MAFUNZO YA PHP LEVEL 1 SOMO LA NNE (4)


image


somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.


SOMO LA NNE

TYPE OF DATA IN PHP:

Kabla ya kuendelea mbele zaidi katika somo la PHP sasa kwanza lazima tujuwe aina za data ambazo tunakwenda kuzitumia kwenye php. Kila taarifa tunayotaka kuitumia aka kuionyesha lazima tujuwe ipo katika aina ipi ya data. Hii itakusaidia wewe katika kupanga actions. Pia katika kuweka fomu za madodoso.

 

Kwa ufupi katika php kuna aina kuu 7 za data ambazo tutakwenda kuziangalia.

  1. Sting
  2. Interger
  3. Float
  4. Boolean
  5. Array
  6. Object
  7. NULL

 

1. STRING

String ni mkusanyiko wa herufi ama character. Mfano “hello” “I am a student”. Katika PHP string huwekwa ndani ya alama za semi yaani alama za kunukuu ambazo ni “ “. hata hivyo pia unaweza kuchaguwa eidha utumie alama ya kunukuu moja ama mbili mfano ‘ ’  au “ “. mfano wa string kwa alama moja ‘hello’   mfano wa string kwa alama mbili “hello”. pia string inaweza kuwa na mchanganyiko wa herufi, namba na character nyingine. Angalia mifano hapo chini.

 

2. INTEGER

Aina hii ya data ni zile data zote ambazo ni namba tu. Pia zinatakiwa ziwe namba ambazo hazina desimali. Pia integer zinaweza kuwa nmaba ambazo ni positive ama negative. Kitu cha kuzingatia hapa ni kuwa integer haitakiwi iwe na desimali. Mfano 6353

 

3. FLOAT

Hizi ni data ambazo ni namba zilizo na desimali ama exponent. Mgano 23.9

 

4. BOOLEAN

Hizi ni data ambazo hutumika katika kujaribu hali. Hizi zinaitwa condition test. Bolean zipo katika namna mbili ambazo ni TRUE au FALSE.

 

5. ARRAY

Hizi ni data ambazo zinahifadhi taarifa zaidia ya moja kwenye variable. Kwa mfano inaweza kuzungumzia variable miti kisha ikaendelea kutaja aina za mita ambayo itahusika kwenye variable hiyo moja.

 

6. OBJECT

Object ni aina ya data ambayo inahifadhi taarifa na namna ambavyo taarifa hiyo itachakatwa. Tutajifunza zaidi kwenye masomo yajayo.

 

7. NULL

Katika php data ambayo ni null ni data maalumu ambayo inakuwa na thamani moja tu a,bayo ni NULL. Na variable yake inakuwa tu. N endapo umeweka variable na hukuweka kuwa itafanya nini amba itatoa thamani ya kitu gani, basi automatic variable hii hubadilishwa kuwa NULL.

 

 

JINSI YA KUJUWA AINA YA DATA KATIKA PHP:

Ili uweze kujuwa aina ya data iliyotumika huwa tunatumia var_dump(). hii ni function ambayo hutumika katika kuonyesha aina ya data iliyotumika kwenye php. Angalia mifano hapo chini:-

 

Mfano 1:

<?php

$a = 7635262;

Var_dump ($a);

?>

Hapa utapata matokeo haya int(7635262) hii inamaana kuwa namba hizo ni integer ambayo ndio aina ya data iliyotumika

 

Mfano 2:

<?php

$a = "hello piga *112#";

Var_dump ($a);

?>

 

Hapa iakuletea: string(16) "hello piga *112#" hii inamaana kuwa data nilizotumia kwenye mfano huu ni string, ambazo ni mkusanyiko wa herufi, namba na alama kama * na #. hiyo 16 hapo ina maanisha kuwa string iliyotumika ina character 16.

 

 

Mfano 3:

<?php

$a = 626.9;

Var_dump ($a);

?>

 

Hii itakuletea matokeo: float(626.9) inamaana kuwa aina ya data iliyotumika ni float ambayo ni namba zenye desimali na exponent.

 

Mfano 4:

<?php

$mti = array("mpera", "muembe", "mchungwa", "mlimao");

Var_dump($mti);

?>

 

Hii itakupa matokeo array(4) { [0]=> string(5) "mpera" [1]=> string(6) "muembe" [2]=> string(8) "mchungwa" [3]=> string(6) "mlimao" }  hii inamaana kuwa data iliyotumika ni array ambayo ndani yake kuna string 5.

 

Mfano 5:

<?php

$a = '';

$a = null;

Var_dump($a);

?>

Hii itakupa matokeo kuwa NULL

 

Tutajifunza zaidi katika viindi vijavyo, tutajifunza zaidi juu ya hizi aina za data. Tutaangalia namna ya kutumia string katika uandishi.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email:[email protected]

Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

 

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    





Je una umaswali, maoni ama mapendekezo?
Download App yetu kuwasiliana nasi




Post Nyingine


image PHP level 1 somo la kumi na mbili (12) final
Mafunzo ya php level 1 somo ka 12 mwisho wa mafunzo. Hapa utaona project ambazo unaweza kufanya kutokana na mafunzo haya. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)
somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia. Soma Zaidi...

image PHP level 1 somo la tisa (9).
Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza. Soma Zaidi...

image PHP level 1 somo la tano (5)
Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi Soma Zaidi...

image Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)
hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php. Soma Zaidi...

image Php level 1 somo la saba (7)
Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe. Soma Zaidi...

image PHP level 1 somo la sita (6)
Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP Soma Zaidi...

image PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form. Soma Zaidi...