Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

SOMO LA NNE

TYPE OF DATA IN PHP:

Kabla ya kuendelea mbele zaidi katika somo la PHP sasa kwanza lazima tujuwe aina za data ambazo tunakwenda kuzitumia kwenye php. Kila taarifa tunayotaka kuitumia aka kuionyesha lazima tujuwe ipo katika aina ipi ya data. Hii itakusaidia wewe katika kupanga actions. Pia katika kuweka fomu za madodoso.

 

Kwa ufupi katika php kuna aina kuu 7 za data ambazo tutakwenda kuziangalia.

  1. Sting
  2. Interger
  3. Float
  4. Boolean
  5. Array
  6. Object
  7. NULL

 

1. STRING

String ni mkusanyiko wa herufi ama character. Mfano “hello” “I am a student”. Katika PHP string huwekwa ndani ya alama za semi yaani alama za kunukuu ambazo ni “ “. hata hivyo pia unaweza kuchaguwa eidha utumie alama ya kunukuu moja ama mbili mfano ‘ ’  au “ “. mfano wa string kwa alama moja ‘hello’   mfano wa string kwa alama mbili “hello”. pia string inaweza kuwa na mchanganyiko wa herufi, namba na character nyingine. Angalia mifano hapo chini.

 

2. INTEGER

Aina hii ya data ni zile data zote ambazo ni namba tu. Pia zinatakiwa ziwe namba ambazo hazina desimali. Pia integer zinaweza kuwa nmaba ambazo ni positive ama negative. Kitu cha kuzingatia hapa ni kuwa integer haitakiwi iwe na desimali. Mfano 6353

 

3. FLOAT

Hizi ni data ambazo ni namba zilizo na desimali ama exponent. Mgano 23.9

 

4. BOOLEAN

Hizi ni data ambazo hutumika katika kujaribu hali. Hizi zinaitwa condition test. Bolean zipo katika namna mbili ambazo ni TRUE au FALSE.

 

5. ARRAY

Hizi ni data ambazo zinahifadhi taarifa zaidia ya moja kwenye variable. Kwa mfano inaweza kuzungumzia variable miti kisha ikaendelea kutaja aina za mita ambayo itahusika kwenye variable hiyo moja.

 

6. OBJECT

Object ni aina ya data ambayo inahifadhi taarifa na namna ambavyo taarifa hiyo itachakatwa. Tutajifunza zaidi kwenye masomo yajayo.

 

7. NULL

Katika php data ambayo ni null ni data maalumu ambayo inakuwa na thamani moja tu a,bayo ni NULL. Na variable yake inakuwa tu. N endapo umeweka variable na hukuweka kuwa itafanya nini amba itatoa thamani ya kitu gani, basi automatic variable hii hubadilishwa kuwa NULL.

 

 

JINSI YA KUJUWA AINA YA DATA KATIKA PHP:

Ili uweze kujuwa aina ya data iliyotumika huwa tunatumia var_dump(). hii ni function ambayo hutumika katika kuonyesha aina ya data iliyotumika kwenye php. Angalia mifano hapo chini:-

 

Mfano 1:

<?php

$a = 7635262;

Var_dump ($a);

?>

Hapa utapata matokeo haya int(7635262) hii inamaana kuwa namba hizo ni integer ambayo ndio aina ya data iliyotumika

 

Mfano 2:

<?php

$a = "hello piga *112#";

Var_dump ($a);

?>

 

Hapa iakuletea: string(16) "hello piga *112#" hii inamaana kuwa data nilizotumia kwenye mfano huu ni string, ambazo ni mkusanyiko wa herufi, namba na alama kama * na #. hiyo 16 hapo ina maanisha kuwa string iliyotumika ina character 16.

 

 

Mfano 3:

<?php

$a = 626.9;

Var_dump ($a);

?>

 

Hii itakuletea matokeo: float(626.9) inamaana kuwa aina ya data iliyotumika ni float ambayo ni namba zenye desimali na exponent.

 

Mfano 4:

<?php

$mti = array("mpera", "muembe", "mchungwa", "mlimao");

Var_dump($mti);

?>

 

Hii itakupa matokeo array(4) { [0]=> string(5) "mpera" [1]=> string(6) "muembe" [2]=> string(8) "mchungwa" [3]=> string(6) "mlimao" }  hii inamaana kuwa data iliyotumika ni array ambayo ndani yake kuna string 5.

 

Mfano 5:

<?php

$a = '';

$a = null;

Var_dump($a);

?>

Hii itakupa matokeo kuwa NULL

 

Tutajifunza zaidi katika viindi vijavyo, tutajifunza zaidi juu ya hizi aina za data. Tutaangalia namna ya kutumia string katika uandishi.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email:mafunzo@bongoclass.com

Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

 

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1002

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

PHP level 1 somo la nane (8)
PHP level 1 somo la nane (8)

Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)

Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 2 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 2 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo ya html level ya 1 na hapa tutakwenda sasa kunanza somo letu rasmi, kwani katika somo la kwanza umejifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2  for beginner (html full course for beginners)
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)

Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7
Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7

Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7.

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.

Soma Zaidi...