Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.
SOMO LA 7
USER DEFINE PHP FUNCTIONS
Katika somo lililotangulia tumejifunza namna ambavyo unaweza kuweka functions kwenye php. Sasa hapa tutaona kuweka function yako mwenyewe kulingana na matarajio yako.
Kanuni
1.Andika neno function mfano function
2.Kisha weka jina la function yako mano function salama
3.Kisha weka mabano () mfano function salamu() mapano haya huitwa curly barce
4.Weka mabano haya {} mfano function salama() {}. Mabano haya huitwa parentheses
5.Ndani ya mabano haya ya pili utaweka code angalia mifano hapo chini
6.Mwisho call function, yaani hapa ndipo utatumia function yako kuleta matokeo. Bila ya call hutaweka kupata matokeo. Kwa mfano salamu(); utaicall kwa kuitaja jina lake kama lilivyo mwanzoni mwa function ilipoanza.
Mfano 1
<?php
function salamu (){
echo "Habari Hujambo!!!";
}
salamu();
?>
Hii itakupa matokeo: Habari Hujambo!!!
KUWEKA VARIABLE NDANI YA FUNCTION
Katika function unaweza kuongeza taarifa zaidi, kwa kutumia argument, hizi ni sawa na varable. Na hizi huwekwa kwenye yale mabado ya parenthes (). kwa mfano unataka kuorothesha majina ya watoto ambao mama yao ni mmoja. Badala ya kuandika kila mtoto jina lake na la baba yake. Basi tutatumia function kuandika jina la baba kwa wote mara moja tu. Angalia mfan hapo chini:-
Mfano 2:
<?php
function b ($mtoto){
echo "$mtoto Saidi. <br>";
}
b ("Shukuru");
b ("Sikuzani");
b ("Neema");
b ("Pendo");
b ("Tabu");
b ("Subira");
?>
Hii itakupa matokeo
Shukuru Saidi.
Sikuzani Saidi.
Neema Saidi.
Pendo Saidi.
Tabu Saidi.
Subira Saidi.
Pia unaweza kutumia variable au argument zaidi ya moja. Kwa mfano unataka kujumlisha namba zaidi ya moja. Kumbuka kutenganisha kwa koma variable moja na nyingine. Unaweza kutumia variable 2 ndani ya mabano ya function. Angalia mfano hapo chini:-
Mfano 3:
<?php
function jumlisha($x, $z){
$jumla = $x + $z;
echo "jumla ni:- $jumla";
}
jumlisha(6, 7);
?>
Hii itakupa matokeo
Jumla ni:- 13
Pia tunaweza kupata matokeo ya function kwa kutumia ststement ya return value. Hata hivyo pia unaweza kutumia hii kwa zaidi ya variable mbili na kuendelea. Angalia mfano hapo chini:-
Mfano 4
<?php
function zidisha($a, $b, $c){
$jibu = $a * $b * $c;
return $jibu;
}
$return_value = zidisha(2, 3, 4);
echo "majibu ni:- $return_value";
Hii itakupamatokeo: majibu ni:- 24
Pia kwa kutumia function moja unaweza kupata matokeo mengi zaidi. Na hii ndio umuhimu wa kutumia function huna haja ya kukiandika kitu kimoja kila wakati. Angalia mfano hapo chini
Mfano 5
<?php
function jumlisha($a, $b){
$c = $a + $b;
return $c;
}
echo jumlisha(5, 2) . "<br>" ;
echo jumlisha(3, 9) . "<br>";
echo jumlisha(100, 101). "<br>";
echo jumlisha(9, 0.4). "<br>";
?>
Hii itakupa matokeo
7
12
201
9.4
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
Soma Zaidi...Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE
Soma Zaidi...haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.
Soma Zaidi...Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.
Soma Zaidi...haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu.
Soma Zaidi...Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.
Soma Zaidi...Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.
Soma Zaidi...