picha

Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

SOMO LA 7
USER DEFINE PHP FUNCTIONS

Katika somo lililotangulia tumejifunza namna ambavyo unaweza kuweka functions kwenye php. Sasa hapa tutaona kuweka function yako mwenyewe kulingana na matarajio yako.


 

Kanuni
1.Andika neno function mfano function
2.Kisha weka jina la function yako mano function salama
3.Kisha weka mabano () mfano function salamu() mapano haya huitwa curly barce
4.Weka mabano haya {} mfano function salama() {}. Mabano haya huitwa parentheses
5.Ndani ya mabano haya ya pili utaweka code angalia mifano hapo chini
6.Mwisho call function, yaani hapa ndipo utatumia function yako kuleta matokeo. Bila ya call hutaweka kupata matokeo. Kwa mfano salamu(); utaicall kwa kuitaja jina lake kama lilivyo mwanzoni mwa function ilipoanza.


 

Mfano 1
<?php
function salamu (){
echo "Habari Hujambo!!!";
}

salamu();
?>
Hii itakupa matokeo: Habari Hujambo!!!
KUWEKA VARIABLE NDANI YA FUNCTION
Katika function unaweza kuongeza taarifa zaidi, kwa kutumia argument, hizi ni sawa na varable. Na hizi huwekwa kwenye yale mabado ya parenthes (). kwa mfano unataka kuorothesha majina ya watoto ambao mama yao ni mmoja. Badala ya kuandika kila mtoto jina lake na la baba yake. Basi tutatumia function kuandika jina la baba kwa wote mara moja tu. Angalia mfan hapo chini:-


 

Mfano 2:
<?php

function b ($mtoto){
echo "$mtoto Saidi. <br>";
}
b ("Shukuru");
b ("Sikuzani");
b ("Neema");
b ("Pendo");
b ("Tabu");
b ("Subira");
?>

Hii itakupa matokeo
Shukuru Saidi.
Sikuzani Saidi.
Neema Saidi.
Pendo Saidi.
Tabu Saidi.
Subira Saidi.


 

Pia unaweza kutumia variable au argument zaidi ya moja. Kwa mfano unataka kujumlisha namba zaidi ya moja. Kumbuka kutenganisha kwa koma variable moja na nyingine. Unaweza kutumia variable 2 ndani ya mabano ya function. Angalia mfano hapo chini:-


 

Mfano 3:
<?php
function jumlisha($x, $z){
$jumla = $x + $z;
echo "jumla ni:- $jumla";
}
jumlisha(6, 7);
?>

Hii itakupa matokeo
Jumla ni:- 13

Pia tunaweza kupata matokeo ya function kwa kutumia ststement ya return value. Hata hivyo pia unaweza kutumia hii kwa zaidi ya variable mbili na kuendelea. Angalia mfano hapo chini:-


 

Mfano 4

<?php
function zidisha($a, $b, $c){
$jibu = $a * $b * $c;
return $jibu;
}
$return_value = zidisha(2, 3, 4);
echo "majibu ni:- $return_value";
Hii itakupamatokeo: majibu ni:- 24

Pia kwa kutumia function moja unaweza kupata matokeo mengi zaidi. Na hii ndio umuhimu wa kutumia function huna haja ya kukiandika kitu kimoja kila wakati. Angalia mfano hapo chini


 

Mfano 5
<?php
function jumlisha($a, $b){
$c = $a + $b;
return $c;
}
echo jumlisha(5, 2) . "<br>" ;
echo jumlisha(3, 9) . "<br>";
echo jumlisha(100, 101). "<br>";
echo jumlisha(9, 0.4). "<br>";
?>

Hii itakupa matokeo
7
12
201
9.4


 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF Views 1364

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...
Matumizi ya AI yanaathiri uwezo wa ubongo

Hii ni tafiti ambayo itakushangaza, kwa namna ambavyo matumizi ya AI yalivyo na athari kwenye uwezo wa kufikiri

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...