Mafunzo ya database MySQL somo la 3


image


Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.


Matumizi ya MySQL katika database.

Naamini umeshajifunzakuwa MySQL ni software ambayo hutumika katika kudhibiti database yako. Pia ulishaweza kuandaa kifaa chako katika somo la kwanza. Katika somo hili nitakwenda kukujuza sehemu muhimu za MySQL na namna ya kutengeneza database yako.

 

Kama ulishawahi kutumia database ya microsoft office inayojulukana kama microsoft access, basi itakuwa rahisi kwako kutambuwa nini kinachotokea. Kama ndio mara yako ya kwanza kutengeneza database somo hili ni kwa ajili yako.

 

Je unajuwa kuwa:

Chati zetu zote za facebook, wasap na instagram zimehifadhiwa kwenye database? Itambulie kuwa karibia  mbog zote hutumia database. Hivyo somo hili ni moja katikamasomomuhmu sana ya wewe kujuwa nini kinachoendelea katika mitandao, na vipi taarifa zako zinahifadhiwa.

 

FUNGUWA MySQL

Pitia tena somo la kwanza namna ya kufunguwa MySQL kwenye simu ama kompyuta kisha uendelee na somo hili.kama umeshafika ile hatuwa ya kuona neno database basi tutaanzia hapo.

 

JINSI YA KUTENGENEZA DATABASE:

Kama umeshaifunguwa MySQL utaona kuna menu hapo juu. Hiyo menu utaona ina items hizi

  1. Databases
  2. SQL
  3. Status
  4. User acounts
  5. Export
  6. Import
  7. Setting
  8. Replication
  9. Variables
  10. Charsets
  11. Engines
  12. Plugins

 

Hizo ndio sehemu kuu za MySQL ambazo zitakwenda kutumika. Katika somo hili la leo tutajifunza menu ya kwanza na ya pili tu tu ambazo ni Databases na SQL. Hii ndio sehemu ambayo utaanza kutengeneza database kabla ya kujifunza kutumia SQL.

 

Create database

Tuanze somo letu sasa na kutengeneza DATABASE. Kama ulivyoifunza ni kuwa database ni mkusanyiko wa taarifa zilizopangiliwa na zinafikiwa kwa njia za ki electronic. Sasa kwa mfano una blog yako na unataka kutengeneza database kwa ajili ya blog. Kita cha kwanza mi kutafuta jina la hiyo database yako. Utaiita vipi?

 

Tuchukulie mfano jina la database yetu ni mafunzo. Sasa hatuwa inayofata ni kutengeneza database inayoitwa mafunzo. Katika menu yako bofya neno database. Utaona kuna sehemu kumeandikwa create database. Kisha chini kuna kabox ndani kana neno database name. Hapo ndani weka jina la database yako, mfano utaweka mafunzo. Kisha bofya neno create.

 

Baada ya hapo utaona kwenye orodha ya database kuna database inayoitwa mafunzo. Katika ukurasa huo pia kwa juu utaona kuna neno structure, pia kuna neno lingine limeandikwa no table found. Chini yake kuna neno limeandikwa CREATE TABLE IF NOT EXISTS. Hizi zote tutakuja ziona somo lijalo.

 

Mpaka kufikia hapo umeweza kutengeneza database yako kwa kutumia menu ya database. Sasa hatuwa inayofata ni kufuta database. Ila kabla ya kufuta database tunakwenda kutengeneza database nyingine kwa kutumia menu ya SQL.

 

Ili kfanya hivi tunatakiwa tujuwe kwanza kuwa SQL ni menu ambayo itakuletea uwanja wa kuingiza code za SQL language. Kwa kutumia sql unaweza kutengeneza database kwa kuandika create database kisha unaweka jina la database yako kwa mfano post kisha utamalza na alama hii ; hivyo itakuwa hivi create database post;. Ukiweka maneno haya maana yake unaiambia MySQL kuwa itengeneze database ambayo inaitwa post.

 

Ok hebu tuanze sasa.

  1. Bofya SQL
  2. Andika SQL statement ambazo ni:- CREATE DATABASE post;
  3. Kisha bofya neno GO utaliona chini upande wa kulia
  4. Baada ya hapo tadabase yako itakuwa ipo tayari angalia kwenye orodha ya dtabase.

 

Mpaka kufikia hapa tutakuwa na database mbili katika listi yetu. Katika somo la tatu nne tutakwenda kujifunza namna ya kufuta, na kubadili jina database yetu.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa ihsai ya

Bongoclass.com

Web:bongoclass.com

Email: [email protected]

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)
Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1
Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL somo la 3
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7
Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL database somo la 9
haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE Soma Zaidi...