inaitwa post.

 

Ok hebu tuanze sasa.

  1. Bofya SQL
  2. Andika SQL statement ambazo ni:- CREATE DATABASE post;
  3. Kisha bofya neno GO utaliona chini upande wa kulia
  4. Baada ya hapo tadabase yako itakuwa ipo tayari angalia kwenye orodha ya dtabase.

 

Mpaka kufikia hapa tutakuwa na database mbili katika listi yetu. Katika somo la tatu nne tutakwenda kujifunza namna ya kufuta, na kubadili jina database yetu.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa ihsai ya

Bongoclass.com

Web:bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1711


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)
hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database MySQL database somo la 9
haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)
Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file. Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la tano (5)
Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)
hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML. Soma Zaidi...

PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho. Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la kumi (10)
Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)
Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...